< Numbers 4 >

1 The Lord told Moses and Aaron,
BWANA akanena na Musa na Haruni. Akasema,
2 “Register the descendants of Kohath from the tribe of Levi, according to their family and father's line.
Fanya sensa ya uzao waume wa Kohathi kutoka kwa Walawi, kwa kufuata jamaa na na familia za koo.
3 Count men aged thirty to fifty—all who are entitled to do the work of serving in the Tent of Meeting.
Uwahesabu wanaume ambao wana umri wa miaka thelathini hadi miaka hamsini. Hawa wataungana na kundi linalotumika kutoa huduma kwenye hema ya kukutania.
4 This work that they are to do in the Tent of Meetings involves the things that are most holy.
Uzao wa Kohathi watalinda vile vitu vitakatifu zaidi vilivyohifadhiwa kwa ajili yangu katika hema ya kukutania.
5 Whenever you move camp, Aaron and his sons will go in, take down the veil, and place it over the Ark of the Testimony.
Wakati kambi inapojiandaa kusonga mbele, Haruni na wanawe lazima waende hemani, kulishusha pazia linalotenganisha mahali patakatifu na kulifunika sanduku la ushuhuda kwa pazia hilo. Watalifunika hilo sanduku kwa ngozi za pomboo.
6 On top of this they are to put a fine leather covering, spread a cloth of solid blue over it, and then insert its carrying poles.
Watatandika juu yake nguo za rangi ya samawi. Watachomeka hiyo miti ya kubebea.
7 Have them spread a blue cloth over the table of the Presence as well, and put the plates and cups on it, as well as the bowls and jugs for the drink offering. The current bread offering is to stay on it.
Watatandika nguo ya rangi ya samawi kwenye meza ya mikate ya wonyesho. Juu yake wataweka sahani, vijiko, mabakuli na vikombe vya kumiminia. Mikate itakuwepo daima mezani.
8 Over everything they are to spread a crimson cloth, next a fine leather covering, and then insert its carrying poles.
Wataifunika na nguo ya rangi nyekundu na ngozi za pomboo. na kuweka miti ya kubebea.
9 Using a blue cloth, they are to cover the lampstand of light, together with its lamps, wick tongs, and trays, as well as the jars of olive oil used to fill them.
Watachukua nguo ya rangi ya samawi na kukifunika kinara, pamoja na taa zake, na koleo zake, na sahani zake na vikombe vyake vya kuwekea mafuta ya taa.
10 Then have them wrap it together with all its utensils inside a fine leather covering and place it on the carrying frame.
Wataweka kinara na vifaa vyake vikiwa vimefunikwa na ngozi ya pomboo, na wataweka kwenye miti ya kukibebea.
11 They are to spread a blue cloth over the gold altar, cover it with fine leather, and then insert its carrying poles.
Watafunika na nguo ya samawi katika madhabau ya dhahabu. Wataifunika na ngozi za pomboo, na kuweka ile miti ya kubebea.
12 They are to place all the utensils used for the service in the sanctuary in a blue cloth, cover them with fine leather, and place them on the carrying frame.
Watavichukua vyombo vyote vya kazi takatifu na kuvizonga kwenye hiyo nguo ya rangi ya samawi. Watavifunika na ngozi za pomboo na kuviweka hivyo vyombo kwenye miti ya kubebea.
13 Have them clean the ashes from the bronze altar and spread a purple cloth over it,
Watayaondoa majivu kwenye madhabahu na kutandika nguo ya rangi ya zambarau juu yake.
14 and put on it all the equipment used in the services on the altar: the firepans, meat forks, shovels, and sprinkling bowls. Spread over it a fine leather covering and then insert its carrying poles.
Watavieka kwenye miti ya kubebea vyombo vyote wanavyovitumia kwa kazi ya madhabahuni. Vyombo hivi ni vyetezo, majembe, mabakuli na vitu vingine vya madhabahuni. Wataifuniks madhabahu na ngozi za pomboo na kuweka ile miti ya kubebea.
15 Once Aaron and his sons have finished covering these holy things and all the equipment connected with them, when the camp is ready to move, the priests of the Kohath family are to come and carry them. But they are forbidden to touch anything holy, otherwise they'll die. These are their responsibilities for moving the Tent of Meeting.
Wakati Haruni na wanawe walipokuwa wamekamilisha kupafunika mahali patakatifu na vyombo vyote, na kambi itakapoanza kuendelea mbele, ndipo wana wa Kohathi watakapokuja kubeba vitu vya mahali patakatifu. Kama watagusa vyombo vitakatifu, lazima watakufa. Hii ni kazi ya wana wa uzao wa Kohathi, kubeba mapambo ya hema ya kukutania.
