< Numbers 7 >

1 On the same day that Moses finished putting up the Tabernacle, he anointed it and dedicated it, along with all its furniture, the altar, and all its utensils.
Siku ambayo Musa alikamilsha masikani, alitia mafuta na kuiweka wakfu kwa BWANA, pamoja na mapambo yake. Aliifanyia hivyo madhabahu na vyombo vyake. Aliitia mafuta na kuiweka wakfu kwa BWANA.
2 The Israelite leaders who were the heads of their families came and gave an offering. They were the same leaders of the tribes who had worked on the registration of the Israelites.
Siku hiyo, viongozi wa Israeli na wale vichwa vya familia za mababu walitoa sadaka. Hawa wanaume walikuwa viongozi wa makabila. Walisaidia kuhesabu watu kwenye ile sensa.
3 They brought to the Lord an offering of six covered wagons and twelve oxen. Each leader gave an ox, and two leaders shared in giving a wagon. They presented them in front of the Tabernacle.
Walileta sadaka zao kwa BWANA. Walileta magari sita yaliyofunikwa na mafahari kumi na mbili. Walileta gari moja kwa kila viongozi wawili, kila kiongozi alileta fahari moja. Walileta vitu hivi mbele ya masikani.
4 The Lord told Moses,
Kisha BWANA akanena na Musa, akamwambia,
5 “Accept what they're giving you and use them in the work of the Tent of Meeting. Give them to the Levites to use as required.”
“Uzipokee hizo sadaka kutoka kwao na uzitumie kwa matumizi ya kazi ya hema ya kukutania. Uwape hizo sadaka Walawi, kwa kila mmoja kadri ya uhitaji wa kazi yake.”
6 Moses accepted the wagons and oxen and handed them over to the Levites.
Musa akayatwaa yale magari na mafahari. na kuwapatia Walawi.
7 He gave two wagons and four oxen to the families of Gershon to use as they required.
Aliwapa magari mawili na mafahari wanne wale wa uzao wa Gerishoni, kwa sababu ndivyo kazi yao ilivyohitaji.
8 He gave four wagons and eight oxen to the families of Merari, to use as they required. The work was all to be done under the direction of Ithamar, son of Aaron the priest.
Aliwapatia uzao wa Merari magari manne na mafahari nane, chini ya uangalizi wa Ithamari mwana wa Haruni kuhani. Alifanya hivi kwa sababu ya uhitaji wa kazi yao.
9 He didn't give any wagons or oxen to the Kohathites because their responsibility was to carry on their shoulders the holy objects assigned to their care.
Lakini wale wa uzao wa Kohathi hakuwapa chochote kwa sababu wao waliangalia vitu vtakatifu amabvyo vilipaswa vibebwe mabagani mwao, siyo kwa magari.
10 The day the altar was anointed, the leaders came forward with their dedicatory offerings, presenting them in front of it.
Viongozi walitoa bidhaa zo zingine kwa ajili ya kuwekwa wakfu kwa madhabahu katika siku ile ambayo Musa aliitia mafuta madhabahu. Viongozi walitoa sadaka zao mbele ya madhabahu hiyo.
11 The Lord told Moses, “Have one leader come every day and present his offering for the dedication of the altar.”
BWANA akasema na Musa, “kila kiongozi atatoa sadaka kwa siku yake kwa ajili ya kuiweka wakfu madhabahu.”
12 The first day Nahshon, son of Amminadab, of the tribe of Judah came forward with his offering.
Katika siku ya kwanza, Nashoni mwana wa Aminadabu, wa kabila ya Yuda, alitoa sadaka yake.
13 His offering was a silver plate that weighed a hundred and thirty shekels, and a silver bowl that weighed seventy shekels, (using the sanctuary shekel standard). They were both filled with the best flour mixed with olive oil as a grain offering.
Sadaka yake ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzani wa shekeli 130 na bakuli moja ya fedha ambayo uzito wake ni shekeli sabini, kwa kipimo cha mahali patakatifu. Vyombo vyote hivi vilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga.
