< Leviticus 25 >

1 The Lord told Moses on Mount Sinai,
Bwana akamwambia Mose katika Mlima Sinai,
2 “Tell the Israelites: When you enter the land that I'm giving you, the land itself must also observe a Sabbath rest in honor of the Lord.
“Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mtakapoingia katika nchi ninayowapa ninyi, nchi yenyewe ni lazima ishike Sabato kwa ajili ya Bwana.
3 Six years you can cultivate your fields, take care of your vineyards, and harvest your crops.
Kwa miaka sita mtapanda mazao katika mashamba yenu, nanyi kwa miaka sita mtaikata mizabibu yenu matawi na kuvuna mazao yake.
4 But the seventh year is to be a Sabbath of complete rest for the land, a Sabbath in honor of the Lord. Don't plant your fields or care for your vineyards.
Lakini mwaka wa saba nchi lazima iwe na Sabato ya mapumziko, Sabato kwa Bwana. Msipande mbegu katika mashamba yenu, wala msikate mizabibu yenu matawi.
5 Don't harvest what may have grown up in your fields, or collect the grapes from your vineyards that you haven't cared for. The land is to have a year of complete rest.
Msivune na kuweka akiba kinachoota chenyewe, wala kuvuna na kusindika zabibu ambayo hamkuhudumia mashamba yake. Nchi lazima iwe na mwaka wa mapumziko.
6 You can eat whatever the land produces during the Sabbath year. This applies to yourself, your male and female slaves, paid workers and foreigners who live with you,
Chochote nchi itoacho katika mwaka wa Sabato kitakuwa chakula chenu wenyewe, watumishi wenu wa kiume na wa kike, mfanyakazi aliyeajiriwa, na mkazi wa muda anayeishi miongoni mwenu,
7 and to your livestock and the wild animals living in your land. Whatever grows can be used for food.
vilevile malisho ya mifugo yenu na wanyama pori katika nchi yenu. Chochote nchi itakachozalisha kinaweza kuliwa.
8 Count seven ‘sabbaths’ of years, in other words, seven times seven years, so that the seven sabbaths of years come to forty-nine years.
“‘Hesabu Sabato saba za miaka, yaani miaka saba mara saba, ili Sabato saba za miaka utakuwa muda wa miaka arobaini na tisa.
9 Then blow the trumpet all through the country on the tenth day of the seventh month, which is the Day of Atonement. Make sure this signal is heard throughout your whole country.
Ndipo tarumbeta itapigwa kila mahali katika siku ya kumi ya mwezi wa saba. Katika Siku ya Upatanisho, piga tarumbeta katika nchi yako yote.
10 You are to dedicate the fiftieth year and announce freedom everywhere in the country for all who live there. This is to be your Jubilee, when each of you is to return to reclaim your property and to be part of your family once more.
Mwaka wa hamsini mtauweka wakfu na kutangaza uhuru katika nchi kwa wakazi wake wote. Itakuwa ni yubile kwenu; kila mmoja wenu atairudia mali ya jamaa yake, na kila mmoja kurudi kwenye ukoo wake.
11 The fiftieth year will be a Jubilee for you. Don't sow the land; don't harvest what may have grown up in your fields, or collect the grapes from your vineyards that you haven't cared for.
Mwaka wa hamsini utakuwa yubile kwenu, msipande wala msivune kile kiotacho chenyewe, au kuvuna zabibu zisizohudumiwa.
12 It is a Jubilee and it is to be holy to you. You can eat whatever the land produces.
Kwa kuwa ni yubile, nayo itakuwa takatifu kwenu; mtakula tu kile kilichotoka moja kwa moja mashambani.
13 In this Jubilee Year, every one of you shall return to your own property.
“‘Katika huu Mwaka wa Yubile, kila mmoja atarudi kwenye mali yake mwenyewe.
14 If you sell land to your neighbor, or buy land from him, don't exploit one another.
“‘Ikiwa utauza ardhi kwa mmoja wa wazawa wa nchi yako, au ukinunua ardhi kutoka kwake, mmoja asimpunje mwingine.