16 Eleazar, son of Aaron the priest, is to supervise obtaining olive oil for the lamps, the aromatic incense, the daily grain offering, and the anointing oil. He is in charge of the whole Tabernacle and everything in it—all the holy things and equipment.”
Eliazari mwana wa Haruni kuhani atalinda na kusimamia mafuta ya taa, ubani mzuri, sadaka za mara kwa mara na mafuta ya upako. Atasimamia ulinzi wa hema lote na vyote vilivyomo, mahali patakatifu na vyombo vyake.”
17 The Lord told Moses and Aaron,
BWANA akanena na Musa na Haruni. Akasema,
18 “Make sure the families of Kohath are not wiped out from the Levites.
Usiruhusu kabila la Wakohathi kuondolewa kati ya Walawi.
19 This is what you have to do so that they'll live and won't die by getting too close to something holy. Aaron and his sons must go in and tell each of them what they have to do and what they have to carry.
Walinde waishi ili wasije wakafa, kwa kufanya hivi. Wanapokuwa wanasogelea
20 But they must not to go in and look at the things that are most holy, even for just a moment, otherwise they'll die.”
wasije wakaingia ndani ili kuona eneo takatifu hata kwa kitambo, vinginevyo watakufa. Bali Haruni na wanawe wanaweza kuingia, ndipo Haruni na Wanawe watakapowapangia Wakohathi kazi maalumu ya kufanya, kwa kila mmoj.”
21 The Lord told Moses,
BWANA akanena na Musa tena, Akasema, “Fanya sensa kwa wana Gerishoni pia, kwa kufuata familia za mababu zao, koo zao.
22 “Register the descendants of Gershon, according to their family and father's line
Uwahesabu wale wenye umri wa mika thelathini hadi miaka hamsini.
23 Count men aged thirty to fifty—all who are entitled to do the work of serving in the Tent of Meeting.
Uwahesabu wote ili waje kuungana na wale wanaotumika katika hema ya kukutania.
24 This is how the families of Gershon will serve in terms of working and carrying:
Hii ndiyo itakuwa kazi ya koo za Gerishoni, wanapotumikia na wanachobeba.
25 Have them carry the Tabernacle curtains, the Tent of Meeting with its fine leather covering, the curtains for the entrance to the Tent of Meeting,
Watabeba pazia la masikani, hema la kukutania, na vifunikio vyake, vifuniko vya ngozi ya pomboo ambvyo viko juu yake, na pazia kwenye lango la hema ya kukutania.
26 the courtyard curtains, the curtain at the entrance to the courtyard surrounding the Tabernacle and altar, the ropes, and everything connected with their use. The families of Gershon are responsible for everything required involving these items.
Watabeba pazia la ua, pazia la kwenye mlango wa ua, ambao uko karibu na maskani karibu na madhabahu, kamba zake na vifaa vyote vya utumishi wake. Chochote kinachotakiwa kufanywa kutokana na vitu hivi, wao ndio watakaofanya.
27 All that they do is to be under the supervision of Aaron and his sons—all their work and carrying assignments. You are to tell them all they are required to carry.
Haruni na wanawe ndio watakaongoza utumishi wa uzao wa Wagerishoni, kwa vitu vyote vile vya kusafirisha, na katika utumishi wao wote. Lazima uwagawie majukumu yao yote.
28 These are their responsibilities for moving the Tent of Meeting, carried out under the direction of Ithamar, son of Aaron the priest.
Huu ndio utumishi wa koo za uzao wa wana wa Wagerishoni katka hema ya kukutania. Ithamari mwana wa Haruni kuhani atawaongoza katika utumishi.
29 Register the descendants of Merari, according to their family and father's line.
Utawahesabu uzao wa Merari kwa koo zao, na uwapange katika familia za mabau zao,
30 Count men aged thirty to fifty—all who are entitled to do the work of serving in the Tent of Meeting.
kuanzia wenye umri wa miaka thelatini hadi miaka hamsini. Umuhesabu kila atakayeungana na kundi lenye utumishi katika hema ya kukutania.
31 This is how they will serve in handling the Tent of Meeting: they are to carry the frames of the Tabernacle with its crossbars, posts, and stands,
Huu ndio wajibu na kazi yao katika utumishi wao kwenye hema ya kukutania. Watazilinda mbao za maskani, mataluma yake, nguzo na makalishio yake,
32 the posts of the surrounding courtyard with their stands, tent pegs, and ropes, all their equipment and everything connected with their use. You are to tell them by name what they are responsible for carrying.
pamoja na nguzo za ua zinazozunguka masikani, makalishio yake, vigingi na kamba zake, na vifaa vinginevya ujenzi. Waorodheshe kwa majina na majukumu yao.
