< Numbers 29 >
1 “Hold a holy meeting on the first day of the seventh month. Don't do any of your normal work. This is the day when you will blow the trumpets.
“‘Katika siku ya kwanza ya mwezi wa saba mtakuwa na kusanyiko takatifu na msifanye kazi ya kawaida. Ni siku kwa ajili yenu ya kupiga tarumbeta.
2 Present a burnt offering of one young bull, one ram, and seven male lambs a year old, all of them without defects, as a sacrifice acceptable to the Lord,
Mtatayarisha sadaka ya kuteketezwa kama harufu nzuri impendezayo Bwana ya fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na wana-kondoo saba wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
3 along with their grain offerings of the best flour mixed with olive oil: three-tenths of an ephah for the bull, two-tenths of an ephah for the ram,
Pamoja na fahali, andaeni sadaka ya nafaka sehemu ya kumi tatu za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; kwa kondoo dume, andaa unga sehemu ya kumi mbili za efa;
4 and one tenth of an ephah for each of the seven male lambs.
na pamoja na wana-kondoo saba kila mmoja aandaliwe na sehemu ya kumi ya efa ya unga.
5 Also present a male goat as a sin offering to make you right.
Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
6 These offerings are in addition to the monthly and daily burnt offerings along with their required grain offerings and drink offerings. They are burnt offerings acceptable to the Lord.
Hivi ni nyongeza ya sadaka za kuteketezwa kila mwezi na kila siku pamoja na sadaka zake za nafaka na sadaka za vinywaji kama ilivyoainishwa. Ni sadaka zinazotolewa kwa Bwana kwa moto, harufu inayopendeza.
7 Hold a holy meeting on the tenth day of this seventh month, and practice self-denial. Don't do any of your normal work.
“‘Kwenye siku ya kumi ya mwezi huu wa saba mtakuwa na kusanyiko takatifu. Mtajikana wenyewe na msifanye kazi.
8 Present a burnt offering of one young bull, one ram, and seven male lambs a year old, all of them without defects, acceptable to the Lord.
Toeni sadaka ya kuteketezwa ya fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na wana-kondoo saba wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari, kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.
9 They are to be accompanied by their grain offerings of the best flour mixed with olive oil: three-tenths of an ephah for the bull, two-tenths of an ephah for the ram,
Pamoja na fahali, andaeni sadaka ya nafaka sehemu ya kumi tatu za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; pamoja na kondoo dume, sehemu ya kumi mbili za efa za unga laini;
10 and one tenth of an ephah for each of the seven lambs.
na kwa kila mmoja wa wana-kondoo saba andaa sehemu ya kumi ya unga laini kwa kila mmoja.
11 Also present a male goat as a sin offering in addition to the sin offering to make you right and the continual burnt offering with its grain offering and drink offering.
Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, katika nyongeza ya sadaka ya dhambi kwa ajili ya upatanisho, na sadaka ya kawaida ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya nafaka, na sadaka zake za vinywaji.
12 Hold a holy meeting on the fifteenth day of the seventh month. Don't do any of your normal work. You are to celebrate a festival dedicated to the Lord for seven days.
“‘Katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa saba, mtakuwa na kusanyiko takatifu, na hamtafanya kazi za kawaida. Adhimisheni sikukuu kwa Bwana kwa siku saba.
13 Present the following as a burnt offering acceptable to the Lord: thirteen young bulls, two rams, and fourteen male lambs a year old, all of them without defects.
Toeni sadaka ya kuteketezwa mafahali wachanga kumi na watatu, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari, kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.
14 They are to be accompanied by their grain offerings of the best flour mixed with olive oil: three-tenths of an ephah of the best flour mixed with olive oil for each of the thirteen bulls, two-tenths of an ephah for each of the two rams,
Pamoja na hao mafahali kumi na watatu, kila mmoja aandaliwe na sadaka ya nafaka sehemu ya kumi tatu za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; kwa kondoo dume wawili, kila mmoja aandaliwe sehemu ya kumi mbili za efa za unga laini;
15 and one tenth of an ephah for each of the fourteen lambs.
na kwa wana-kondoo kumi na wanne, kila mmoja aandaliwe sehemu ya kumi ya efa ya unga laini.
