< Psalms 100 >
1 A psalm of thanksgiving. Everyone on earth shout for joy to the Lord!
Zaburi ya shukrani. Mpigieni Bwana kelele za shangwe, dunia yote.
2 Worship the Lord with gladness; come into his presence with joyful songs!
Mwabuduni Bwana kwa furaha; njooni mbele zake kwa nyimbo za shangwe.
3 Know that the Lord is God! He made us, so we belong to him. We are his people, the flock he cares for.
Jueni kwamba Bwana ndiye Mungu. Yeye ndiye alituumba, sisi tu mali yake; sisi tu watu wake, kondoo wa malisho yake.
4 Go in through his gate with thanks; enter his courts with praise. Thank him; praise him for who he is.
Ingieni malangoni mwake kwa shukrani na katika nyua zake kwa kusifu, mshukuruni yeye na kulisifu jina lake.
5 For the Lord is good. His trustworthy love lasts forever; his faithfulness continues for all generations.
Kwa maana Bwana ni mwema na upendo wake wadumu milele; uaminifu wake unadumu kwa vizazi vyote.