< Leviticus 6 >

1 The Lord told Moses,
Bwana alisema na Musa kumwabia,
2 “If you sin against the Lord, breaking your commitment to him, then this is what must happen. You may have lied to your neighbor about something you were looking after for them, about some deposit paid, about something was stolen, or maybe you were trying to cheat them.
“Kama mtu akifanya dhambi na kuvunja amri kinyume na Bwana, kama kujihusisha na uongo dhidi ya jirani yake kuhusu kitu fulani cha kutokuwa mwaminifu, au kama akidanganya au kuiba au amemdhurumu jirani.
3 You may have found property someone lost, and you lied and made false statements about it, or you have sinned in others ways that people do in such situations.
Au akiokota kitu fulani ambacho jirani yake amepoteza na kusema uongo kuhusu hicho, na kuapa kwa uongo au kwa mambo kama haya ambayo watu wanaweza kutenda dhambi.
4 If you have sinned and become guilty you must return what you have stolen or cheated from your victims, the deposit you took, the lost property you found,
Ndipo itakuwa hivi, kama ametenda dhambi na hatia, kwamba lazima akirudishe kwa vyovyote alichoiba au kudanganya au amedhurumu au kitu kilichopotea naye kukiokota.
5 or anything else that must be given back that you lied about. You must pay full compensation plus a fifth of the value, and give it to the owner as soon as you accept that you are guilty of sin.
Au kama amedanganya kwa jambo lolote, lazima atakirudisha kamilina kuongezea sehemu ya tano kwa kumlipa anayedai, kwa siku ile anayopatikana na hatia.
6 Then you must take to the priest your guilt offering for the Lord: a ram without defects of the appropriate value from the flock.
Ataleta sadka ya hatia kwa Bwana: kondoo dume asiye na kasoro kutoka katika kundi lake kulingana na thamani yake, kama sadaka ya hatia kwa kuhani.
7 This is how the priest will make you right before the Lord, and you will be forgiven whatever sins you may have done that you are guilty of.”
Kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake mbele ya Bwana, atakuwa amesamehewa kulingana na chochote kilicho mfanya kuwa na hatia.”
8 The Lord told Moses,
Ndipo Bwana alisema na Musa kumwambia,
9 “Give Aaron and his sons these instructions regarding the burnt offering: The burnt offering is to be left on the fireplace of the altar throughout night until morning, and the fire must be kept burning on the altar.
“Mwagize Haruni na wanawe, kusema, 'hii ni sheria ya sadaka ya kuteketezwa: Sadaka ya kuteketezwa lazima iwe juu ya makaa ya madhabahu usiku wote hata asubuhi, na moto wa madhabahu utaendelea kuwaka.
10 The priest shall put on his linen clothes and underwear, and he shall take from the altar the greasy ashes of the burnt offering that the fire has burned up and set them down beside the altar.
Kuhani atavaa nguo zake za kitani na atavaa nguo za kitani ndani yake. Atatoa majivu yaliyobaki baada ya moto kutekeza sadaka ya kuteketezwa juu ya madhabahu, na ataweka majivu pembeni mwa madhabahu.
11 Then he has to change his clothes, and take the ashes outside the camp to a place that's ceremonially clean.
Atavua mavazi haya na kuvaa mavazi mengine ili kuchukua majivu nje ya kambi na kupeleka mahali palipo safi.
12 The fire on the altar must be kept burning—don't let it go out. Each morning the priest is to add wood to the fire, carefully place the burnt offering on it, and burn the fat parts of the peace offerings on it.
Moto katika madhabahu utaendelea kuwaka. Usizimike, na kuhani ataongeza kuni kila asubuhi. Atapanga juu yake sadaka ya kuteketezwa kama inavyotakiwa, na atateketeza juu yake mafuta ya sadaka ya amani.
13 The fire must always be kept burning on the altar continually—don't let it go out.
Moto lazima utaendelea kuwaka katika madhabahu, kamwe usizimike.
14 These are the regulations for the grain offering: Aaron's sons are to present it before the Lord, in front of the altar.
Hii ni sheria ya sadaka ya nafaka. Wana wa Haruni watatoa mbele ya Bwana katika madhabahu.
15 The priest shall remove a handful of the best flour mixed with olive oil, as well as all the frankincense from the grain offering, and burn the ‘reminder part’ on the altar to be to be accepted by the Lord.
Kuhani atachukua konzi ya unga laini wa sadaka ya nafaka na mafuta na ubani ambao uko juu ya sadaka ya nafaka, atateketeza juu ya madhabahu kuleta harufu nzuri ya shukrani ya kumpendeza Bwana.
