< Mark 11 >
1 As they approached Jerusalem, near to Bethphage and Bethany, beside the Mount of Olives, Jesus sent two of his disciples on ahead.
Walipokaribia Yerusalemu, wakafika Bethfage na Bethania katika Mlima wa Mizeituni. Yesu akawatuma wawili wa wanafunzi wake,
2 He told them, “Go into the village ahead of you, and as soon as you enter, you'll find a colt tied up that no one has ever ridden before. Untie it and bring it here.
akawaambia, “Nendeni katika kijiji kilichoko mbele yenu. Na hapo mtakapoingia kijijini, mtamkuta mwana-punda amefungwa hapo, ambaye hajapandwa na mtu bado. Mfungueni, mkamlete hapa.
3 If anyone asks you what you are doing, tell them, ‘The Lord needs it and will send it back soon.’”
Kama mtu yeyote akiwauliza, ‘Mbona mnamfungua?’ Mwambieni, ‘Bwana anamhitaji, na atamrudisha hapa baada ya muda mfupi.’”
4 So they set off, and found a colt tied to a door, out on the street, and they untied it.
Wakaenda, wakamkuta mwana-punda amefungwa kando ya barabara, karibu na mlango wa nyumba.
5 Some of the people standing around asked, “What are you doing, untying that colt”?
Walipokuwa wanamfungua, watu waliokuwa wamesimama karibu wakawauliza, “Mna maana gani mnapomfungua huyo mwana-punda?”
6 The disciples replied just as Jesus told them to, and the people let them go.
Wakawajibu kama vile Yesu alivyokuwa amewaagiza, nao wale watu wakawaruhusu.
7 They brought the colt to Jesus, put their cloaks on it, and Jesus sat on it.
Kisha wakamleta huyo mwana-punda kwa Yesu na kutandika mavazi yao juu yake, naye akampanda.
8 Many people spread their cloaks on the road, while others laid down leafy branches that they'd cut in the fields.
Watu wengi wakatandaza mavazi yao barabarani, na wengine wakatandaza matawi waliyokuwa wamekata mashambani.
9 Those leading in the front and those that were following were all shouting, “Hosanna! Bless the one coming in the name of the Lord.
Kisha wale waliokuwa wametangulia mbele na wale waliokuwa wakifuata nyuma wakapaza sauti, wakisema, “Hosana!” “Amebarikiwa yeye ajaye kwa Jina la Bwana!”
10 Bless the kingdom of our father David that is coming! Hosanna in the highest!”
“Umebarikiwa Ufalme unaokuja wa baba yetu Daudi!” “Hosana kwake yeye aliye juu!”
11 Jesus entered Jerusalem and went in to the Temple. He looked around him, observing everything, and then, since it was getting late, he returned to Bethany with the twelve disciples.
Yesu akaingia Yerusalemu na kwenda Hekaluni. Akaangalia kila kitu kilichokuwamo, lakini kwa kuwa ilishakuwa jioni, akaenda zake Bethania pamoja na wale kumi na wawili.
12 The next day, as they left Bethany, Jesus was hungry.
Kesho yake walipokuwa wakitoka Bethania, Yesu alikuwa na njaa.
13 From some distance away he saw a fig tree with leaves, so he went over to it to see if it had any fruit. But when he got there, he found it had only leaves, because it was not the season for figs.
Akauona mtini kwa mbali, naye akaenda ili aone kama ulikuwa na matunda. Alipoufikia, akakuta una majani tu, kwa kuwa hayakuwa majira ya tini.
14 He said to the tree, “May no one eat fruit from you ever again.” His disciples heard his words. (aiōn )
Akauambia ule mti, “Tangu leo mtu yeyote asile kamwe matunda kutoka kwako.” Wanafunzi wake walimsikia akisema hayo. (aiōn )
15 They arrived back in Jerusalem, and Jesus went into the Temple. He started driving out the people who were buying and selling in the Temple. He overturned the tables of the money-changers and the chairs of the people selling doves.
Walipofika Yerusalemu, Yesu akaingia katika eneo la Hekalu, akaanza kuwafukuza wale waliokuwa wakinunua na kuuza humo ndani. Akazipindua meza za wale waliokuwa wakibadilisha fedha, na pia viti vya wale waliokuwa wakiuza njiwa,
16 He stopped anyone carrying things through the Temple.
wala hakumruhusu mtu yeyote kuchukua bidhaa kupitia ukumbi wa Hekalu.
