< Leviticus 16 >
1 The Lord spoke to Moses after the death of two of Aaron's sons when they went into the Lord's presence.
Yahwe alizungumza na Musa - hii ni baada vifo vya wana wawili wa Haruni, walipomkaribia Yahwe na ndipo wakafa.
2 The Lord told Moses: “Warn your brother Aaron not to come into the Most Holy Place whenever he wants, otherwise he'll die. For that's where I appear in the cloud above the atonement cover of the Ark, behind the veil.
Yahwe alimwambia Musa, “Ongea na Haruni kaka yako na umwambie hapana kuja tu wakati wowote katika patakatifu pa patakatifu ndani ya pazia, mbele ya kifuniko cha upatanisho kilicho juu ya sanduku. Akifanya hivyo, anakufa, kwasababu naonekana katika wingu juu ya kifuniko cha upatanisho.
3 These are the instructions as to how Aaron is to enter the sanctuary. He is to come with a young bull for a sin offering and a ram for a burnt offering.
Hivi ndivyo jinsi Haruni lazima aje katika patakatifu pa patakatifu. Yeye lazima aingie pamoja na ndama kama sadaka ya dhambi, na kondoo dume kama sadaka ya dhambi.
4 He is to be wearing the holy linen tunic, with linen underwear. He has to tie a linen sash around him and put on the linen turban. These are holy clothes. He must wash himself with water before he puts them on.
Ni lazima avae kanzu ya kitatani, na lazima avae ndani yake nguo ya kitani, na lazima avae mshipi wa kitani na kilemba cha kitani. Haya ni mavazi matakatifu. Lazima aoge mwili wake katika maji na avae mavazi haya.
5 From the people of Israel he is to bring two male goats for a sin offering, and a ram for a burnt offering.
Lazima achukue kwenye umati wa watu wa Israeli mbuzi wawili waume kama sadaka ya dhambi na kondoo dume moja ikiwa ni sadaka ya kuteketezwa.
6 Aaron will present the bull as his own sin offering to make himself and his household right.
Ndipo Haruni lazima alete ng'ombe kama sadaka ya dhambi, ambayo itakuwa kwaajili yake mwenyewe, kufanya upatanisho kwaajili yake mwenyewe na familia yake.
7 Then he will bring the two goats and present them before the Lord at the entrance to the Tent of Meeting.
Ndipo lazima achukue mbuzi wawili na kuwaweka mbele ya Yahwe katika mlango wa kuingilia kwenye hema ya mkutano.
8 Aaron will casts lots to choose between the goats, one for the Lord and the other for the scapegoat.
Ndipo Haruni lazima apige kura kwaajili ya mbuzi hao wawili, kura moja kwaajili ya Yahwe, na kura nyingine kwaajili ya msingiziwa.
9 He will present the goat that was chosen by lot for the Lord and sacrifice it as a sin offering.
Ndipo Haruni lazima awasilishe mbuzi ambaye kura imeangukia kwa Yahwe, na kumtoa mbuzi huyo kama sadaka ya dhambi.
10 The goat chosen by lot as the scapegoat is to be presented alive before the Lord to make things right by sending it away into the wilderness as the scapegoat.
Lakini mbuzi ambaye kura ya usingiziwa imemwangukia lazima aletwe kwa Yahwe akiwa hai, kufanya upatanisho kwa kumwachia aende porini kama, mbuzimsingiziwa.
11 Aaron is to present the bull for his sin offering to make things right for himself and his household by killing the bull as his own sin offering.
Pia Haruni lazima alete ng'ombe kwaajili ya sadaka ya dhambi, ambayo itakuwa kwaajili yake mwenyewe, lazima afanye upatanisho kwaajili yake mwenyewe na familia yake, hivyo lazima yeye amuue huyo ng'ombe kama sadaka ya dhambi kwaajili yake mwenyewe.
12 Then he will fill up a incense burner with burning coals from the altar that is before the Lord, and with his hands full of finely-ground sweet-smelling incense, take them behind the veil.
Haruni lazima achukue chetezo iliyojaa mkaa wa moto kutoka kwenye madhabahu mbele ya Yahwe, na mikono imejaa ubani mzuri, na kuleta vitu hivi ndani ya pazia.
13 In the presence of the Lord he will put the incense on the burning coals, and the smoke from the incense will cover the atonement cover above the Testimony, so that he will not die.
