< Proverbs 9 >

1 Wisdom has built her house; she has prepared its seven pillars.
Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo saba kutoka katika miamba.
2 She has slaughtered her animals for meat; she has mixed her wine; and she has set her table.
Ameandaa wanyama wake kwa chakula cha usiku; ameichanganya divai yake; na kuandaa meza yake.
3 She has sent out her servant girls with invitations. She calls out from the highest places of the town,
Amewatuma watumishi wake kupeleka mialiko na kutoka mahali pa juu sana kwenye mji anaita:
4 “Everybody who needs to learn, come and see me!” To people who don't have any sense she says,
“Wale wasiofunzwa waje hapa!” anawaambia wale wasionaufahamu.
5 “Come, eat my food, and drink the wine I have mixed.
Njoo, ule chakula, na unywe divai nimeshaichanganya.
6 Leave your foolish ways and you will live; follow the path that makes sense.”
Acheni njia zenu za kijinga, na mkaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
7 If you correct a mocker all you get are insults; if you argue with the wicked all you get is abuse.
Yeyote amrekebishaye mwenye dhihaka hukaribisha matusi na yeyote anayemshutumu mtu mbaya atapata madhara.
8 So don't argue with mockers or they'll only hate you; argue with the wise and they'll love you.
Usimshutumu mwenye dhihaka, ama atakuchukia; mshutumu mtu mwenye busara, naye atakupenda.
9 Educate the wise and they'll become even wiser; teach those who live right and they will increase their learning.
Mpe mafundisho mtu mwenye busara, naye atakuwa na busara zaidi; mfundishe mtu mwenye haki, naye ataongeza elimu.
10 Honoring the Lord is the beginning of wisdom; knowledge of the Holy One brings insight.
Hofu ya Mungu ni chanzo cha hekima na maarifa ya Mtakatifu ni ufahamu.
11 Through wisdom you'll have many more days, increasing the years of your life.
Maana kwa njia yangu siku zako zitazidishwa na uzima wako utaongezewa miaka.
12 If you are wise, you are the one to profit from it; if you scoff, you alone will have to suffer the consequences.
Kama unahekima, unahekima kwako mwenyewe, lakini ukidharau, utaibeba peke yako.
13 Stupidity is like a loud, ignorant woman who doesn't know anything.
Mwanamke mpumbavu anakelele nyingi- hajafunzwa wala haelewi chochote.
14 She sits at the door of her house, on a seat in the high places of the town,
Anakaa kwenye mlango wa nyumba yake, kwenye kiti cha sehemu ya juu sana ya mji.
15 calling out to those passing by, going about their business,
Anawaita kwa sauti wanaopita karibu, watu wale wanaotembea wima katika njia zao.
16 “Everybody who needs to learn, come and see me!” To people who don't have any sense she says,
Wale ambao hamjafunzwa njoni hapa ndani!” anawaambia wale wasio na akili. “
17 “Stolen water is sweet, and food eaten in secret tastes good!”
Maji ya kuiba ni matamu na mkate unaoliwa kwa siri unapendeza.”
18 But they don't know that the dead are there, that those she's invited are in the depths of the grave. (Sheol h7585)
Lakini hajui kwamba wafu wapo pale, wageni wake wapo kwenye vina vya kuzimu. (Sheol h7585)

< Proverbs 9 >