14 He also presented a gold dish that weighed ten shekels filled with incense. As sacrifices he brought
Pia alimpa unga wa dhahabu kiasi cha bakuli moja chenye uzani wa shekeli kumi kilichojaa ubani
15 a young bull, a ram, and a one-year-old male lamb as a burnt offering,
Alitoa sadaka ya kuteketezwa fahari mchanga, kondoo dume mmoja na mwanakondoo dume mmoja wa mwaka mmoja.
16 a male goat as a sin offering,
Alitoa beberu kama kama sadaka ya hatia.
17 and a peace offering of two oxen, five rams, five male goats, and five one-year-old male lambs. This was the offering of Nahshon, son of Amminadab.
Alitoa makisai mbili, kondoo waume watano, beberu watano na wanakondoo dume watano wenye umri wa mwaka mmoja mmoja, kama sadaka ya amani. Hii ilikuwa sadaka ya Nashoni mwana wa Aminadabu.
18 The second day Nethanel, son of Zuar, the leader of the tribe of Issachar, came forward.
Siku ya pili, Nethanel mwana wa Zuari, kiongozi wa Isakari, alitoa sadaka yake.
19 The offering he presented was a silver plate that weighed a hundred and thirty shekels, and a silver bowl that weighed seventy shekels, (using the sanctuary shekel standard). They were both filled with the best flour mixed with olive oil as a grain offering.
Sadaka yake ilikuwa sahani moja ya fedha ya uzito wa shekeli130 na bakuli moja la fedha lenye uzani wa sheli sabini, kwa kipimo cha mahali patakatifu. Viyombo vyote hivi vilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kwa sadaka ya unga.
20 He also presented a gold dish that weighed ten shekels filled with incense. As sacrifices he brought
Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu chenye uzito wa shekeli kumi, iliyojaa ubani.
21 a young bull, a ram, and a one-year-old male lamb as a burnt offering,
Alitoa sadaka ya kuteketezwa fahari mchanga, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo mmoja dume.
22 a male goat as a sin offering,
Alitoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi.
23 and a peace offering of two oxen, five rams, five male goats, and five year-old male lambs. This was the offering of Nethanel, son of Zuar.
Alitoa makisai wawili, Kondoo dume watano, beberu watano, na wanakondoo dume watano wa mwaka mmoja mmoja kuwa sadaka ya amani. Hiii likuwa sadaka ya Nethaneli mwana wa Zuari.
24 The third day Eliab, son of Helon, the leader of the tribe of Zebulun, came forward.
Siku ya tatu, Eliabu mwana wa Heloni, kiongozi wa uzao wa Zabuloni alitoa sadaka yake.
25 The offering he presented was a silver plate that weighed a hundred and thirty shekels, and a silver bowl that weighed seventy shekels, (using the sanctuary shekel standard). They were both filled with the best flour mixed with olive oil as a grain offering.
Sadaka yake ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzani wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha lenye uzito wa shekeli sabini kwa kipimo cha shekeli za mahali patakatifu. vyombo vyote hivi vilikuwa vimeja unga mwembemba uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga.
26 He also presented a gold dish that weighed ten shekels filled with incense. As sacrifices he brought
Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu chenye uzani wa shekeli kumi, kilichojaa ubani.
27 a young bull, a ram, and a one-year-old male lamb as a burnt offering,
Alitoa sadaka ya fahari mchanga, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo dume mmoja.
28 a male goat as a sin offering,
Alitoa beberu mmoja kama sadaka ya dhambi.
29 and a peace offering of two oxen, five rams, five male goats, and five year-old male lambs. This was the offering of Eliab, son of Helon.
Alitoa makisai wawili, kondoo dume watano, beberu watano, na wanakondoo dume watano wa mwaka mmoja mmoja. kuwa sadaka ya amani. Hii ilikuwa sadaka ya Eliabu mwana Heloni.
30 The fourth day Elizur, son of Shedeur, the leader of the tribe of Reuben, came forward.
Siku ya nne, Elizuri mwana wa shedeuri, kiongozi wa uzao wa Reubeni, alitoa sadaka yake.