33 These are their responsibilities for all their work in moving the Tent of Meeting, carried out under the direction of Ithamar, son of Aaron the priest.”
Huu ndio utumishi wa koo za uzao wa Merari, ambao wanatakiwa kufanya katika hema ya kukutania, chini ya uongozi wa Ithmari mwana wa Haruni kuhani.”
34 Moses, Aaron, and the Israelite leaders registered the families of Kohath according to their family and father's line.
Musa na Haruni na viongozi wa watu waliwahesabu wana wa uzao wa Wakohathi kwa kufuata koo za familia za mababu zao.
35 They counted men aged thirty to fifty—all who were entitled to do the work of serving in the Tent of Meeting.
Waliwahesabu wale wenye umri wa miaka thelathini hadi miaka hamsini. Walimhesabu kila mmoja aliyepaswa kuungana na kundi linalotoa huduma ya utumishi kwenye hema ya kukutania.
36 The total by families was 2,750.
Waliwahesabu wanaume 2, 750 kwa kufuata koo zao.
37 This was the total of the families of Kohath—all who were entitled to do the work of serving in the Tent of Meeting. Moses and Aaron registered them in accordance with the Lord's instructions to Moses.
Musa na Haruni waliwahesabu wanaume wote kutoka koo na familia za Wakohathi ambao hutumika kwenye hema ya kukutania. Walifanya hivi kwa kumtii BWANA aliyewaagiza kupitia kwa Musa.
38 The families of Gershon were counted, according to their family and father's line,
Uzao wa Gerishoni walihesabiwa kufuata koo na familia za mababu zao,
39 men aged thirty to fifty—all who were entitled to do the work of serving in the Tent of Meeting.
kuanzia umri wa miaka thelathini hadi miaka hamsini, kwa kila mmoja aliyetakiwa kuungana na watu wanaotoa huduma kwenye hema ya kukutania.
40 The total by families and father's line was 2,630.
Wanaume wote waliohesabiwa kufuata koo na familia za mababu zao walikuwa 2, 630.
41 This was the total of the families of Gershon —all who were entitled to do the work of serving in the Tent of Meeting. They were registered by Moses and Aaron in accordance with the Lord's instructions.
Musa na Haruni walizihesabu koo za uzao wa Gerishoni ambao watatumika kwenye hema ya kukutania. Walifanya hivi ili kutii ambacho BWANA aliwaamuru kufanya kuptia kwa Musa.
42 The families of Merari were counted, according to their family and father's line,
Uzao wa Merari walihesabiwa kwa koo kupitia familia za mababu zao,
43 men aged thirty to fifty—all who were entitled to do the work of serving in the Tent of Meeting.
kuanzia wenye umri wa miaka thelathini hadi miaka hamsini, kila anayepaswa kuungana na watu wanaotumika kwenye hema ya kukutania.
44 The total by families was 3,200.
Wanaume wote waliohesabiwa kupitia koo za familia za mababu zao walikuwa 3. 200.
45 This was the total of the families of Merari registered by Moses and Aaron in accordance with the Lord's instructions.
Musa na Haruni waliwahesabu wanaume hawa, uzao wa Merari. Kw kufanya hivi walitii amri ya BWANA aliyowaaagiza kufanya kupitia kwa Musa.
46 This is how Moses, Aaron, and the Israelite leaders registered all the Levites according to their family and father's line.
Kwa hiyo Musa na Haruni na viongozi wa Israeli waliwahesabu Walawi wote kw kufuata koo na familia za mababu zao
47 They counted men aged thirty to fifty—all who were entitled to do the work of serving in the Tent of Meeting and carrying it.
kuanzia wenye umri wa miaka thelathini hadi miaka hamsini. walimhesabu kila aliyepaswa kufanya kazi kwenye masikani, na kila aliyepaswa kubeba na kulinda vitu vya kwenye hema ya kukutania.
48 The sum total was 8,580.
Waliwahesabu wanaume 8, 580.
49 It was in response to the Lord's instructions that they were registered by Moses. Each of those registered were told what to do and what to carry, as the Lord had ordered Moses.
Kwa agizo la BWANA, Musa alimhesabu kila mwanamume na kutunza kumbukumbu ya kazi ambayo kila mmoja anaweza kufanya. Kwa hivyo, walitii kile ambacho BWANA alikuwa amewaagiza kufanya kupitia kwa Musa.

< Numbers 4 >