< Leviticus 14 >

1 The Lord told Moses,
Yahwe alizungumza na Musa, akisema,
2 “These are the regulations regarding those who have had a skin disease when they are declared clean having been brought to the priest.
“Hii itakuwa sheria kwaajili ya mtu aliyekufa kwenye siku ya utakaso. Lazima aletwe kwa kuhani.
3 The priest must go outside the camp and inspect the person. If the skin disease has healed,
Kuhani atakwenda nje ya kambi kumchunguza mtu kuona kama madhara ya ugonjwa wa ngozi yameponywa.
4 the priest shall have two ceremonially clean birds brought to him, also some cedar wood, crimson thread, and hyssop, on behalf of the person to be made clean.
Ndipo kuhani ataamuru kwamba mtu mwenye kutakaswa lazima achukue ndege safi wawili, waliohai, mti wa mwerezi, kitani nyekundu na hisopo.
5 The priest will order one of the birds to be killed over a clay pot filled with fresh water.
Kuhani atamwamuru kuua moja ya hao ndege juu ya maji safi yaliyo kwenye chungu cha udongo.
6 He will take the live bird together with the cedar wood, crimson thread, and hyssop, and dip them in the blood of the bird that was killed over the fresh water.
Ndipo kuhani atamchukua ndege aliyehai na mti wa mwerezi, na kitani nyekundu na hisopo, na vyote hivi, pamoja na ndege aliyehai atavichovya kwenye damu ya ndege aliyechinjiwa kwenye maji safi.
7 He will use the blood to sprinkle seven times the person being made clean of the skin disease. Then the priest will declare them clean and let the live bird fly away.
Ndipo kuhani atanyunyiza maji haya mara saba juu ya mtu anayetakaswa katika ugonjwa, na ndipo kuhani atamtangaza kuwa msafi. Ndipo kuhani atamwachia ndege aliyehai katika eneo wazi.
8 The one being made clean must wash their clothes, shave off all their hair, and wash themselves with water; then they will be will be ceremonially clean. After that they can enter the camp, but they must stay outside their tent for seven days.
Mtu aliyetakaswa atafua nguo zake, atanyoa nywele zake zote, ataoga kwa maji, na ndipo atakuwa safi. Baada ya hayo lazima aje kwenye kambi, lakini ataishi nje ya hema lake kwa siku saba.
9 On the seventh day they must shave off all their hair: their head, beard, eyebrows, and the rest of their hair. They must wash their clothes and wash themselves with water, and they will be clean.
Katika siku ya saba lazima anyoe nywele za kichwa chake, na lazima pia anyoe ndevu zake na nyusi. Lazima anyoe nywele zake zote, na lazima afue nguo zake na aoge kwenye maji; ndipo atakuwa safi.
10 On the eighth day they are to bring two male lambs and one female lamb, all a year old and without defects; a grain offering consisting of three-tenths of an ephah of best flour mixed with olive oil, and one ‘log’ of olive oil.
Katika siku ya nane lazima achukue dume wa wana kondoo wawili wasio na lawama, mwana kondoo jike wa mwaka mmoja asiye na lawama, na tatu ya kumi ya efa ya unga safi uliochanganywa mafuta kama sadaka ya nafaka, na kipimo kimoja cha mafuta.
11 The priest who conducts the ceremony will present the person to be made clean to the Lord, along with these offerings, at the entrance to the Tent of Meeting.
Kuhani ambaye amemtakasa mtu atamsimamisha mtu ambaye aliyemtakasa, pamoja na vile vitu, mbele ya Yahwe mahali pa kuingilia kwenye hema ya mkutano.
12 The priest will take one of the male lambs and present it as a guilt offering, together with the log of olive oil; and he will wave them before the Lord as a wave offering.
Kuhani atachukua mmoja wa wanakondoo dume na kumtoa kama sadaka ya hatia, pamoja na kipimo cha mafuta; atavitikisa kwa sadaka ya kutikiswa mbele ya Yahwe.
13 Then he will kill the lamb near the sanctuary where the sin offering and burnt offering are killed. The sin offering and the guilt offering belong to the priest; it is most holy.