16 The rest is for Aaron and his sons to eat. It must be eaten without yeast in a holy place—the courtyard of the Tent of Meeting.
Haruni na wanae watakula sadaka inayobaki, italiwa bila kutiwa chachu mahali patakatifu. Watakula katika ua ya hema ya kukutania.
17 It must not be baked with yeast. I have provided it as their share of my food offerings. It is most holy, just like the sin offering and the guilt offering.
Haitaokwa pamoja na chachu. Nimewapa kama sehemu ya sadaka yangu itolewayo kwa moto, ni takatifu sana, kama sadaka ya dhambi na sadaka ya hatia.
18 Any of Aaron's male descendants may eat it. This is a permanent allowance from the food offerings to the Lord for future generations. Whatever touches them shall become holy.”
Kwa nyakati zote zijazo kupitia watu wa kizazi chako, mwanaume yeyote mzaliwa kutoka kwa Haruni aweza kula ni sehemu yake, ichukuliwayo katika sadaka ya Bwana kwa moto. Yeyote anayeigusa atakuwa mtakatifu.”
19 The Lord told Moses,
Bwana aliongea tena na Musa kumwambia,
20 “This is the offering that Aaron and his sons are to present to the Lord when they're anointed: a tenth of an ephah of best flour as a usual grain offering, half in the morning and half in the evening.
“Hii ni sadaka ya Haruni na wanawe ambayo watatoa kwa Bwana katika siku ambayo kila mwana atawekwa wakfu: sehemu ya kumi ya efa ya unga laini kama kawaida sadaka ya nafaka nusu yake asubuhi na nusu yake jioni.
21 Cook it with olive oil on a griddle. Bring it well-kneaded and present it as a grain offering broken into pieces, to be accepted by the Lord.
Itatengenezwa na mafuta katika kikaango, utaileta ikiwa imeandaliwa imeokwa katika vipande utatoa sadaka ya nafaka ili kuleta harufu nzuri kwa Bwana.
22 It is to be cooked by the priest who is one of Aaron's descendants and who is to be anointed to take his place. In this case since it is permanently allocated to the Lord, it must be burned completely.
Mwana wa Kuhani Mkuu atakayekuwa Kuhani Mkuu mpya kutoka miongoni mwa wanawe ataitoa. Kama amri ya milele, yote itateketezwa kwa Bwana.
23 Every grain offering for a priest is to be burned completely. It must not be eaten.”
Kila sadaka ya nafaka ya kuhani itatekezwa yote. Haitaliwa kamwe.”
24 The Lord told Moses,
Bwana alisema tena Musa, kumwambia,
25 “Tell Aaron and his sons that these are the regulations for the sin offering. The sin offering is to be killed where the burnt offering is killed before the Lord, and it is most holy.
“Sema na Haruni na watoto wake kwamba, 'Hii ni sheria ya sadaka ya dhambi: Sadaka ya dhambi lazima kuchinjwa mahali pa sadaka ya kuteketezwa itachinjwa mbeleya Bwana. Ni takatifu sana.
26 The priest who offers the sin offering is to eat it. It must be eaten without yeast in a holy place—the courtyard of the Tent of Meeting.
Kuhani atakayeitoa kwa ajili ya dhambi ndiye atakayeila. Italiwa mahali patakatifu katika ua wa hema ya kukutania.
27 Whatever touches it shall become holy and if any of the blood is splashed on clothing, you must wash it in a holy place.
Yeyote atakayeigusa nyama yake atakuwa ni mtakatifu na kama damu itadondokea mavazi yatafuliwa mahali palipodondokewa, mahali patakatifu.
28 The clay pot used to boil the sin offering must be broken. If it's boiled in a bronze pot, the pot must be thoroughly cleaned and washed out with water.
Lakini chungu kikipikiwa kitavunjwa, kama imepikiwa katika chombo cha shaba, lazima kitasuguliwa na kusafishwa kwa maji.
29 Any male among the priests may eat it, it is most holy.
Mwanaume yeyote miongoni mwa makuhani anaweza kula nyama hiyo kwa sababu ni takatifu sana.
30 But no sin offering may be eaten if its blood has been taken into the Tent of Meeting to as a means to make things right in the Holy Place. In that case it must be burned.”
Na hakuna sadaka ya dhambi italiwa ambayo damu yake imeletwa katika hema ya kukutania kufanya upatanisho katika mahali patakatifu. Ni lazima iteketezwe.

< Leviticus 6 >