< Numbers 3 >
1 This is the account concerning Aaron and Moses when the Lord spoke to Moses on Mount Sinai.
Hii ni hesabu ya jamaa ya Aroni na Mose kwa wakati ambao Bwana alizungumza na Mose katika Mlima Sinai.
2 The names of the sons of Aaron were: Nadab (firstborn), Abihu, Eleazar, and Ithamar.
Majina ya wana wa Aroni yalikuwa: Nadabu mzaliwa wa kwanza na Abihu, Eleazari na Ithamari.
3 These were the names of Aaron's sons who were anointed and ordained to serve as priests.
Hayo yalikuwa majina ya wana wa Aroni, makuhani wapakwa mafuta, waliokuwa wamesimikwa kuhudumu kama makuhani.
4 Nadab and Abihu died in the Lord's presence when they offered forbidden fire before the Lord in the Sinai desert. Since they didn't have any sons, Eleazar and Ithamar served as priests while their father Aaron was alive.
Hata hivyo Nadabu na Abihu walikufa mbele za Bwana walipotoa sadaka kwa moto usioruhusiwa mbele zake katika Jangwa la Sinai. Hawakuwa na wana; kwa hiyo Eleazari na Ithamari walihudumu peke yao kama makuhani wakati wote wa maisha ya Aroni baba yao.
6 “Gather the tribe of Levi together and present them to Aaron the priest to help him with the ministry.
“Walete watu wa kabila la Lawi mbele ya Aroni kuhani ili wamsaidie.
7 They are to carry out duties on his behalf and for all the Israelites at the Tent of Meeting, looking after the service of the Tabernacle.
Watafanya huduma kwa ajili yake na kwa jumuiya yote katika Hema la Kukutania kwa kufanya kazi za Maskani.
8 They are responsible for caring for all the furniture of the Tent of Meeting, serving the Israelites through what they do in the Tabernacle.
Watatunza samani zote za Hema la Kukutania, wakitimiza wajibu wa kuhudumia Waisraeli kwa kufanya kazi ya Maskani.
9 The Levites are to work exclusively for Aaron and his sons of because this is their assignment among the Israelites.
Wakabidhi Walawi kwa Aroni na wanawe; hao ndio Waisraeli ambao wanakabidhiwa kwake kabisa.
10 You are to appoint Aaron and his sons to have the responsibility of the priesthood. Anyone else who tries to act as a priest must be executed.”
Waweke Aroni na wanawe kuhudumu kama makuhani; mtu mwingine yeyote atakayesogea mahali patakatifu ni lazima auawe.”
12 “I've taken the Levites from the Israelites in place of every one of their firstborn. The Levites belong to me
“Nimewatwaa Walawi kutoka miongoni mwa Waisraeli badala ya mzaliwa wa kwanza wa kiume wa kila mwanamke wa Mwisraeli. Walawi ni wangu,
13 because all the firstborn are mine. When I killed every firstborn in Egypt I set apart as holy to me all the firstborn of Israel, human and animal. They are mine. I am the Lord.”
kwa kuwa wazaliwa wote wa kwanza ni wangu. Nilipowaua wazaliwa wa kwanza huko Misri, nilimtenga kila mzaliwa wa kwanza katika Israeli awe wangu, akiwa mwanadamu au mnyama. Watakuwa wangu. Mimi ndimi Bwana.”
14 The Lord spoke to Moses in the Sinai desert. He told him,
Bwana akamwambia Mose katika Jangwa la Sinai,
15 “Register the Levites by their father's line and family. Count every male aged one month or older.”
“Wahesabu Walawi kwa jamaa zao na koo zao. Mhesabu kila mwanaume mwenye umri wa mwezi mmoja au zaidi.”
16 So Moses registered them following the Lord's instructions, just as he had been told.
Kwa hiyo Mose akawahesabu, kama alivyoamriwa na neno la Bwana.
17 These were the names of Levi's sons: Gershon, Kohath, and Merari.
Haya yalikuwa majina ya wana wa Lawi: Gershoni, Kohathi na Merari.
18 These were the names of the Gershon's sons by family: Libni and Shimei.
Haya ndiyo yaliyokuwa majina ya koo za Wagershoni: Libni na Shimei.