Lazima aue mwana kondoo dume mahali ambapo wanapochinjia sadaka ya dhambi na sadaka ya kuteketezwa, katika eneo la hema, sababu sadaka ya dhambi ni ya kuhani, kama afanyavyo sadaka ya hatia, kwasababu ni takatifu zaidi.
14 The priest will put some of the blood from the guilt offering on their right earlobe, on their right thumb, and on the big toe of their right foot of the person being made clean.
Kuhani atachukua baadhi ya damu ya sadaka ya hatia na kuiweka kwenye ncha ya sikio la kulia la mtu yule wa kutakaswa, katika dole gumba la kulia, katika dole la mguu wa kulia.
15 The priest will pour some of the log of olive oil into his left palm,
Ndipo kuhani atachukua mafuta kutoka chombo na kuyamimina katika kiganja cha mkono wake wa kushoto, na kuzamisha kidole chake katika mafuta hayo yaliyo kwenye mkono wa kushoto,
16 dip his right index finger in it, and using his finger, sprinkle some of the olive oil seven times before the Lord.
na kunyunyiza baadhi ya mafuta kwa kidole mara saba mbele za Yahwe.
17 The priest will then use some of the rest of the olive oil remaining in his palm on the person being made clean, and put it on top of the blood of the guilt offering. This will be on their right earlobe, on their right thumb, and on the big toe of their right foot, on top of the blood of the guilt offering.
kuhani ataweka mafuta yaliyobaki kwenye mkono wake kwenye ncha ya sikio la kulia la mtu wa kutakaswa, juu ya dole gumba la mkono wa kulia, na katika dole kubwa la mguu wa kulia. Lazima aweke mafuta haya juu ya damu kutoka kwenye sadaka ya hatia.
18 What is left of the olive oil in his palm, the priest will put on the head of the person being made clean and then make them right before the Lord.
Kama kwa mafuta yaliyosalia kwamba katika mkono wa kuhani, atayaweka juu ya kichwa cha mtu ambaye atakaswaye, na kuhani atafanya utakaso kwaajili yake mbele za Yahwe.
19 The priest will sacrifice the sin offering to make the person right, so that they are now clean from their uncleanness. After that, the priest will kill the burnt offering
Ndipo kuhani atatoa sadaka ya dhambi na kufanya upatanisho kwaajili yake atakaswaye kwa sababu ya kutokuwa safi kwake, na badaye ataua sadaka ya kuchomwa.
20 and offer it on the altar, together with the grain offering, to make them right, and they will be clean.
Ndipo kuhani atatoa sadaka ya kuteketezwa na sadaka ya nafaka juu ya madhabahu. Kuhani atafanya upatanisho kwaajili ya mtu huyo, na ndipo atakuwa safi.
21 But those who are poor and can't afford these offerings must bring one male lamb as a guilt offering to be waved to make them right, together with a tenth an ephah of best flour mixed with olive oil for a grain offering, a log of olive oil,
Kwa namna hiyo, kama mtu ni masikini na hawezi kumudu matoleo haya, ndipo anaweza kuchukua kondoo mmoja dume kama sadaka ya hatia ya kutikiswa, kufanya upatanisho kwaajili yake mwenyewe, na moja ya kumi ya efa ya unga safi uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka, na chombo cha mafuta,
22 and two turtledoves or two young pigeons, whichever they can afford. One is to be used as a sin offering and the other as a burnt offering.
pamoja na njiwa wawili au kinda mbili za njiwa, ambao anaweza kupata; ndege mmoja atakuwa sadaka ya dhambi na mwingine sadaka ya kuteketezwa.
23 On the eighth day they are to take them to the priest at the entrance to the Tent of Meeting before the Lord so they can be made clean.
Katika siku ya nane lazima awalete kwa kuhani kwaajili ya utakaso, pakuigilia katika hema ya mkutano, mbele ya Yahwe.
24 The priest will take the lamb for the guilt offering, together with the log of olive oil, and wave them as a wave offering before the Lord.
Kuhani atachukua mwana kondoo kwaajili ya sadaka, na atachukua pamoja na kiasi cha mafuta ya mzeituni, na ataviinua juu kama anaviwasilisha kwa Yahwe.