16 Also present a male goat as a sin offering in addition to the continual burnt offering with its grain offering and drink offering.
Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka ya vinywaji.
17 On the second day present twelve young bulls, two rams, and fourteen male lambs a year old, all of them without defects.
“‘Katika siku ya pili andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
18 They are to be accompanied by their grain offerings and drink offerings for the bulls, rams, and lambs, all according to the number required.
Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
19 Also present a male goat as a sin offering in addition to the continual burnt offering with its grain offering and drink offering.
Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
20 On the third day present eleven young bulls, two rams, and fourteen male lambs a year old, all of them without defects.
“‘Katika siku ya tatu andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
21 They are to be accompanied by their grain offerings and drink offerings for the bulls, rams, and lambs, all according to the number required.
Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
22 Also present a male goat as a sin offering in addition to the continual burnt offering with its grain offering and drink offering.
Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
23 On the fourth day present ten young bulls, two rams, and fourteen male lambs a year old, all of them without defects.
“‘Katika siku ya nne andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
24 They are to be accompanied by their grain offerings and drink offerings for the bulls, rams, and lambs, all according to the number required.
Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
25 Also present a male goat as a sin offering in addition to the continual burnt offering with its grain offering and drink offering.
Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
26 On the fifth day present nine young bulls, two rams, and fourteen male lambs a year old, all of them without defects.
“‘Katika siku ya tano andaeni mafahali tisa, kondoo dume wawili na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
27 They are to be accompanied by their grain offerings and drink offerings for the bulls, rams, and lambs, all according to the number required.
Pamoja na mafahali, kondoo dume na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za kinywaji kulingana na idadi iliyoainishwa.
28 Also present a male goat as a sin offering in addition to the continual burnt offering with its grain offering and drink offering.
Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi katika nyongeza ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa na sadaka yake ya nafaka pamoja na sadaka ya kinywaji.
29 On the sixth day present eight young bulls, two rams, and fourteen male lambs a year old, all of them without defects.
“‘Katika siku ya sita andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
30 They are to be accompanied by their grain offerings and drink offerings for the bulls, rams, and lambs, all according to the number required.
Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
31 Also present a male goat as a sin offering in addition to the continual burnt offering with its grain offering and drink offering.
Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
32 On the seventh day present seven young bulls, two rams, and fourteen male lambs a year old, all of them without defects.
“‘Katika siku ya saba andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
33 They are to be accompanied by their grain offerings and drink offerings for the bulls, rams, and lambs, all according to the number required.
Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
34 Also present a male goat as a sin offering in addition to the continual burnt offering with its grain offering and drink offering.
Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
35 On the eighth day all of you are to meet together. Don't do any of your normal work.
“‘Katika siku ya nane mtakuwa na kusanyiko, na msifanye kazi ya kawaida.
36 Present the following as a burnt offering acceptable to the Lord: one bull, two rams, and seven male lambs a year old, all of them without defects.
Toeni sadaka ya kuteketezwa kama harufu nzuri inayompendeza Bwana, sadaka ya kuteketezwa ya fahali mmoja, kondoo dume mmoja, na wana-kondoo dume saba wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
37 They are to be accompanied by their grain offerings and drink offerings for the bulls, rams, and lambs, all according to the number required.
Pamoja na fahali, kondoo dume na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka, na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
38 Also present a male goat as a sin offering in addition to the continual burnt offering with its grain offering and drink offering.
Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, katika nyongeza ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka pamoja na sadaka ya kinywaji.
39 Present these offerings to the Lord at the times you are required to do so, in addition to your offerings to fulfill a promise and freewill offerings, whether they are burnt offerings, grain offerings, drink offerings, or peace offerings.”
“‘Zaidi ya kile unachoweka nadhiri na sadaka zenu za hiari, andaeni hizi kwa ajili ya Bwana kwenye sikukuu zenu zilizoamriwa: sadaka zenu za kuteketezwa, sadaka za nafaka, sadaka za vinywaji, pamoja na sadaka zenu za amani.’”
40 Moses repeated all this to the Israelites as the Lord ordered him to do.
Mose akawaambia Waisraeli yale yote Bwana alimwagiza.