19 Kohath's sons by family were Amram, Izhar, Hebron, and Uzziel.
Koo za Wakohathi zilikuwa ni: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
20 Merari's sons by family were Mahli and Mushi. These were the families of the Levites, according to their father's line.
Koo za Wamerari zilikuwa ni: Mahli na Mushi. Hizi ndizo zilizokuwa koo za Walawi, kufuatana na jamaa zao.
21 The family of Libni and the family of Shimei came from Gershon. These were the families of Gershon.
Kulikuwa na koo za Walibni na Washimei kwa Gershoni; hizi ndizo zilizokuwa koo za Wagershoni.
22 The total of all males aged one month or older was 7,500.
Idadi ya waume wote waliokuwa na mwezi mmoja au zaidi waliohesabiwa walikuwa 7,500.
23 The camp of families of Gerson was to the west, behind the Tabernacle.
Ukoo wa Wagershoni walitakiwa kuweka kambi zao upande wa magharibi, nyuma ya Maskani.
24 The leader of the Gershon families was Eliasaph, son of Lael.
Kiongozi wa jamaa za Wagershoni alikuwa Eliasafu mwana wa Laeli.
25 Their assigned responsibility for the Tent of Meeting was to take care of the Tabernacle and tent, its covering, the curtain at the entrance of the Tent of Meeting,
Katika Hema la Kukutania, Wagershoni walikuwa na wajibu wa kutunza Maskani na hema, vifuniko vyake, pazia katika mlango wa kuingilia ndani ya Hema la Kukutania,
26 the courtyard curtains, the curtain at the entrance to the courtyard surrounding the Tabernacle and altar, the ropes, and everything connected with their use.
mapazia ya ua, pazia katika ingilio la ua unaozunguka Maskani na madhabahu, pamoja na kamba, na kila kinachohusika kwa matumizi yake.
27 The families of Amram, Izhar, Hebron, and Uzziel came from Kohath. These were the families of Kohath.
Kwa Kohathi kulikuwepo koo za Waamramu, Waishari, Wahebroni na Wauzieli; hizi ndizo zilizokuwa koo za Wakohathi.
28 The total of all males aged one month or older was 8,600. Their assigned responsibility was to take care of the sanctuary.
Hesabu ya waume wote wenye mwezi mmoja au zaidi ilikuwa watu 8,600. Wakohathi waliwajibika kutunza mahali patakatifu.
29 The camp of families of Kohath was on the south side of the Tabernacle.
Koo za Wakohathi zilitakiwa kuweka kambi zao upande wa kusini wa Maskani.
30 The leader of the Kohath families was Elizaphan son of Uzziel.
Kiongozi wa jamaa za koo za Wakohathi alikuwa Elisafani mwana wa Uzieli.
31 Their assigned responsibility was to care for the Ark, the table, the lampstand, the altars, the articles of the sanctuary used with them, the veil, and everything connected with these items.
Waliwajibika kutunza Sanduku la Agano, meza, kinara cha taa, madhabahu, na vile vyombo vya mahali patakatifu vinavyotumika kuhudumu, pazia, na kila kitu kinachohusika na matumizi yake.
32 The chief of the leaders of the Levites was Eleazar, son of Aaron the priest. He was in charge of those responsible for serving in the sanctuary.
Kiongozi mkuu wa Walawi alikuwa Eleazari mwana wa kuhani, Aroni. Aliwekwa juu ya wale waliowajibika kutunza mahali patakatifu.
33 The family of Mahli and the family of Mushi came from Merari. These were the families of Merari.
Kwa Merari kulikuwa na koo za Wamahli na Wamushi; hizi zilikuwa koo za Merari.
34 The total of all males aged one month or older was 6,200.
Hesabu ya waume wote wenye umri wa mwaka mmoja au zaidi waliohesabiwa walikuwa 6,200.
35 The leader of the Merari families was Zuriel, son of Abihail. Their camp was on the north side of the Tabernacle.
Kiongozi wa jamaa za koo za Wamerari alikuwa Surieli mwana wa Abihaili; hawa walitakiwa kuweka kambi zao upande wa kaskazini mwa Maskani.