Hapo lazima aweke ubani juu ya moto mbele za Yahwe ili kwamba wingu kutoka kwenye ubani liweze kufunika kifuniko cha agano la imani ya upatanisho. Yeye afanye hivyo ili kwamba asife.
14 He will take some of the bull's blood and with his finger sprinkle it on the east side of the atonement cover. He shall also sprinkle some of it with his finger seven times in front of the atonement cover.
Ndipo lazima achukue kiasi cha damu ya ng'ombe na kuinyunyiza kwa kidole chake mbele ya kifuniko cha upatanisho. Lazima anyunyize kiasi cha damu kwa kidole chake mara saba mbele ya kifuniko cha upatanisho.
15 Then Aaron will slaughter the goat for the sin offering for the people and bring its blood behind the veil, and with its blood he must do as he did with the bull's blood: He is to sprinkle it against the mercy seat and in front of it.
Ndipo lazima aue mbuzi kwaajili ya sadaka ya dhambi ambayo ni kwaajili ya watu na kuileta damu yake ndani kwenye pazi. Hapo lazima aifanyie damu kama alivyofanya kwenye damu ya fahali: lazima ainyunyize juu ya kifuniko cha upatanisho na mbele ya kifunuko cha upatanisho.
16 This is how he will set right the Most Holy Place and purify it from the uncleanness of the Israelites, their acts of rebellion, and all their sins. He will do the same for the Tent of Meeting which is in the middle of their camp, surrounded by their unclean lives.
Yeye lazima afanye upatanisho kwaajili ya mahali patakatifu kwa sababu ya matendo ya unajisi ya watu wa Israeli, na kwa sababu ya uasi na dhambi zao zote. Yeye pia lazima afanye haya kwaajili ya hema ya mkutano, ambapo Yahwe anaishi kati yao, katika uwepo wa matendo yao ya unajisi.
17 No one can be in the Tent of Meeting from the time Aaron enters to purify the Most Holy Place until he leaves, after he has made things right for himself, his household, and all the Israelites.
Hakuna mtu anayetakiwa kuwepo katika hema ya mkutano wakati Haruni anaingia kufanya upatanisho katika mahali patakatifu pa patakatifu, na mpaka atoke nje na amemaliza kufanya upatanisho kwaajili yake mwenyewe na kwaajili ya familia yake, na kwaajili umati wa Israeli.
18 Then he shall go to the altar that is before the Lord and purify it. He is to take some of the blood from the bull and the goat and put it on all the horns of the altar.
Yeye lazima aende nje kwenye madhabahu hapo mbele za Yahwe na kufanya upatanisho kwaajili ya hiyo, na lazima achukue kiasi cha damu ya mbuzi na kuiweka juu ya pembe za madhabahu yote kuzunguka.
19 He is to sprinkle some of the blood on it with his finger seven times to dedicate it and purify it from the uncleanness of the Israelites.
Anatakiwa anyunyize kiasi cha damu juu yake kwa kidole chake mara saba kuitakasa na kuitenga maalumu kwa Yahwe, mbali kutoka matendo ya unajisi wa watu wa Israeli.
20 Once Aaron has finished purifying the Most Holy Place, the Tent of Meeting, and the altar, he is to present the live goat.
Atakapo maliza kupatanisha kwaajili ya mahali patakatifu sana, hema la mkutano, na madhabahu, lazima amlete mbuzi aliyehai.
21 Then he will put both hands on the head of the live goat and confess over it all the wrongs of the Israelites, all their acts of rebellion, and all their sins. He is to put them on the goat's head and send it away into the desert, taken there by a man chosen to do it.
Haruni lazima aweke mikono yake yote juu ya kichwa cha mbuzi huyu aliyehai na akiri juu yake maovu yote ya watu wa Israeli, uasi wao wote, dhambi zao zote. Ndipo lazima aweke dhambi hizo juu ya kichwa cha mbuzi na amwachie katika uangalizi wa mtu aliyetari kumwongoza mbuzi huyo porini.
22 The goat will take upon itself all their sins and go into a distant place, and the man will send it away into the desert.
Mbuzi lazima abebe juu yake mwenyewe uovu wote kwenda mahali pakiwa. Kule msituni, huyo mtu amwache mbuzi aende huru.