31 The offering he presented was a silver plate that weighed a hundred and thirty shekels, and a silver bowl that weighed seventy shekels, (using the sanctuary shekel standard). They were both filled with the best flour mixed with olive oil as a grain offering.
Sadaka yake ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzani wa shekeli 130 na bakuli moja la fedha lenye uzani wa shekeli sabini, kwa kipimo cha shekeli za mahali patakatifu. Vyombo hivi vyote vilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga.
32 He also presented a gold dish that weighed ten shekels filled with incense. As sacrifices he brought
Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu chenye uzani wa shekeli kumi, kilichoo jaa ubani.
33 a young bull, a ram, and a one-year-old male lamb as a burnt offering,
Alitoa sadaka ya kuteketezwa fahari mmoja mchanga, mwanakondoo dume mmoja mchanga wa mwaka mmoja.
34 a male goat as a sin offering,
Alitoa beberu moja kuwa sadaka ya dhambi.
35 and a peace offering of two oxen, five rams, five male goats, and five year-old male lambs. This was the offering of Elizur, son of Shedeur.
Alitoa maksai wawili, kondoo dume watano wa mwaka mmoja kuwa sadaka ya amani. Hii ilikuwa sadaka ya Elizuri mwana wa Shedeuri.
36 The fifth day Shelumiel, son of Zurishaddai, the leader of the tribe of Simeon, came forward.
Siku ya tano, Shelumieli mwana wa Zurishadai, kiongozi wa uzao wa Simeoni, alitoa sadaka yake.
37 The offering he presented was a silver plate that weighed a hundred and thirty shekels, and a silver bowl that weighed seventy shekels, (using the sanctuary shekel standard). They were both filled with the best flour mixed with olive oil as a grain offering.
Sadaka yake ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzani wa shaekali 130 na bakuli mojala fedha lenye uzani wa shekeli sabini kwa kipimo cha shekeli za mahali patakatifu. Vyombo vyote hivi vilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga.
38 He also presented a gold dish that weighed ten shekels filled with incense. As sacrifices he brought
Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu chenye uzani wa shekeli kumi, uliojaa ubani.
39 a young bull, a ram, and a one-year-old male lamb as a burnt offering,
Alitoa sadaka ya kuteketezwa fahari mchanga, dume la kondoo, na dume la mwanakondoo la mwaka mmoja.
40 a male goat as a sin offering,
Alitoa beberu moja kuwa sadaka ya dhambi.
41 and a peace offering of two oxen, five rams, five male goats, and five year-old male lambs. This was the offering of Shelumiel, son of Zurishaddai.
Alitao maksai wawili, dume wawili wa kondoo, beberu watano, na dume watano wa wanakondoo wa mwaka mmoja mmoja kuwa sadaka y amani. Hiindiyo iliyokuwa sadka ya Shelumei mwana wa Zurishadai.
42 The sixth day Eliasaph, son of Deuel, the leader of the tribe of Gad, came forward.
Siku ya sita, Eliasafu mwana wa Deuli, kiongozi wa uzao wa Gadi, alitoa sadaka yake.
43 The offering he presented was a silver plate that weighed a hundred and thirty shekels, and a silver bowl that weighed seventy shekels, (using the sanctuary shekel standard). They were both filled with the best flour mixed with olive oil as a grain offering.
Sadaka yake ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzani wa shekeli 130 na bakuli la shaba lenye uzani wa shekeli sabini, kwa kipimo cha shekeli za mahali patakatifu. Vyombo hivi vyote vilikuwa vimejaa unga mwembemba uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya sadaka ya unga.
44 He also presented a gold dish that weighed ten shekels filled with incense. As sacrifices he brought
Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu chenye uzani wa shekeli kumi, kilichojaa ubani.
45 a young bull, a ram, and a one-year-old male lamb as a burnt offering,
Alitoa sadaka ya kuteketezwa ya fahari changa, kondoo dume mmoja, na dume la mwanakondoo mmoja wa mwaka mmoja.
46 a male goat as a sin offering,
Alitoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi.
47 and a peace offering of two oxen, five rams, five male goats, and five year-old male lambs. This was the offering of Eliasaph, son of Deuel.