15 When you buy from your neighbor work out how many years have passed since the last Jubilee, for he is to sell to you depending on how many years of harvest remain.
Utanunua ardhi kwa mzawa wa nchi yako kwa misingi ya hesabu ya miaka baada ya Yubile. Naye ataiuza kwako kwa misingi ya hesabu ya miaka iliyobaki kwa kuvuna mavuno.
16 The more years that are left, the more you shall pay; the fewer years that are left, the less you shall pay, because he is actually selling you a specific number of harvests.
Miaka inapokuwa mingi, utaongeza bei, nayo miaka ikiwa michache, utapunguza bei, kwa sababu kile anachokuuzia kwa hakika ni hesabu ya mazao.
17 Don't exploit one another, but have respect for your God, because I am the Lord your God.
Mmoja asimpunje mwingine, bali utamcha Mungu wako. Mimi ndimi Bwana Mungu wako.
18 Keep my rules and observe my regulations, so you can live in safety in the land.
“‘Fuateni amri zangu, mwe waangalifu kutii amri zangu, nanyi mtaishi salama katika nchi.
19 Then the land will produce good harvest, so you will have plenty to eat and live in safety there.
Kisha nchi itazaa matunda yake, nanyi mtakula na kushiba na kuishi humo kwa salama.
20 But if you ask, ‘What are we going to in the seventh year if we do not sow or harvest our crops?’
Mwaweza kuuliza, “Tutakula nini katika mwaka wa saba ikiwa hatutapanda wala kuvuna mazao yetu?”
21 I will bless you in the sixth year, so that the land will produce a crop that will be enough for three years.
Nitawapelekeeni baraka ya pekee katika mwaka wa sita, kwamba nchi itazalisha mazao ya kutosha kwa miaka mitatu.
22 As you sow in the eighth year, you will still be eating from that harvest, which will last until your harvest in the ninth year.
Mnapopanda mwaka wa nane, mtakula mavuno ya miaka iliyopita. Pia mtaendelea kuyala mazao hayo hadi mvune mavuno ya mwaka wa tisa.
23 Land must not be permanently sold, because it really belongs to me. To me you are only foreigners and travelers passing through.
“‘Kamwe ardhi isiuzwe kwa mkataba wa kudumu, kwa sababu nchi ni mali yangu, nanyi ni wageni na wapangaji wangu.
24 So whatever land you buy to own, you must make arrangements so it can be returned to its original owner.
Katika nchi yote mtakayoshika kuwa milki yenu, ni lazima mtoe ukombozi wa ardhi.
25 If one of your people becomes poor and sells you some of their land, their close family can come and buy back what they have sold.
“‘Ikiwa mmoja wa wazawa wa nchi yako amekuwa maskini na akauza baadhi ya mali yake, ndugu yake wa karibu atakuja na kukomboa kile ndugu yako alichokiuza.
26 However, if they don't have anyone who can buy it back, but in the meantime their financial situation improves and they have enough to buy back the land,
Iwapo mtu huyo hana jamaa wa karibu wa kukomboa mali hiyo kwa ajili yake, lakini yeye mwenyewe akafanikiwa na kupata mali itoshayo kuikomboa,
27 they will work how many years it has been since the sale, and pay back the balance to the person who bought it, and go back to their property
ataamua tena thamani yake kwa miaka tangu alipoiuza, na kurudisha kiasi kilichobaki cha thamani kwa mtu ambaye alikuwa amemuuzia mali hiyo, naye ataweza kuirudia mali yake.
28 If they can't raise enough to pay the person back for the land, the buyer will remain its owner until the Jubilee Year. But in the Jubilee the land will be returned so that the original owner can so that they can go back to their property.
Lakini kama hatapata njia ya kumlipa mnunuzi, ile mali aliyouza itabaki kumilikiwa na mnunuzi mpaka Mwaka wa Yubile. Mali hiyo itarudishwa mwaka wa Yubile, naye ataweza kuirudia mali yake.