23 Aaron is to return to the Tent of Meeting, take off the linen clothes he put on before he went into the Most Holy Place, and leave them there.
Ndipo Haruni anapaswa kwenda tena humo kwenye hema ya mkutano na kuvua mavazi ya kitani ambayo amayavaa kabla hajaenda mahali patakatifu sana, na anatakiwa kuyaacha mavazi hayo pale.
24 He is to wash himself with water in the sanctuary and put on his own clothes. Then he will go out and sacrifice his burnt offering and the people's burnt offering that makes him and the people right.
Anapaswa aoshe mwili wake kwa maji mahali patakatifu, na avae nguo zake za kawaida; pia lazima atoke nje kutoa sadaka ya kuteketezwa na sadaka ya kuteketezwa na sadaka ya kuteketezwa kwaajili ya wale watu, na kwa njia hii anafanya upatanisho kwaajili yake mwenyewe na kwaajili ya watu.
25 He also must burn the fat of the sin offering on the altar.
Lazima yeye achome mafuta ya sadaka ya dhambi juu ya madhabahu.
26 The man who went and sent away the scapegoat must wash his clothes and wash himself with water; then he may come back into the camp.
Huyu mtu anayemwacha mbuzi msingiziwa aende huru anafua nguo zake na kuosha mwili wake katika maji; baada ya hayo, anaweza kurudi tena kambini.
27 The remains of the bull used for the sin offering and the goat for the sin offering, whose blood was brought into the Most Holy Place to purify it, must be taken outside the camp. Their skin, meat, and waste must be burned.
Yule fahali kwaajili ya sadaka ya dhambi na mbuzi kwaajili ya sadaka za dhambi, ambaye damu yake ililetwa kufanya upatanisho katika mahali patakatifu, lazima ipelekwe nje ya kambi. kule lazima wachome, ngozi zao, nyama yao na kinyesi chao.
28 The person who burns them must wash his clothes and wash himself with water; then he may come back into the camp.
Huyu anayechoma sehemu hizo lazima afue nguo zake na aoge mwili wake katika maji; baada ya hapo, anaweza kurudi tena kwenye kambi.
29 This regulation applies to you for all time. The tenth day of the seventh month is a day of self-denial for you. You are not to do any work. This applies to all who are native-born and also any foreigner who living among you,
Hii itakuwa sharti kwaajili yenu kwamba katika mwezi wa saba, kwenye siku ya kumi ya mwezi, mtanyenyekea wenyewe na msifanye kazi, iwe mwenyeji wa kuzaliwa au mgeni anayeishi kati yenu.
30 for on this day the process of making you right will be done, to make you clean from all your sins, clean before the Lord.
Hii ni kwasababu katika siku hii ya upatanisho utafanywa kwaajili yenu, kuwatakasa ninyi kutoka dhambi zenu zote ili mwe safi mbele za Yahwe.
31 It is a Sabbath of Sabbaths, a day of rest and self-denial. This regulation applies for all time.
Hii ni maalumu kwa Sabato ya kupumzika kwaajili yenu, na lazima mnyenyekee wenyewe na msifanye kazi. Hili litakuwa sharti kati yenu.
32 The priest who is anointed and dedicated to succeed his father as high priest shall carry out the ceremony of making things right, and put on the holy linen clothes.
Kuhani mkuu, ambaye atapakwa mafuta na kuwekwa wakfu kuwa kuhani mkuu katika nafasi ya baba yake, lazima afanye upatanisho huu na kuvaa mavazi ya kitani, hayo ni mavazi matakatifu.
33 He will carry out the purification of the Most Holy Place, the Tent of Meeting, and the altar, also making right the priests and all the people.
Lazima afanye upatanisho kwaajili ya mahali patakatifu sana; lazima afanye upatanisho kwaajili ya hema ya mkutano na madhabahu, na lazima afanye upatanisho kwaajili ya makuhani na kwaajili ya kusanyiko la watu.
34 This regulation applies to you for all time: once a year the Israelites have all their sins made right.” Moses did everything as the Lord had ordered.
Hii daima itakuwa sharti kwaajili yako, kufanya upatanisho kwaajili ya watu wa Israeli kwasababu ya dhambi zao zote, mara moja kwa kila mwaka.” Na ilikuwa ikifanika kama Yahwe alivyomwamuru Musa.