Alitoa maksai wawili, dume watano wa kondoo, beberu watano, na wanakondoo dume watano wa mwaka mmoja kuwa sadaka ya amani. Hii ndiyo iliyokuwa sadaka ya Eliasafu mwana wa Deuli.
48 The seventh day Elishama, son of Ammihud, the leader of the tribe of Ephraim, came forward.
Siku ya saba, Elishama mwana wa Amihudi, kiongozi wa uzao wa Efraimu, alitoa sadaka yake.
49 The offering he presented was a silver plate that weighed a hundred and thirty shekels, and a silver bowl that weighed seventy shekels, (using the sanctuary shekel standard). They were both filled with the best flour mixed with olive oil as a grain offering.
Sadaka yake ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzani wa shekeli 130 na bakuli la fedha lenye uzani wa shekeli sabini, kwa kipimo cha shekeli za mahali patakatifu. Vyombo hivi vyote ilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga.
50 He also presented a gold dish that weighed ten shekels filled with incense. As sacrifices he brought
Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu, kilichojaa ubani
51 a young bull, a ram, and a one-year-old male lamb as a burnt offering,
Alitoa sadaka ya kuteketezwa, fahari mmoja, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo dume mmoja wa mwaka mmoja.
52 a male goat as a sin offering,
Alitoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi.
53 and a peace offering of two oxen, five rams, five male goats, and five year-old male lambs. This was the offering of Elishama, son of Ammihud.
Alitoa maksai wawili, kondo dume watano, beberu watano, na na wanakondoo dume watano wa mwaka mmoja mmoja kuwa sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sdaka ya Elishama mwana wa Amidu.
54 The eighth day Gamaliel, son of Pedahzur, the leader of the tribe of Manasseh, came forward.
Siku y a nane, Gamaliel mwana wa Pedazuri, kiongozi wa uzao wa Manase, alitoa sadaka yake.
55 The offering he presented was a silver plate that weighed a hundred and thirty shekels, and a silver bowl that weighed seventy shekels, (using the sanctuary shekel standard). They were both filled with the best flour mixed with olive oil as a grain offering.
Sadaka yake ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzani wa shekeli130 na bakuli moja la fedha lenye uzani wa shekeli sabini, kwa kipimo cha shekeli za mahali patakatifu. Vyombo vyote hivi vilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga.
56 He also presented a gold dish that weighed ten shekels filled with incense. As sacrifices he brought
Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu chenye uzani wa shekeli kumi, kilichojaa ubani.
57 a young bull, a ram, and a one-year-old male lamb as a burnt offering,
Alitoa sadaka ya kuteketezwa ya fahari mmoja, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo dume mmoja wa mwaka mmoja.
58 a male goat as a sin offering,
Alitoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi.
59 and a peace offering of two oxen, five rams, five male goats, and five year-old male lambs. This was the offering of Gamaliel, son of Pedahzur.
Alitoa maksai wawili, kondoo dume watano, beberu watano, na wanakondoo dume watano wa mwaka mmoja mmoja kuwa sadaka ya amani. Hii ndiyo iliyokuwa sadaka ya Gamaliel mwana wa Pedazuri.
60 The ninth day Abidan, son of Gideoni, the leader of the tribe of Benjamin, came forward.
Siku ya tisa, Abidani mwana wa Gidioni, kiongozi wa uzao wa Benjamini, alitoa sadaka yake.
61 The offering he presented was a silver plate that weighed a hundred and thirty shekels, and a silver bowl that weighed seventy shekels, (using the sanctuary shekel standard). They were both filled with the best flour mixed with olive oil as a grain offering.
Sadaka yake ilikuwa sahani moja yafedha yenye uzani wa sheli 130 na bakuli moja la fedha lenye uzito wa shekeli sabini, kwa kipimo cha shekeli za mahali patakatifu. Vyombo vyote hivi vilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga.
62 He also presented a gold dish that weighed ten shekels filled with incense. As sacrifices he brought
Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu chenye uzani wa shekeli kumi, kilichojaa ubani.
