< Numbers 23 >
1 Then Balaam told Balak, “Build seven altars for me here, and prepare seven bulls and seven rams for me to sacrifice.”
Balaamu akamwabia Balaki, “Jenga madhabahu saba kwa ajili yangu na uandae mafahari saba na kondoo dume saba.”
2 Balak did as Balaam had said, and together they offered a bull and a ram on each altar.
Kwa hiyo Balaki akafanya kama Balaamu alivyoomba. Kisha Balaki na Balaamu wakatoa sadaka ya fahari mmoja na kondoo dume mmoja kwa kila madhabahu.
3 Balaam said to Balak, “Wait here beside your burnt offering while I go and see if perhaps the Lord will come and meet with me. Whatever he reveals to me, I'll share with you.” Then Balaam left to climb up a rocky crag.
Ndipo Balaamu alipomwamiba Balaki, “Simama kwenye sadaka yako ya kuteketezwa na mimi nitaenda. Labda BWANA atakuja kukutana na mimi. Chochote atakachoniambia nitakuambia.” Kwa hiyo akaenda juu ya mlima usiokuwa na miti.
4 God met with him there, and Balaam said. “I have built seven altars and on each altar I have offered a bull and a ram.”
Wakati bado akiwa juu ya mlima. Mungu akakutana naye, na Balaamu akamwambia, “Nimejenga madhabahu saba, na nimetoa sadaka ya fahari na kondoo dume kwa kila madhabahu.”
5 The Lord gave Balaam a message to share. He told him, “Go back to Balak and this is what you are to say to him.”
BWANA akaweka ujumbe kwenye kinywa cha Baalamu akasema, “Rudi kwa Balaki ukamwambie.”
6 So he went back to Balak, who was waiting there beside his burnt offering, along with all the Moabite leaders.
Kwa hiyo Balaamu akarudi kwa Balaki aliyekuwa amesimama karibu na sadaka yake ya kuteketezwa, na viongozi wote wa Moabu walikuwa pamoja naye.
7 This is the declaration that Balaam gave: “Balak brought me from Aram; the king of Moab brought me from the mountains of the east. He said, ‘Come and curse Jacob for me! Come and condemn Israel!’
Ndipo Balaamu alipoanza kunena unabii wake akisema, “Balaki amenileta kutoka Aramu, Mfalme wa Moabu kutoka katika milima ya mashariki, 'Njoo, nilaanie Yakobo kwa ajili yangu,' alisema, 'Njoo umtie unajisi Israeli,'
8 But how can I curse what God has not cursed? How can I condemn what the Lord has not condemned?
Nawezaje kuwalaani wale ambao Mungu hajawalaani? Nawezaje kuwapinga wale ambao Mungu hawapingi?
9 For I'm looking down on them from the top of rocky crags; I'm watching them from the hills. I see a people who live on their own, different from the other nations.
Kwa kuwa kutoka juu ya miamba Ninamwona; kutoka kwenye milima ninamtazama. Kuna watu wanaoishi pekee yao na hawajioni wenyewe kama ni taifa la kawaida.
10 Who can count Jacob's descendants? They are so many they're like dust! Who can count even a quarter of the Israelites? I would like to die as a good person dies! Let the end of my life be like their end!”
Nani awezaye kuyahesabu mavumbi ya Yakobo au kuhesabu hata robo ya Israeli? Naomba nife kifo cha mtu mwenye haki, na mwisho wa maisha yangu uwe kama wake!”
11 Then Balak complained to Balaam, “What on earth have you done to me? I brought you here to curse my enemies, and now look! All you have done is bless them!”
Balaki akamwambia Balaamu, “Umenifanyia nini? Nilikuleta ili uwalaani maadui wangu, lakini ona, umewabariki,”
12 But Balaam replied, “Don't you think I should I say precisely what the Lord tells me?”
Balaamu akajibu akasema, “Kwa nini nisiwe mwangalifu kusema kile ambacho BWANA anaweka kinywani mwangu?”
13 Then Balak said to him, “Please come with me to another place where you can see them. But you'll only see a part of their camp—you won't see all of them. You can curse them for me from there.”
Basi Balaki akamwambia, “Hebu uje nami kwenye eneo jingine ili uwaone. Utakaowaona ni wale wa karibu tu, huwezi kuwaona wote. Huko sasa unaweza kunilaania hawa watu.”
14 He took him to the field of Zophim at the top of Mount Pisgah. There he built seven altars and offered a bull and a ram on each altar.
