< Nehemiah 3 >

1 Eliashib the high priest and other priests with him began rebuilding at the Sheep Gate. They dedicated it and set up its doors. Then they continued building as far as the Tower of the Hundred and the Tower of Hananel and dedicated it.
Kisha Eliashibu, kuhani mkuu, akasimama pamoja na ndugu zake makuhani, wakajenga lango la kondoo. Walitakasa na kuweka milango yake. Waliweka wakfu hadi mnara wa Hamea na hadi mnara wa Hananeli.
2 The men of Jericho built the section next to Eliashib, and Zaccur, son of Imri, built the one after.
Baada yao watu wa Yeriko walijenga, na baada yao Zakuri mwana wa Imri alijenga.
3 The Fish Gate was rebuilt by the sons of Hassenaah. They laid its beams and set up its doors, together with its bolts and bars.
Wana wa Senaa wakajenga lango la samaki. Wanaweka mihimili yake na kuweka milango yake na vyuma vyake na makomeo yake.
4 The next section was repaired by Meremoth, son of Uriah, son of Hakkoz; next to him, was Meshullam, son of Berechiah, son of Meshezabel; and next to him, Zadok, son of Baana.
Meremoth aliandaa sehemu inayofuata. Yeye ni mwana wa Uria mwana wa Hakosi. Na baada yao Meshulamu akatengeneza. Yeye ni mwana wa Berekia mwana wa Meshezabeli. Karibu nao Sadoki akatengeneza. Yeye ni mwana wa Baana.
5 Next were the Tekoites, but their nobles refused to do manual work under a supervisor.
Baada yao Watekoi wakatengeneza, lakini viongozi wao walikataa kufanya kazi iliyoagizwa na wakuu wao.
6 The Old Gate was repaired by Joiada, son of Paseah and Meshullam, son of Besodeiah. They laid its beams and set up its doors, together with its bolts and bars.
Yoyada mwana wa Pasea, na Meshulamu mwana wa Besodeya, walitengeneza lango la Kale. Wanaweka mihimili, na kuweka milango yake na vyuma vyake na makomeo yake.
7 Next were Melatiah the Gibeonite, Jadon the Meronothite, and the men of Gibeon and Mizpah, who were under the jurisdiction of the governor of the province west of the Euphrates.
Nao, Melatia Mgibeoni, na Yadoni Meronothi, watu wa Gibeoni na Mispa, walifanyia matengenezo juu ya sehemu ambapo mkuu wa mkoa wa ng'ambo ya Mto aliishi.
8 Next was Uzziel, son of Harhaiah, one of the goldsmiths; and next to him was Hananiah, son of the perfumer. They strengthened Jerusalem as far as the Broad Wall.
Na baada yake Uzieli mwana wa Harhaya, mmoja wa wafua dhahabu, akatengeneza; na baada yake Hanania, mtengenezaji wa manukato. Wakajenga tena Yerusalemu mpaka Ukuta mpana.
9 Next was Rephaiah, son of Hur, ruler of a Jerusalem half-district.
Na baada yao Refaya mwana wa Huri akajenga. Alikuwa mtawala wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu.
10 Next was Jedaiah, son of Harumaph, who made repairs opposite his house. Next was Hattush, son of Hashabneiah.
Na baada yao Yedaya mwana wa Harumafu akajenga karibu na nyumba yake. Na baada yake Hatushi mwana wa Hashabneya akajenga.
11 Malchijah, son of Harim, and Hasshub, son of Pahath-moab, worked on another section, as well as the Tower of the Ovens.
Malkiya mwana wa Harimu na Hashubu mwana wa Pahat Moabu, wajenga sehemu nyingine pamoja na mnara wa tanuu.
12 Next was Shallum, son of Hallohesh, ruler of a Jerusalem half-district, helped by his daughters.
Baada yao Shalumu mwana wa Haloheshi, mkuu wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu, akajenga, pamoja na binti zake.
13 The Valley Gate was repaired by Hanun and the people who lived in Zanoah. They rebuilt it, set up its doors, together with its bolts and bars, and repaired a thousand cubits of the wall up to the Refuse Gate.
Hanuni na wenyeji wa Zanoa walijenga lango la bondeni. Walijenga tena na kuweka milango yake, na vyuma vyake na makomeo yake. Walijenga dhiraa elfu hadi lango la jaa.
14 The Refuse Gate was repaired by Malchijah, son of Rechab, ruler of the district of Beth-haccherem, He rebuilt it and set up its doors, together with its bolts and bars.
Malkiya, mwana wa Rekabu, mkuu wa wilaya ya Beth-Hakeremu, akajenga lango la jaa. Alijenga na kuweka milango yake, na vyuma vyake na makomeo yake.
15 The Fountain Gate was repaired by Shallun, son of Col-hozeh, ruler of the Mizpah district. He rebuilt it, put a roof on it, set up its doors, together with its bolts and bars. He rebuilt the wall of the Pool of Shelah by the king's garden, as far as the steps that go down from the City of David.
Shalumu mwana wa Kolhoze, mkuu wa wilaya ya Mispa, akajenga lango la Chemchemi. Alijenga, na kuweka kifuniko juu yake na kuweka milango yake na vyuma vyake na makomeo yake. Alijenga upya ukuta wa Pwani wa Silowamu kwa bustani ya mfalme, hadi ngazi ya kuongoza kutoka mji wa Daudi.