63 a young bull, a ram, and a one-year-old male lamb as a burnt offering,
Alitoa sadaka ya kuteketezwa fahari mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo dume mmoja wa mwaka mmoja.
64 a male goat as a sin offering,
Alitoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi.
65 and a peace offering of two oxen, five rams, five male goats, and five year-old male lambs. This was the offering of Abidan, son of Gideoni.
Alitoa makisai wawili, kondoo dume watano, beberu watano, na wanakondoo dume watano kuwa sadaka ya amani. Hii ndiyo iliyokuwa sadaka ya Abidani mwana wa Gidioni.
66 The tenth day Ahiezer, son of Ammishaddai, the leader of the tribe of Dan, came forward.
Siku ya kumi, Ahizeri mwana wa Amishadai kiongozi wa Dani alitoa sadaka yake.
67 The offering he presented was a silver plate that weighed a hundred and thirty shekels, and a silver bowl that weighed seventy shekels, (using the sanctuary shekel standard). They were both filled with the best flour mixed with olive oil as a grain offering.
Alitoa sahani moja ya fedha yenye uzani wa shaekeli 130 na bakuli moja lenye uzani wa shekeli sabini, kwa kipimo cha shekeli za mahali patakatifu. Vyombo vyote hivi vilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga.
68 He also presented a gold dish that weighed ten shekels filled with incense. As sacrifices he brought
Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu chenye uzito wa shekeli kumi, kilichojaa ubani.
69 a young bull, a ram, and a one-year-old male lamb as a burnt offering,
Alitoa sadaka ya kuteketezwa fahari mmoja mchanga, dume moja la kondoo, na dume moja la mwanakondoo wa mwaka mmoja.
70 a male goat as a sin offering,
Alitoa beberu moja kuwa sadaka ya dhambi.
71 and a peace offering of two oxen, five rams, five male goats, and five year-old male lambs. This was the offering of Ahiezer, son of Ammishaddai.
Alitoa maksai wawili, kondoo dume watano, beberu watano, na wanakondoo dume watano wa mwaka mmoja mmoja, kuwa sadaka ya amani. Hii ndiyo iliyokuwa sadaka ya Ahizeri mwana wa Amishadai.
72 The eleventh day Pagiel, son of Ocran, the leader of the tribe of Asher, came forward.
Siku ya kumi na moja. Pagieli mwana wa Okrani kiongozi wa uzao wa Asheri alaitoa sadaka yake.
73 The offering he presented was a silver plate that weighed a hundred and thirty shekels, and a silver bowl that weighed seventy shekels, (using the sanctuary shekel standard). They were both filled with the best flour mixed with olive oil as a grain offering.
Sadaka yake ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzani wa shekeli 130 na bakuli moja la fedha lenye uzani wa shekeli sabani, kwa kipimo cha shekeli ya mahali patakatifu. Vyombo vyote hivi ilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga.
74 He also presented a gold dish that weighed ten shekels filled with incense. As sacrifices he brought
Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu chenye uzani wa shekeli kumi, kilichojaa ubani.
75 a young bull, a ram, and a one-year-old male lamb as a burnt offering,
Alitoa sadaka ya kuteketezwa fahari mmoja mchanga. dume la kondoo moja, dume moja la mwanakondoo wa mwaka mmoja.
76 a male goat as a sin offering,
Alitoa beberu moja kuwa sadaka ya dhambi.
77 and a peace offering of two oxen, five rams, five male goats, and five year-old male lambs. This was the offering of Pagiel, son of Ocran.
Alitoa maksai wawili, dume watano wa kondoo, na wanakondoo dume watano kuwa sadaka ya amani. Hii ndiyo iliyokuwa sadaka ya Pagieli mwana wa Okrani.
78 The twelfth day Ahira, son of Enan, the leader of the tribe of Naphtali, came forward.
Siku ya kumi na mbili., Ahira mwana wa Enani, kiongozi wa uzao wa Naftali, alitoa sadaka yake.
79 The offering he presented was a silver plate that weighed a hundred and thirty shekels, and a silver bowl that weighed seventy shekels, (using the sanctuary shekel standard). They were both filled with the best flour mixed with olive oil as a grain offering.