36 Their assigned responsibility was to take care of the Tabernacle's frames, crossbars, posts, stands, all its equipment, and everything connected with their use,
Wamerari waliwekwa kutunza miimo ya Maskani, mataruma yake, nguzo, vitako na vifaa vyake vyote na kila kitu kilichohusika na matumizi yake,
37 as well as the posts of the surrounding courtyard with their stands, tent pegs, and ropes.
na pia nguzo za ua unaozunguka pamoja na vitako vyake, vigingi vya hema na kamba zake.
38 The camp of Moses, Aaron, and Aaron's sons was to the east of the Tabernacle, in the direction of the sunrise, in front of the Tent of Meeting. They were responsible for the sanctuary on behalf of the Israelites. Anyone else who tried to act as a priest was to be executed.
Mose, na Aroni na wanawe walitakiwa kuweka kambi zao mashariki mwa Maskani, kuelekea mawio ya jua, mbele ya Hema la Kukutania. Wao walihusika na utunzaji wa mahali patakatifu kwa niaba ya Waisraeli. Mtu mwingine yeyote aliyepasogelea mahali patakatifu angeuawa.
39 The sum total of Levites registered by Moses and Aaron as the Lord ordered was 22,000. This included all males aged one month or older.
Jumla ya hesabu ya Walawi waliohesabiwa na Mose na Aroni kwa amri ya Bwana, kufuatana na koo, pamoja na kila mume mwenye umri wa mwezi mmoja au zaidi, walikuwa 22,000.
40 The Lord told Moses, “Conduct a census of all the firstborn Israelite males aged one month or older, and register their names.
Bwana akamwambia Mose, “Wahesabu wazaliwa wa kwanza wa kiume wote wa Waisraeli wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi na uorodheshe majina yao.
41 Assign the Levites to me. I am the Lord. They are in place of all of the Israelites' firstborn children. The livestock of the Levites are in place of all the Israelites' firstborn livestock.”
Nitwalie Walawi badala ya wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli, nayo mifugo ya Walawi badala ya wazaliwa wa mifugo ya Waisraeli. Mimi ndimi Bwana.”
42 Moses conducted a census of all the firstborn of the Israelites, as the Lord had instructed him.
Hivyo Mose akawahesabu wazaliwa wa kwanza wote wa Waisraeli, kama Bwana alivyomwamuru.
43 The sum total of the firstborn males a month old or more, registered by name, was 22,273.
Jumla ya hesabu ya wazaliwa wa kwanza waume wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi, walioorodheshwa kwa majina, walikuwa 22,273.
44 The Lord spoke to Moses and told him,
Bwana akamwambia Mose,
45 “You are to take the Levites in place of all the firstborn children of Israel, and the livestock of the Levites in place of their livestock, because the Levites belong to me. I am the Lord.
“Watwae Walawi badala ya wazaliwa wa kwanza wote wa Israeli, nayo mifugo ya Walawi badala ya mifugo yao. Walawi watakuwa wangu. Mimi ndimi Bwana.
46 In order to buy back the 273 firstborn Israelites who are more than the number of Levites,
Ili kukomboa wazao wa kwanza 273 wa Waisraeli ambao wamezidi hesabu ya Walawi,
47 collect five shekels for each of them, (using the sanctuary shekel standard of twenty gerahs).
kusanya shekeli tano kwa kila mmoja, kufuatana na shekeli ya mahali patakatifu, ambayo ina uzito wa gera ishirini.
48 He handed the money over to Aaron and his sons as the redemption price for the extra Israelites.”
Mpe Aroni na wanawe hizo fedha kwa ajili ya ukombozi wa idadi ya Waisraeli waliozidi.”
49 Moses collected the redemption money for those extra Israelites that were more than the number redeemed by the Levites.
Kwa hiyo Mose akakusanya fedha za ukombozi kutoka kwa wale ambao hesabu yao ilizidi wale waliokombolewa na Walawi.
50 He collected the money given on behalf of the Israelites' firstborn children. It came to 1,365 shekels, (using the sanctuary shekel standard).
Kutokana na wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli alikusanya fedha yenye uzito wa shekeli 1,365 kufuatana na shekeli ya mahali patakatifu.
51 Moses gave this redemption money to Aaron and his sons as the Lord had told him to, following the Lord's instructions.
Mose akampa Aroni na wanawe ile fedha ya ukombozi, kama alivyoamriwa na neno la Bwana.