29 If someone sells a house located in a walled town, they have the right to buy it back for a full year after selling it. It can be bought back any time during that year.
“‘Ikiwa mtu atauza nyumba iliyo ndani ya mji uliozungukwa kwa ukuta, yeye anayo haki ya kuikomboa mwaka mzima baada ya mauzo ya hiyo nyumba. Wakati huo anaweza kuikomboa.
30 If it isn't bought back be the end of a full year, then ownership of the house in the walled town is permanently transferred to the one who bought it and their descendants. It won't be returned in the Jubilee.
Ikiwa haikukombolewa kabla ya mwaka mmoja kamili kupita, nyumba iliyo ndani ya mji uliozungukwa kwa ukuta itakuwa mali ya kudumu ya mnunuzi na wazao wake. Haitarudishwa mwaka wa Yubile.
31 But houses in villages that don't have walls around them are to be treated as located in the fields. They can be bought back, and will be returned in the Jubilee.
Lakini nyumba zilizo vijijini bila ya kuwa na kuta zilizozizunguka zitahesabiwa kama mashamba. Zinaweza kukombolewa, nazo zirudishwe katika mwaka wa Yubile.
32 However, the Levites always have the right to buy back their houses in the towns that belong to them.
“‘Walawi siku zote wana haki ya kukomboa nyumba zao katika miji ya Walawi wanayoimiliki.
33 Whatever the Levites own can be bought back, even houses sold in their towns, and must be returned in the Jubilee. That's because the houses in the towns of the Levites are what they were given to own as their share among the Israelites.
Kwa hiyo mali ya Mlawi inaweza kukombolewa, yaani nyumba iliyouzwa katika mji wowote wanaoushikilia itarudishwa mwaka wa Yubile, kwa sababu nyumba zilizo katika miji ya Walawi ni mali yao miongoni mwa Waisraeli.
34 However, the fields surrounding their towns must not be sold because they belong to the Levites permanently.
Lakini nchi ya malisho iliyo mali ya miji yao kamwe isiuzwe, ni milki yao ya kudumu.
35 If any of your people become poor and can't survive, you must help them in the same way you would help a foreigner or a stranger, so that they can go on living in your neighborhood.
“‘Ikiwa mmoja wa wazawa wa nchi yako amekuwa maskini, naye akashindwa kujitegemeza mwenyewe katikati yako, msaidie kama vile ambavyo ungelimsaidia mgeni au kama mkazi wa muda, ili aweze kuendelea kuishi katikati yako.
36 Don't make them pay you any interest or demand more than they borrowed, but respect your God so that they can remain living in your area.
Usichukue riba wala faida yoyote kutoka kwake, bali utamwogopa Mungu wako, ili mzawa wa nchi yako aweze kuendelea kuishi katikati yako.
37 Don't lend them silver with interest or sell them food at an inflated price.
Usimkopeshe fedha ili alipe na riba, wala usimuuzie chakula kwa faida.
38 Remember, I am the Lord your God who led you out of Egypt to give you the land of Canaan and to be your God.
Mimi ndimi Bwana Mungu wako, niliyekuleta kutoka nchi ya Misri nikupe nchi ya Kanaani, nami niwe Mungu wako.
39 If any of your people become poor and have to sell themselves to work for you, don't force them to work as a slave.
“‘Ikiwa mmoja wa wazawa wa nchi yako amekuwa maskini katikati yako, naye akajiuza kwako, usimfanye atumike kama mtumwa.
40 Have them live with you like a paid worker who is staying with you for a while. They are to work for you until the Jubilee Year.
Atatendewa kama mfanyakazi aliyeajiriwa, au kama mkazi wa muda katikati yako, naye atatumika mpaka Mwaka wa Yubile.
41 Then they and their children must be freed, and they can go back to their family and to their family's property.
Ndipo yeye na watoto wake wataachiwa, naye atarudi kwa watu wa ukoo wake, na kwenye mali ya baba zake.