Sadaka yake ailikuwa sahani moja ya fedha yenye uzani wa shaekeli 130 na bakuli moja la fedha lenye uzani wa shekeli sabini, kwa kipimo cha shekeli za mahali patakatifu. Vyombo vyote hivi vilikuwa vimejaa unga mwembamba ulichanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga.
80 He also presented a gold dish that weighed ten shekels filled with incense. As sacrifices he brought
Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu chenye uzani wa shekeli kumi, kilichojaa ubani.
81 a young bull, a ram, and a one-year-old male lamb as a burnt offering,
Alitoa sadaka ya kuteketezwa fahari mmoja mchanga, dume moja la kondoo, na mwanakondoo dume moja wa mwaka mmoja.
82 a male goat as a sin offering,
Alitoa beberu moja kuwa sadaka ya dhambi.
83 and a peace offering of two oxen, five rams, five male goats, and five year-old male lambs. This was the offering of Ahira, son of Enan.
Alitoa maksai wawili, kondoo dume watano, beberu watano, na wanakondoo dume watano wa mwaka mmoja mmoja kuwa sadaka ya amani. Hii ndiyo iliyokuwa sadaka ya Ahra mwana wa Enani.
84 So on the day the altar was anointed, the dedicatory offerings brought by the Israelite leaders were twelve silver plates, twelve silver bowls, and twelve gold dishes.
Viongozi wa Israeli waliviweka wakfu hivi vitu vyote siku ambayo Musa alimimina mafuta kwenye madhabahu. Waliziweka wakfu zile sahani kumi na mbili za fedha, Bakuli kumi na mbili za fedha, na vijiko kumi na vili vya dhahabu.
85 Each silver platter weighed a hundred and thirty shekels, and each bowl weighed seventy shekels. The total weight of the silver was two thousand four hundred shekels, (using the sanctuary shekel standard).
Zile sahani za fedha kila moja ilikuwa na uzani wa shaekeli 130 na kila bakuli ye fedha ilikuwa na uzani wa shekeli sabini. Vyombo vyote vya fedh vilikuwa na ujumla ya uzani wa shekeli 2, 400, kwa kipimo cha shekeli za mahali patakatifu.
86 The twelve gold dishes filled with incense each weighed ten shekels, (using the sanctuary shekel standard). The total weight of the gold was a hundred and twenty shekels.
Vile vijiko vya dhahabu vilivyokuwa vimejaa ubani, vilikuwa na uzani wa shekeli kumi kila kimoja. Vijiko vyote vya dhahabu vilikuwa na uzani wa shekeli 120.
87 The animals presented as a burnt offering were twelve bulls, twelve rams, and twelve one-year-old male lambs, as well as their grain offerings, and twelve male goats as the sin offering.
Waliwatenga wanyama wote kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, fahari kumi na wawili, kondoo dume kumi na wawili, na wanakondoo dume kumi na wawili wa mwaka mmoja mmoja. Walitoa sadaka yao ya unga. Walitoa beberu kumi na wawili kuwa sadaka ya dhambi.
88 The animals presented as a peace offering were twenty-four bulls, sixty rams, sixty male goats, and sixty one-year-old male lambs. This was the dedicatory offering for the altar once it had been anointed.
Kutokana na ng'ombe zao, walitoa fahari ishirini na nne, kondoo dume sitini beberu sitini, na wanakondoo dume sitini wa mwaka mmoja mmoja kuwa sadaka ya amani. Hii ilikuwa kwa ajiliya kuiweka wafu ile madhabahu baada ya kumiminiwa mafuta.
89 Whenever Moses went into the Tent of Meeting to speak with the Lord, he would hear the voice speaking to him from the atonement cover on the Ark of the Testimony between the two cherubim. This is how the Lord spoke to him.
Musa alipoingia kwenye hema ya kukutania kusema na BWANA, ndipo alipoisikia sauti yake ikisema naye. BWANA alinena naye kutoka juu ya kiti cha rehema kilichokuwa juu ya sanduku la ushahidi, kutoka katikati ya makerubi. Alinena naye.

< Numbers 7 >