< Proverbs 29 >
1 Anyone who goes on stubbornly rejecting many warnings will be suddenly destroyed, without hope of healing.
Mtu aliyepokea makaripio mengi lakini anashupaza shingo yake atavunjika ndani ya muda mfupi na hata pona.
2 When good people are in charge, everybody celebrates; but when the wicked rule, everybody groans.
Watenda mema wanapoongezeka, watu wanafurahi, bali wakati mtu mwovu anapotawala, watu huugua.
3 A man who loves wisdom makes his father happy, but one who visits prostitutes throws away his money.
Mwenye kupenda hekima baba yake anafurahi, bali anayeshikamana na makahaba huuharibu utajiri wake.
4 A king who rules justly makes the country secure, but one who asks for bribes will destroy it.
Mfalme huimarisha nchi kwa haki, bali mwenye kudai rushwa huirarua.
5 Those who flatter their friends lay a net to trip them up.
Mtu anayejipendekeza kwa jirani yake anatandaza wavu kwenye miguu yake.
6 Evil people are trapped by their own sins, but those who do right sing and celebrate.
Mtu mbaya hunaswa kwenye mtego wa dhambi yake mwenyewe, bali yeye atendaye haki huimba na kufurahi.
7 Good people care about treating the poor fairly, but the wicked don't think about it at all.
Atendaye haki hutetea madai ya masikini; mtu mwovu hafahamu maarifa kama hayo.
8 Cynical people can inflame a whole city, but the wise calm angry people down.
Mwenye dhihaka huutia moto mji, bali wale wenye busara huigeuza ghadhabu.
9 When a wise man takes a stupid man to court, there's raging and ridicule, but nothing is settled.
Mtu mwenye busara anapojadiliana na mpumbavu, hughadhabika na kucheka, hakutakuwa na utulivu.
10 Murderers hate people of integrity, but those who live right try to help them.
Mkatili humchukia mwenye ukamilifu na hutafuta maisha ya mwenye haki.
11 Stupid people let all their anger out, while wise people quietly hold it in.
Mpumabavu huonyesha hasira yake, bali mtu mwenye busara huishikilia na kujituliza mwenyewe.
12 A ruler who listens to lies will have nothing but wicked officials.
Kama matawala atazinagatia uongo, maafisa wake wote watakuwa waovu.
13 Poor people and their oppressors have this in common: the Lord gives life to all of them.
Mtu masikini na mkandamizaji wanafanana, maana Yehova huyapa nuru macho yao wote.
14 If a king judges the poor fairly, he will have a long rule.
Kama mfalme atamhukumu masikini kwa uaminifu, kiti chake cha enzi kitaimarishwa milele.
15 Discipline and correction provide wisdom, but a son left undisciplined is an embarrassment to his mother.
Fimbo na maonyo huleta hekima, bali mtoto huru mbali na makaripio humwaibisha mama yake.
16 When the wicked are in power, sin increases; but the good will see their downfall.
Watu waovu wanapotawala, uovu huongezeka, bali wenye kutenda haki wataona anguko la watu waovu.
17 Discipline your children and they won't give you any worries; they will make you very happy.
Mwadibishe mwanao naye atakupa pumziko; ataleta furaha katika maisha yako.
18 Without a revelation from God, the people go out of control, but those who keep the law are happy.
Pasipo na maono ya kinabii watu huenda bila utaratibu, bali mwenye kuitunza sheria amebarikiwa.
19 A servant can't be disciplined by words alone; though they understand, they don't follow what they're told.
Mtumwa hawezi kurekebishwa kwa maneno, maana ingawa anaelewa, hakuna mwitikio.
20 Have you seen a man who speaks without thinking? There's more hope for stupid people than for him!
Je unamwona mtu mwenye haraka katika maneno yake? Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.
21 A servant indulged from childhood will in the end become unmanageable.
Mwenye kumdekeza mtumwa wake tangu ujana, mwisho wake itakuwa taabu.
22 Angry people stir up trouble, those with short tempers commit many sins.
Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi na bwana mwenye hasira sana hutenda dhambi nyingi.
23 If you're proud, you'll be humiliated; but if you're humble, you'll be honored.
Kiburi cha mtu humshusha chini, bali mwenye roho ya unyenyekevu atapewa heshima.
24 A thief's partner hates his life; even under the threat of being cursed he can't tell the truth.
Anayeshirikiana na mwizi huyachukia maisha yake mwenyewe; husikia laana na wala hasemi chochote.
25 Being afraid of people traps you, but if you trust in the Lord you're safe.
Kumwogopa binadamu ni mtego, bali mwenye kumtumaini Yehova atalindwa.
26 Many people look for favors from a ruler, but justice comes from the Lord.
Wengi huutafuta uso wa mtawala, bali kutoka kwa Yehova huja haki kwa ajili yake.
27 Good people hate those who are unjust; the wicked hate those who do what's right.
Mtu dhalimu ni chukizo kwa wenye kutenda haki, bali mwenye njia ya haki ni chukizo kwa watu waovu.