< Psalms 114 >

1 At the time of the exodus of Israel from Egypt, when the descendants of Jacob left that foreign country,
Wakati Israeli walipotoka Misri, nyumba ya Yakobo kutoka kwa watu wa lugha ngeni,
2 the land of Judah became the Lord's sanctuary, Israel his kingdom.
Yuda alifanywa makao matakatifu ya Mungu, Israeli akawa milki yake.
3 The Red Sea saw them and ran away; the Jordan River retreated.
Bahari ilitazama ikakimbia, Yordani ulirudi nyuma,
4 Mountains jumped in fright like rams, hills startled like lambs.
milima ilirukaruka kama kondoo dume, vilima kama wana-kondoo.
5 Red Sea—why did you run away? Jordan River—why did you retreat?
Ee bahari, ni nini kilichokufanya ukakimbia, nawe, ee Yordani, ukarudi nyuma,
6 Mountains—why did you jump in fright? Hills—why did you startle like lambs?
enyi milima mkarukaruka kama kondoo dume, enyi vilima, kama wana-kondoo?
7 Earth, tremble in the presence of the Lord, tremble in the presence of the God of Jacob!
Ee dunia, tetemeka mbele za Bwana, mbele za Mungu wa Yakobo,
8 He is the one who turned the rock into a pool of water; making water flow from the hard rock.
aliyegeuza mwamba kuwa dimbwi la maji, mwamba mgumu kuwa chemchemi za maji.

< Psalms 114 >