< Leviticus 21 >

1 The Lord told Moses, “Tell Aaron's sons, the priests: A priest is not to make himself unclean by touching the dead body of any of his relatives.
Bwana akamwambia Mose, “Sema na makuhani, wana wa Aroni, uwaambie: ‘Kamwe kuhani asijitie unajisi kwa utaratibu wa kiibada kwa ajili ya mtu wake yeyote anayekufa,
2 The only exceptions are for his immediate family. This includes his mother, father, son, daughter, or brother,
isipokuwa jamaa wake wa karibu, kama vile mama yake au baba yake, mwanawe au binti yake, ndugu yake,
3 or his unmarried sister since she is a close relative because she doesn't have a husband.
au dada yake asiyeolewa ambaye anamtegemea kwa kuwa hana mume, kwa ajili ya hao aweza kujitia unajisi.
4 He must not make himself unclean for those only related to him by marriage—he is not to make himself ceremonially impure.
Kamwe asijitie unajisi mwenyewe kutokana na wale watu ambao anahusiana nao kwa kuoana, na hivyo kujitia unajisi.
5 Priests are not to shave bald spots on their heads, trim the sides of their beards, or cut their bodies.
“‘Kamwe makuhani wasinyoe nywele za vichwa vyao wala wasinyoe pembeni mwa ndevu zao, au kuweka chale kwenye miili yao.
6 They must be holy to their God and not disgrace their God's reputation. They are the one who present the food offerings to the Lord, the food of their God. Consequently they must be holy.
Lazima wawe watakatifu kwa Mungu wao, na kamwe wasilinajisi jina la Mungu wao. Kwa sababu ndio wanaotoa sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa Bwana, chakula cha Mungu wao, hivyo lazima wawe watakatifu.
7 A priest is not to marry a woman made unclean through prostitution or who is divorced by her husband, for the priest must be holy to his God.
“‘Kamwe wasioe wanawake waliojinajisi kwa ukahaba, au waliopewa talaka na waume wao, kwa sababu makuhani ni watakatifu kwa Mungu wao.
8 You shall consider him holy because he presents the food offerings to your God. He shall be holy to you, because I am holy. I am the Lord, and I chose you as my special people.
Waoneni kuwa watakatifu, kwa sababu ndio wanaotoa chakula cha Mungu wenu. Kumbukeni kuwa ni watakatifu, kwa sababu Mimi Bwana ni mtakatifu, Mimi niwafanyaye ninyi kuwa watakatifu.
9 A priest's daughter who makes herself unclean through prostitution makes her father unclean. She must be executed by burning.
“‘Ikiwa binti wa kuhani anajitia unajisi kwa kufanya ukahaba, anamwaibisha baba yake; lazima achomwe kwa moto.
10 The high priest has the highest place among the other priests. He has been anointed with olive oil poured on his head and has been ordained to wear the priestly clothing. He must not leave his hair uncombed or tear his clothes.
“‘Kuhani mkuu, yule miongoni mwa ndugu zake ambaye amekwisha kutiwa mafuta kwa kumiminiwa juu ya kichwa chake, na ambaye amewekwa wakfu kuvaa mavazi ya ukuhani, kamwe asiache nywele zake bila kufunikwa, wala asirarue nguo zake.
11 He is not to go near any dead body. He must not make himself unclean, even it is for his own father or mother.
Kamwe asiingie mahali palipo maiti ndani. Kamwe asijitie unajisi, hata kwa ajili ya baba yake au mama yake,
12 He must not leave to deal with someone who has died or make the sanctuary of his God unclean because he has been dedicated by the anointing oil of his God. I am the Lord.
wala asiondoke mahali patakatifu pa Mungu wake au kupanajisi, kwa sababu amewekwa wakfu kwa mafuta ya Mungu wake. Mimi ndimi Bwana.
13 He can only marry a virgin.
“‘Mwanamke kuhani atakayemwoa lazima awe bikira.
14 He must not marry a widow, a divorced woman, or one made unclean through prostitution. He has to marry a virgin from his own people,
Kamwe asimwoe mjane, au mwanamke aliyepewa talaka, wala mwanamke aliyejinajisi kwa ukahaba, bali atamwoa tu bikira kutoka miongoni mwa watu wake,
15 so that he doesn't make his children unclean among his people, for I am the Lord who makes him holy.”
na hivyo hatawatia unajisi watoto wake miongoni mwa watu wake. Mimi ndimi Bwana, nimfanyaye mtakatifu.’”
16 The Lord told Moses,
Bwana akamwambia Mose,
17 “Tell Aaron: These rules apply for all future generations. If any of your descendants has a physical defect, he is not allowed to come and present the food offerings of his God.
“Mwambie Aroni: ‘Kwa vizazi vijavyo, hakuna mzao wako mwenye dosari atakayekaribia kutoa chakula cha Mungu wake.
18 No man is allowed to do this if he has any defects, including anyone who is blind, crippled, facially disfigured, or has deformities,
Hakuna mtu mwenye dosari yoyote awezaye kukaribia: hakuna mtu aliye kipofu au kiwete, au aliyeharibika uso au asiye na viungo kamili,
19 anyone who has a broken foot or arm,
hakuna mtu mwenye mguu au mkono uliolemaa,
20 anyone who is a hunchback or dwarf, or who has cataracts, skin sores or scabs, or a damaged testicle.
au mwenye kibiongo au aliyedumaa, au aliye na tatizo la macho, au aliye na uvimbe wenye usaha au majipu, au aliyehasiwa.
21 No descendant of Aaron the priest who has a defect is allowed to come and present the food offerings to the Lord. Because he has a defect, he must not come and offer the food of his God.
Hakuna mzao wa kuhani Aroni mwenye kilema chochote atakayekaribia kutoa sadaka kwa Bwana ya kuteketezwa kwa moto. Kama ana kilema, kamwe asikaribie kutoa chakula cha Mungu wake.
22 He is still allowed to eat the food from the Most Holy Place of his God and also from the sanctuary,
Anaweza kula chakula kitakatifu sana cha Mungu wake, pia hata chakula kitakatifu.
23 but because he has a defect, he is not allowed to go near the curtain or the altar, so that my sanctuary and everything in it are not made unclean, because I am the Lord who makes them holy.”
Lakini kwa sababu ya kilema chake, kamwe asikaribie karibu na pazia wala kukaribia madhabahu, asije akanajisi mahali patakatifu pangu. Mimi ndimi Bwana, niwafanyaye watakatifu.’”
24 Moses repeated this to Aaron and his sons, and to all the Israelites.
Basi Mose akamwambia Aroni jambo hili na wanawe, pamoja na Waisraeli wote.

< Leviticus 21 >