< Psalms 111 >

1 Praise the Lord! I will thank the Lord with all my heart in the congregation of the faithful.
Msifuni Yahwe. Nitamshukuru Yahwe kwa moyo wangu wote katikati ya kusanyiko la wanye haki, na katika mkutano.
2 All the wonderful things the Lord has done are studied by everyone who loves them.
Kazi za Yahwe ni kuu, zikisubiriwa na wale wazitamanio.
3 His majesty and honor are revealed by what he does; his goodness lasts forever.
Kazi yake ni adhama na utukufu, na haki yake yadumu milele.
4 He wants the wonderful things he has done to be remembered; the Lord is gracious and kind.
Hufanya mambo makuu ambayo yatakumbukwa; Yahwe ni mwenye huruma na neema.
5 He feeds those who respect him; he always remembers the agreement he made.
Huwapa chakula wafuasi wake waaminifu. Siku zote atalikumbuka agano lake.
6 He demonstrated to his people the powerful things he could do by giving them the lands of other nations.
Alionesha uweza wa kazi zake kwa watu wake kwa kuwapa urithi wa mataifa.
7 Everything he does can be depended on, and is right; all his commandments are trustworthy.
Kazi za mikono yake ni za kuaminika na haki; maagizo yake yote ni ya kuaminika.
8 They remain rock-solid forever. He was true and right in saying what should be done.
Yamethibitika milele, yamefanywa katika uaminifu na vizuri.
9 He delivered his people. He commanded that his agreement would continue forever. How holy and awesome is his reputation!
Aliwapa ushindi watu wake; aliliteuwa agano lake milele; jina lake ni takatifu na lakutisha.
10 The beginning of wisdom is honoring the Lord. Those who follow what he says do well. He is to be praised forever!
Kumcha Yahwe ni mwanzo wa hekima; wale washikao maagizo yake wana uelewa mzuri. Sifa yake yadumu milele.

< Psalms 111 >