< Psalms 109 >

1 For the music director. A psalm of David. God, the one I praise, please don't remain silent,
Zaburi ya Daudi. Mungu ninaye msifu, usinyamaze kimya.
2 because wicked and deceitful people are attacking me, telling lies about me.
Kwa maana waovu na wadanganyifu wananishambulia; wanazungumza uongo dhidi yangu.
3 They surround me with words of hate, fighting against me for no reason.
Wananizunguka na kusema mambo ya chuki, na wananishambulia bila sababu.
4 I love them, but they respond with hostility towards me, even while I'm praying for them!
Wananilipa kashfa badala ya upendo, lakini mimi ninawaombea.
5 They pay me back with evil instead of good, with hatred instead of love.
Wananilipa uovu badala ya mema, na wanachukia upendo wangu.
6 “Appoint someone wicked over him. Have someone stand as an accuser against him.
Teua mtu mwovu aliye adui zaidi kama watu hawa; teua mshitaki asimame mkono wake wa kuume.
7 When he is judged and sentenced, may he be found guilty. Let his prayers be counted as sins.
Na atakapohukumiwa, aonekane na hatia; maombi yake yachukuliwe kuwa ni dhambi.
8 May his life be short; let someone else take over his position.
Siku zake na ziwe chahe; mamlaka yake na yachukuliwe na mtu mwingine.
9 May his children be left fatherless, and his wife become a widow.
Watoto wake wawe yatima, na mke wake awe mjane.
10 May his children be homeless, wandering beggars, driven from their ruined houses.
Watoto wake wenye kutanga tanga na kuombaomba, wakiondoka katika nyumba zao zilizo haribika na kuomba chakula au pesa kwa wapita njia.
11 May creditors seize all that he owns; may strangers take all that he worked for.
Mdai na achukue vitu vyake vyote amilikivyo; wageni wateke mapato ya kazi yake.
12 May no one be kind to him; may no one take pity on his fatherless children.
Asiwepo mtu yeyote wa kumfanyia wema; mtu yeyote asiwahurumie yatima wake.
13 May his descendants die; may his family name be wiped out in the next generation.
Watoto wake waangamizwe; majina yao na yafutwe katika kizazi kijacho.
14 May the Lord be reminded of the sins of his fathers; may his mother's sins not be blotted out.
Uovu wa baba zake utajwe kwa Yahwe; na dhambi ya mama yake isisahaulike.
15 May their sins be constantly before the Lord; may his name be totally forgotten by people.
Hatia zao na ziwe mbele ya Yahwe siku zote; Yahwe na aiondoe kumbukumbu yao duniani.
16 For he didn't think to be kind to others, instead he harassed and killed the poor, the needy, the brokenhearted.
Yahwe na afanye hivi kwa sababu mtu huyu kamwe hakusumbuka kuonesha uaminifu wa agano wowote, lakini badala yake aliwasumbua wanyonge, wahitaji, na kuwaua walio vunjika moyo.
17 He loved to put a curse on others—let it come back on him. He had no time for blessings—so may he never receive any.
Alipenda kulaani; na imrudie juu yake. Alichukia kubariki; baraka zozote na zisije kwake.
18 He cursed as often as he got dressed. May his curses go into him like the water he drinks, like the olive oil he rubs on his skin that enters his bones.
Alijivika kulaani kana kwamba ni vazi lake, na laana yake iliingia ndani yake kama maji, na kama mafuta mifupani mwake.
19 May his curses stick to him like clothing, may they be pulled tight around him like a belt.”
Laana zake na ziwe kwake kama vazi avaalo kujifunika mwenyewe, na kama mkanda avaao kila siku.
20 May all this be the punishment of the Lord on my enemies, on those who speak evil of me.
Na haya yawe malipo ya mshitaki wangu kutoka kwa Yahwe, ya wale wasemao mambo maovu juu yangu.
21 But treat me well, Lord God, because of your own reputation. Save me because you are faithful and good.
Yahwe Bwana wangu, unishughulikie kwa wema kwa ajili ya jina lako. Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni mwema, uniokoe.
22 For I am poor and needy, and my heart is breaking.
Kwa maana ni mnyonge na muhitaji, na moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.
23 I am fading away like an evening shadow; I am like a locust that is shaken off.
Ninatoweka kama kivuli cha jioni; ninapeperushwa kama nzige.
24 I am so weak from lack of food that my legs give way; my body is just skin and bones.
Magoti yangu ni dhaifu kutokana na kufunga; ninakuwa mwembamba na mifupa.
25 People ridicule me—they look at me and shake their heads!
Nimedharauliwa na washitaki wangu; wanionapo; hutikisa vichwa vyao.
26 Help me, Lord my God; save me because of your trustworthy love.
Nisaidie, Yahwe Mungu wangu; uniokoe kwa uaminifu wa agano lako.
27 May they recognize that this is what you are doing—that you are the one who saves me.
Nao wajue kuwa wewe umefanya haya, kwamba wewe, Yahwe, umetenda haya.
28 When they curse me, you will bless me. When they attack me, you will defeat them. And I, your servant, will be happy.
Ingawa wananilaani, tafadhali unibariki; wanishambuliapo, waaibishwe, lakini mtumishi wako afurahi.
29 May those who accuse me be clothed with disgrace; may they cover themselves with a cloak of shame.
Washitaki wangu na wavishwe kwa aibu; wavae aibu yao kama vazi.
30 But I will keep on thanking the Lord, praising him to everyone around me.
Kwa kinywa changu ninatoa shukrani kuu kwa Yahwe; nitamsifu yeye katikati ya kusanyiko.
31 For he takes a stand to defend the needy, to save them from those who condemn them.
Maana nitasimama mkono wa kuume wa mhitaji, ili nimuokoe dhidi ya wale wanao muhukumu.

< Psalms 109 >