Kwa hiyo akampeleka Balaamu kwenye shamba la Zofimu, lililo juu ya Mlima Pisiga, na kule akajenga madhabau zingine saba. Akatoa sadaka ya fahari mmoja na kondoo dume kwa kila madhabahu.
15 Balaam told Balak, “Wait here beside your burnt offering while I meet the Lord over there.”
Kisha Balaamu akamwambia Balaki, “Simama hapa karibu na sadaka zako, wakati mimi naenda kukutana na BWANA kule.”
16 The Lord met Balaam and gave him a message to share. He told him, “Go back to Balak and this is what you are to say to him.”
Kwa hiyo BWANA akakutana na Balaamu na kumwekea ujumbe kinywani mwake. Alimwambia, “Rudi kwa Balaki ukamwambie huu ujumbe toka kwangu.”
17 So he went back to Balak, who was waiting there beside his burnt offering, along with all the Moabite leaders. “What did the Lord say?” Balak asked.
Balaamu akamrudia, na tazama, alikuwa amesimama karibu na sadaka zake za kuteketezwa, na vionigozi wa Moabu walikuwa pamoja naye. Balaki akamwuliza, “BWANA amekwambiaje?”
18 This is the prophecy that Balaam delivered: “Stand up, Balak, and pay attention! Listen to me, son of Zippor!
Balaamu akaanza kutoa unabii. Akasema, “Inuka, Balaki na usikilize. Nisikilize mimi wewe mwana wa Zippori.
19 God isn't a human being who would lie. He's not a mere mortal who changes his mind. Does he say he's going to do something but doesn't? Does he make promises he doesn't carry out?
Mungu siyo mtu, kwamba umdanganye, au mwanadamu awezaye kubadili mawazo. Je, alishawahi kuahidi kitu pasipo kukitekeleza? Je, alishawahi kusema kuwa atafanya kitu bila kufanya kama alivyosema?
20 Look, I have been ordered to give a blessing. God has blessed, and I can't change that.
Tazama, Mimi nimeamriwa kuwabariki. Mungu ametoa baraka, nami siwezi kuibadilisha.
21 He's not expecting anything bad will happen to Jacob; he doesn't foresee any trouble for Israel. The Lord their God is with them; they celebrate him as their king.
Hajawahi kuona magumu katika Yakobo au tabu katika Israeli. BWANA Mungu wao yuko pamoja nao, na kelele za wafalme wao ziko pamoja nao.
22 God led them out of Egypt with great power, as strong as an ox.
Mungu aliwatoa Misri kwa nguvu kama za nyati.
23 No spell can be cast against Jacob; no magic can be used against Israel. People will talk about Jacob and Israel, saying, ‘What amazing things God has done for them!’
Hakuna uganga utakaofanikiwa dhidi ya Yakobo, na hakuna uchawi utakaomwumiza Israeli. Badala yake, itasemwa juu ya Yakobo na Israeli, 'Tazama kile ambacho Mungu amefanya!'
24 Look! The Israelites go out hunting like a lioness; they chase like a lion. They don't rest until they eat their prey, and drink the blood of their dead victim.”
Tazama, watu wanainuka kama simba jike, kama vile simba ainukavyo na kuvamia. Halali chini mpaka ale windo lake na kunywa damu ya windo lake,”
25 Then Balak said to Balaam, “If you can't give them any curses then at least don't give them any blessings!”
Kisha Balaki akamwambia Balaamu, “Kamwe usiwalaani wala kuwabariki.”
26 But Balaam replied, “Didn't I explain to you that I have to do whatever the Lord tells me?”
Lakini Balaamu akamjibu Balaki, “Sijakuambia kuwa nitasema yote ambayo BWANA ananiambia kusema?
27 “Please come with me and I will take you somewhere else,” Balak said. “Maybe God would let you curse them for me from there.”
Balaki akamwambia Balaamu, “Njoo sasa, Nami nitakupeleka mahali pengine. Labda kule itampendeza Mungu kunilaania hawa hawa watu.”
28 Balak took Balaam to the top of Mount Peor, which looks down on the wastelands.
Kwa hiyo Balaki akampeleka Balaamu juu ya Mlima Peori, ambao unalitazama chini lile jangwa,
29 Balaam told Balak, “Build seven altars for me here, and prepare seven bulls and seven rams for me to sacrifice.”
Balaamu akamwambia Balaki, “Nijengee madhabahu saba hapa na uniandalie mafahari saba na kondoo duume saba.
30 Balak what Balaam told him, and he offered a bull and a ram on each altar.
“Kwa hiyo Balaki akafanya kama alivyoambiwa; akatoa sadaka ya fahari na kondoo mume kwenye kila madhabahu.