< Psalms 108 >
1 A song. A psalm of David. God, I have complete confidence in you! My whole being sings praises to you!
Wimbo. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
2 Wake up, harp and lyre! I will wake up the dawn!
Amka, kinubi na zeze! Nitayaamsha mapambazuko.
3 I will thank you among the peoples, Lord, I will sing your praises among the nations.
Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
4 For your trustworthy love reaches higher than the heavens, your faithfulness is higher than the clouds.
Kwa maana upendo wako ni mkuu, ni juu kuliko mbingu; uaminifu wako unazifikia anga.
5 God, your greatness is above the highest heavens; and your glory is over all the earth!
Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, utukufu wako na uenee duniani kote.
6 Rescue those you love! Answer us, and save us by your power!
Tuokoe na utusaidie kwa mkono wako wa kuume, ili wale uwapendao wapate kuokolewa.
7 God has spoken from his Temple: “Triumphantly I divide up Shechem, and portion out the Valley of Succoth.
Mungu amenena kutoka patakatifu pake: “Nitaigawa Shekemu kwa ushindi na kulipima Bonde la Sukothi.
8 Both Gilead and Manasseh belong to me. Ephraim is my helmet, and Judah is my scepter.
Gileadi ni yangu, Manase ni yangu, Efraimu ni kofia yangu ya chuma, nayo Yuda ni fimbo yangu ya utawala.
9 I will treat Moab as my washbasin; I will place my sandal on Edom; I will shout in triumph over Philistia.”
Moabu ni sinia langu la kunawia, juu ya Edomu natupa kiatu changu; nashangilia kwa kushindwa kwa Ufilisti.”
10 Who will bring me into the fortified city? Who will lead me into Edom?
Ni nani atakayenipeleka hadi mji wenye ngome? Ni nani atakayeniongoza hadi nifike Edomu?
11 Have you rejected us, God? Won't you go out with our armies?
Ee Mungu, si ni wewe uliyetukataa sisi, na hutoki tena na majeshi yetu?
12 Please give us help against our enemies, for human help is worthless.
Tuletee msaada dhidi ya adui, kwa maana msaada wa mwanadamu haufai kitu.
13 Our strength is in God, and he will crush our enemies.
Kwa msaada wa Mungu tutapata ushindi, naye atawaponda adui zetu.