< Proverbs 7 >
1 My son, accept what I say and value my instructions.
Mwanangu, yatunze maneno yangu na ndani yako udhihifadhi amri zangu.
2 Do what I tell you and you will live. Observe my teachings, valuing them as your main focus in life.
Uzilinde amri zangu ili uishi na uyatunzetu mafundisho yangu kama mboni ya jicho.
3 Tie them to your fingers; write them in your mind.
Uyafunge katika vidole vyako; uyaandike katika kibao cha moyo wako.
4 Tell wisdom, “You're my sister,” and call insight your best friend.
Mwambie hekima, “wewe ni dada yangu,” na ufahamu mwite jamaa yako,
5 They will protect you from the immoral woman, from the prostitute with her seductive words.
ili ujitunze mwenyewe dhidi ya mwanake haramu, dhidi ya mwanamke mgeni mwenye maneno laini.
6 One time I looked through the lattice of the window in my house,
Nilikuwa naangalia kwenye wavu wa dirisha la nyumba yangu.
7 and I saw among the immature young men one who had no sense at all.
Nikawatazama watu mwenye ukosefu wa uzoefu, na miongoni mwa watu vijana nikamwona kijana asiye na akili.
8 He was walking down the street near the corner where she lived and took the road passing her house.
Kijana huyo alishuka mtaani kwenye kona karibu na yule mwanamke, akaenda kwenye nyumba yake.
9 It was at dusk in the evening, as the light was fading and the dark night closed in.
Ilikuwa katika utusiutusi wa siku muda wa jioni, wakati wa usiku na giza.
10 Then out came a woman came to meet him. She was dressed as a prostitute and had deceptive intentions.
Akakutana na yule mwanake, amevaa kama kahaba, katika moyo wa udanyanyifu.
11 (She was loud and provocative, never wanting to stay at home.
Alikuwa na kelele na upotovu; miguu yake haikutulia kwenye masikani.
12 One moment she'd be walking the streets, the next she'd be there in the town squares, loitering at every corner.)
Alielekea mitaani, kisha sehemu ya sokoni, na katika kila upande alisubiri kwa kuviza.
13 She grabbed hold of him and kissed him, and with a bold face she told him,
Basi akamshika na kumbusu, kwa uso wa nguvu akamwambia,
14 “I sacrificed my peace offering today, and paid my vows.
leo nimetoa sadaka yangu ya amani, nimelipa nadhili yangu,
15 That's why I came out to meet you. I was looking for you and now I've found you!
hivyo nilikuja kukutana nawe, kuutafuta uso wako kwa hamu, na sasa nimekupata.
16 My bed is made, covered with colorful linens from Egypt.
Nimeweka matandiko juu ya kitanda changu, kitani za rangi kutoka Misri.
17 I've sprinkled perfume on my bed—myrrh, aloes, and cinnamon.
Kitanda changu nimenyunyizia manemane, udi na mdalasini.
18 Come with me, let's make love until the morning. Let's enjoy one another in our love-making!
Njoo, tunywe tujishibishe kwa upendo wetu hata asubuhi; tupate furaha kuu kwa matendo ya mahaba.
19 My husband isn't home; he's gone on a long trip.
Maana mume wangu hayupo nyumbani kwake; amekwenda safari ya mbali.
20 He took a bag of money with him, and he won't be coming back until the full moon.”
Alichukua mkoba wa fedha; atarudi siku ya mwezi mpevu.
21 She convinced him with all that she said; she seduced him with her smooth talking.
katika maneno yake mengi akamshinda; na kwa midomo yake laini anampotosha.
22 He followed her right away, like an ox to the slaughter. Like a stag that's caught in a snare
Ghafula alimfuata kama maksai anayekwenda kwa mchinjaji, kama ayala aliyekamatwa kwa nguvu,
23 until an arrow pierces its liver, like a bird flying into a trap, he's unaware he will pay with his life.
mpaka mshale upasue ini lake. Alikuwa kama ndege anayekimbili kwenye mtego. Hakujua kuwa itamgharimu maisha yake.
24 So now listen to me, my sons, and pay attention to what I'm saying.
Na sasa, wanangu, nisikilizeni; zingatieni maneno ya kinywa changu.
25 Don't even think about following her. Don't stray down her road.
Moyo wako usiyageukie mapito yake; usipotoshwe katika mapito yake.
26 For she has brought down and destroyed a lot of men; she's killed so many.
Amesababisha watu wengi kuanguka kwa kuwajeruhi; ameua watu wengi.
27 Her house leads to the grave—it goes down to the rooms of death. (Sheol )
Nyumba yake ipo juu ya barabara ya kwenda kuzimu; huelekea chini kwenye vyumba vya mauti. (Sheol )