42 Israelites are not to be sold as slaves because they belong to me as my slaves—I led them out of Egypt.
Kwa sababu Waisraeli ni watumishi wangu niliowaleta kutoka nchi ya Misri, kamwe wasiuzwe kama watumwa.
43 Don't treat them with brutality. Have respect for your God.
Usiwatawale kwa ukatili, lakini utamcha Mungu wako.
44 Buy your male and female slaves from the surrounding nations.
“‘Watumwa wako wa kiume na wa kike watatoka katika mataifa yanayokuzunguka; kutoka kwao waweza kununua watumwa.
45 You can also buy them from foreigners who have come to live among you, or from their descendants born in your land. You can treat them as your property.
Pia waweza kununua baadhi ya wakazi wa muda wanaoishi katikati yako, na jamaa ya koo zao waliozaliwa katika nchi yako, nao watakuwa mali yako.
46 You can pass them on to your children to inherit as property after you die. You can make them slaves for life, but you must not brutally treat any of your own people, the Israelites, as a slave.
Hao waweza kuwarithisha watoto wako kuwa urithi wao, na wanaweza kuwafanya watumwa maisha yao yote, lakini usiwatawale ndugu zako Waisraeli kwa ukatili.
47 If a foreigner among you becomes successful, and one of your people living nearby becomes poor and sells themselves to the foreigner or to a member of the foreigner's family,
“‘Ikiwa mgeni au mkazi wa muda katikati yako atakuwa tajiri, na mmoja wa wazawa wa nchi yako akawa maskini, naye akajiuza kwa yule mgeni anayeishi katikati yako, au kwa mmoja wa jamaa wa koo za wageni,
48 they still have the right of being bought back after the sale. A member of their family can buy them back—
anayo haki ya kukombolewa baada ya kujiuza. Mmoja wa jamaa zake aweza kumkomboa:
49 an uncle or cousin or any close relative from their family can buy them back. If they become successful, they can buy themselves back.
Mjomba wake, au binamu yake, au yeyote aliye ndugu wa damu katika ukoo wake aweza kumkomboa. Au ikiwa atafanikiwa, anaweza kujikomboa mwenyewe.
50 The person concerned and their buyer will work out the time from the year of the sale up to the Jubilee Year. The price will depend on the number of years, calculated using the daily rate for a paid worker.
Yeye na huyo aliyemnunua watahesabu muda kuanzia mwaka aliojiuza hadi Mwaka wa Yubile. Mahali pa kuanzia bei ya kuachiwa kwake itakadiriwa kwa ujira unaolipwa mfanyakazi aliyeajiriwa kwa idadi ya hiyo miaka.
51 If there are many years left, they must pay a larger percentage of the purchase price.
Ikiwa imebaki miaka mingi, ni lazima atalipia ukombozi wake fungu kubwa la bei iliyolipwa kumnunua yeye.
52 If there are only a few years remaining before the Jubilee Year, then they only have to pay a percentage depending on the number of years still left.
Ikiwa miaka iliyobaki ni michache kufikia Mwaka wa Yubile, atafanya hesabu yake, naye atalipa malipo yanayostahili kwa ajili ya ukombozi wake.
53 They are to live with their foreign owner just like a paid worker, hired from year to year, but see to it that the owner doesn't treat him brutally.
Atatendewa kama mtu wa kuajiriwa mwaka hadi mwaka; lazima uone kwamba yule aliyemnunua hamtawali kwa ukatili.
54 If they are not bought back in any of the ways described, they and their children shall be freed in the Jubilee Year.
“‘Hata ikiwa hakukombolewa kwa njia mojawapo ya hizi, yeye na watoto wake wataachiwa katika Mwaka wa Yubile,
55 For the Israelites belong to me as my slaves. They are my slaves—I led them out of Egypt. I am the Lord your God.”
kwa maana Waisraeli ni mali yangu kama watumishi. Wao ni watumishi wangu, niliowatoa kutoka nchi ya Misri. Mimi ndimi Bwana Mungu wako.

< Leviticus 25 >