17 He explained to them, “Doesn't Scripture say, ‘My house will be called a house of prayer for all nations’? But you have turned it into a den of thieves!”
Naye alipokuwa akiwafundisha, akasema, “Je, haikuandikwa kuwa: “‘Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa mataifa yote’? Lakini ninyi mmeifanya kuwa ‘pango la wanyangʼanyi.’”
18 The chief priests and religious teachers heard what had happened, and tried to find a way to kill Jesus. But they were afraid of him, for everyone was so impressed by his teaching.
Viongozi wa makuhani na walimu wa sheria wakapata habari hizi, nao wakaanza kutafuta njia ya kumuua, kwa kuwa walikuwa wakimwogopa, kwa sababu umati wote ulikuwa unashangazwa na mafundisho yake.
19 When evening came Jesus and his disciples left the city.
Ilipofika jioni, Yesu na wanafunzi wake wakatoka nje ya mji.
20 The following morning as they returned, they saw the fig tree, withered from the roots up.
Asubuhi yake walipokuwa wakipita, wakauona ule mtini umenyauka kutoka juu hadi kwenye mizizi yake.
21 Peter remembered what Jesus had done, and said to him, “Rabbi, look, the fig tree that you cursed has withered.”
Petro akakumbuka na kumwambia Yesu, “Rabi, tazama! Ule mtini ulioulaani umenyauka!”
22 “Trust in God,” Jesus replied.
Yesu akawajibu, “Mwaminini Mungu.
23 “Believe me when I say to you that if you told this mountain, ‘Get out of here and be thrown into the sea,’ and you don't doubt in your heart, but are convinced about what you're asking, then it will happen!
Amin, nawaambia, mtu yeyote atakayeuambia mlima huu, ‘Ngʼoka ukatupwe baharini,’ wala asione shaka moyoni mwake, bali aamini kwamba hayo asemayo yametukia, atatimiziwa.
24 I'm telling you that whatever you pray for, whatever you ask, trust that you've received it, and it's yours.
Kwa sababu hiyo nawaambia, yoyote mtakayoyaomba mkisali, aminini ya kwamba mmeyapokea, nayo yatakuwa yenu.
25 But when you're praying, if you have something against someone, forgive them, so that your Father in heaven may also forgive you your sins.”
Nanyi kila msimamapo kusali, sameheni mkiwa na neno na mtu, ili naye Baba yenu aliye mbinguni awasamehe ninyi makosa yenu. [
Lakini kama ninyi msiposamehe, wala Baba yenu aliye mbinguni hatawasamehe ninyi makosa yenu.]”
27 They returned to Jerusalem, and as he was walking in the Temple, the chief priests, religious teachers, and the leaders approached him.
Wakafika tena Yerusalemu, na Yesu alipokuwa akitembea Hekaluni, viongozi wa makuhani, walimu wa sheria pamoja na wazee wa watu wakamjia.
28 “By what authority are you doing all this?” they demanded. “Who gave you the right?”
Wakamuuliza, “Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Na ni nani aliyekupa mamlaka ya kufanya hayo?”
29 “Let me ask you a question,” Jesus told them. “You answer me, and I'll tell you by whose authority I do these things.
Yesu akawajibu, “Nitawauliza swali moja. Nijibuni, nami nitawaambia ni kwa mamlaka gani ninafanya mambo haya.
30 John's baptism—did that come from heaven, or from people?”
Niambieni, je, ubatizo wa Yohana ulitoka mbinguni au kwa wanadamu?”
31 They discussed it among themselves. They said, “If we say it's from heaven, he'll reply, ‘So why didn't you believe him?’
Wakahojiana wao kwa wao, wakisema, “Kama tukisema, ‘Ulitoka mbinguni,’ atatuuliza, ‘Mbona hamkumwamini?’
32 But if we say, it's of human origin, well…” They were afraid of the crowd, because everyone believed that John was a true prophet.
Lakini tukisema, ‘Ulitoka kwa wanadamu,’…” (Waliwaogopa watu, kwa sababu kila mtu aliamini kwamba Yohana alikuwa nabii wa kweli.)
33 So they answered Jesus, “We don't know.” “Then I'm not telling you by whose authority I do these things,” replied Jesus.
Kwa hiyo wakamjibu Yesu, “Hatujui.” Naye Yesu akawaambia, “Wala mimi sitawaambia ni kwa mamlaka gani ninatenda mambo haya.”