16 Past him, Nehemiah, son of Azbuk, ruler of a Beth-zur half-district, repaired up to a point opposite David's cemetery, as far as the man-made pool and the House of the Mighty Warriors.
Nehemia mwana wa Azbuki, mtawala wa nusu ya wilaya ya Beth-suri, akajenga mahali hapo, toka maburini ya Daudi, mpaka birika lililojengwa na watu, na nyumba ya watu wenye nguvu.
17 Next were the Levites under Rehum son of Bani, and next was Hashabiah, ruler of Keilah half-district, who made repairs on behalf of his district.
Baada yake, Walawi walijenga, pamoja na Rehumi mwana wa Bani na baada yake, Hashabia, mtawala wa nusu ya wilaya ya Keila, kwa wilaya yake.
18 Next to them were their neighbors under Binnui, son of Henadad, ruler of the other Keilah half-district.
Baada yake watu wa nchi zao walijenga, ikiwa ni pamoja na Binui mwana wa Henadadi, mkuu wa nusu ya wilaya ya Keila.
19 Next was Ezer, son of Jeshua, ruler of Mizpah, who repaired another section opposite Armory Hill, where the wall turns.
Baada yake alijenga Ezeri, mwana wa Yeshua, mtawala wa Mispa, alijenga sehemu nyingine kuelekea ghala ya silaha, kwenye kona ya ukuta.
20 Next was Baruch, son of Zabbai, who worked hard repairing another section, from where the wall turns to the entrance of Eliashib the high priest's house.
Baada yake Baruki, mwana wa Zakai, akajenga kwa hiari sehemu nyingine, toka kona ya ukuta mpaka mlango wa nyumba ya Eliashibu, kuhani mkuu.
21 Next was Meremoth, son of Uriah, ton of Hakkoz, who repaired another section, from the entrance of Eliashib the high priest's house to its end.
Baada yake Meremothi, mwana wa Uria, mwana wa Hakosi, akajenga sehemu nyingine, toka mlango wa nyumba ya Eliashibu mpaka mwisho wa nyumba ya Eliashibu.
22 Next were the priests from the area around made repairs.
Kisha baada yake makuhani, watu wa eneo hilo karibu na Yerusalemu, walijenga.
23 Past them were Benjamin and Hasshub who made repairs in front of their house, and next to them, Azariah, son of Maaseiah, son of Ananiah, made repairs beside his house.
Baada yao Benyamini na Hashubu walijenga kuielekea nyumba yao. Baada yao Azaria mwana wa Maaseya, mwana wa Anania, alijenga karibu na nyumba yake.
24 Next was Binnui, son of Henadad, who repaired another section, from Azariah's house to where the wall turns and the corner.
Baada yake Binui mwana wa Henadadi akajenga sehemu nyingine, kutoka nyumba ya Azaria hadi kona ya ukuta.
25 Palal, son of Uzai, worked opposite where the wall turns and the tower that extends from the upper palace, near the court of the guard. Next were Pedaiah, son of Parosh
Palali, mwana wa Uzai, akajenga juu ya kona ya ukuta na mnara unaoenea juu kutoka nyumba ya juu ya mfalme katika uwanda wa walinzi. Baada yake Pedaya mwana wa Paroshi akajenga.
26 and the Temple servants that lived on the hill of Ophel who made repairs opposite the Water Gate toward the east and the tower that extends.
Sasa watumishi wa hekalu waliokaa Ofeli walijenga mpaka upande wa Hifadhi ya Maji upande wa mashariki wa mnara unaojitokeza.
27 Next were the Tekoites who repaired to another section opposite the great tower that extends to the wall of Ophel.
Baada yake, Watekoi walijenga sehemu nyingine, kuelekea mnara mkubwa ulio nje, mpaka ukuta wa Ofeli.
28 Above the Horse Gate, each of the priests made repairs opposite his own house.
Makuhani wakajenga juu ya lango la farasi, kila mmoja kuelekea nyumba yake.
29 Next was Zadok, son of Immer, who worked opposite his house, and next was Shemaiah, son of Shecaniah, the guard at the East Gate.
Baada yao Sadoki, mwana wa Imeri, alijenga sehemu hiyo kuelekea nyumba yake. Na baada yake Shemaya mwana wa Shekania, mlinzi wa lango la mashariki, akajenga.
30 Next were Hananiah, son of Shelemiah, as well as Hanun, the sixth son of Zalaph, who repaired. Next was Meshullam, son of Berechiah, who made repairs opposite where he lived.
Baada yake Hanania, mwana wa Shelemia, na Hanuni, mwana wa sita wa Salafu, wakajenga sehemu nyingine. Meshulamu mwana wa Berekia akajenga kuelekea kwenye vyumba vyake.
31 Next was Malchijah, one of the goldsmiths, made repairs as far as the house of the Temple servants and the merchants, opposite the Inspection Gate, and as far as the room above the corner.
Baada yake Malkiya, mmoja wa wafua dhahabu, akajenga mpaka nyumba ya watumishi wa hekalu na wafanyabiashara waliokuwa wakielekea lango la gereza na mpaka chumba cha juu cha pembeni.
32 The goldsmiths and merchants made repairs between the room above the corner and the Sheep Gate,
Wafanyabiashara wa dhahabu na wafanyabiashara walijenga kati ya chumba cha juu cha kona na Lango la Kondoo.

< Nehemiah 3 >