25 After he kills the lamb for the guilt offering, the priest will take some of the blood of the guilt offering and put it on the right earlobe of the one being made clean, on their right thumb, and on the big toe of their right foot.
Atamuua mwana kondoo kwaajili ya sadaka ya hatia, na atachukua baadhi ya ya damu ya sadaka ya hatia na kuiweka juu ya ncha ya sikio la kulia la yule wakutakaswa, juu ya dole gumba la mkono wake wa kulia, na kwenye dole kubwa la mguu, wa kulia.
26 Then the priest will pour some of the olive oil into his left palm
Ndipo kuhani atamimina baadhi ya mafuta katika kiganja cha mkono wake wa kushoto,
27 and using his right index finger, will sprinkle some of the oil from his left palm seven times before the Lord.
na atanyunyiza kwa kidole chake cha kulia baadhi ya mafuta ambayo yako kwenye mkono wa kushoto mara saba mbele za Yahwe.
28 The priest shall also put some of the olive oil in his palm on the right earlobe of the person being made clean, on their right thumb, and on the big toe of his right foot, in the same places as the blood of the guilt offering.
Ndipo kuhani ataweka kiasi cha mafuta ambayo yako kwenye mkono wake kwenye ncha ya sikio la yule mtu wa kutakaswa, katika dole gumba lake la mkono wa kulia, na dole kubwa la mguu wa kulia, maeneo yale yale ambayo kaweka damu ya sadaka ya hatia.
29 What is left of the olive oil in his palm, the priest will put on the head of the person being made clean and then make them right before the Lord.
Ataweka mafuta yaliyobaki yaliyo mkononi mwake juu ya yule wakutakaswa, kufanya upatanisho kwaajili yake mbele za Yahwe.
30 Then they must sacrifice one of the turtledoves or young pigeons, whichever they can afford,
Lazima atoe sadaka ya njiwa au makinda ya njiwa, yale ambayo mtu ameweza kupata -
31 one as a sin offering and the other as a burnt offering, along with the grain offering. This is how the priest will make the person right and clean before the Lord.
moja kama ya sadaka ya dhambi na nyingine kama sadaka ya kuteketezwa, pamoja na sadaka ya nafaka. Ndipo kuhani atafanya upatanisho kwaajili ya yule ambaye atatakaswa mbele za Yahwe.
32 These are the regulations for those who have a skin disease and can't afford the usual offerings to make people clean.”
Hii ni sheria kwaajili ya mtu kwake kuna athari za ugonjwa wa ngozi, ambaye hawezi kumudu kiwango cha sadaka kwaajili ya utakaso wake.”
33 Then the Lord told Moses and Aaron,
Yahwe alizungumza na Musa na Haruni, akisema,
34 “When you get to Canaan, the land I'm giving you to own, if I put some mold into a house there and contaminate it,
“Wakati mtakuja katika nchi ya Kanaani ambayo nimewapa kama miliki, na kama naweka ukungu unaenea ndani ya nyumba katika nchi ya miliki yenu,
35 the owner of the house must come and tell the priest, ‘It seems my house has something like mold.’
ndipo yeye ambaye anamiliki nyumba ile lazima aje na kumwambia kuhani. Lazima aseme 'Inaonekana kwangu kuna kitu fulani kama ukungu ndani ya nyumba yangu.'”
36 The priest must order the house to be emptied before he goes in to inspect the mold, so that nothing in the house will be declared unclean. Once that's done, the priest is to go in and inspect the house.
Ndipo kuhani ataamuru kwamba watoe vitu vyote ndani kabla hajaenda ndani kuona uthibitisho wa ukungu, kiasi kwamba hakuna ndani ya nyumba kitakachofanywa najisi. Badaye kuhani lazima aende ndani kuona humo ndani.
37 He will examine the house and see whether the mold on the walls is made up of green or red indentations that go under the surface,
Yeye lazima achunguze ukungu kuona kama umo katika kuta za nyumba, na kuona ikiwa kunaonekana ukijani au wekundu katika bonde za mwonekano wa kuta.
38 the priest shall go out of door and seal the house for seven days.
Kama nyumba inao ukungu, ndipo kuhani atatoka nje ya nyuma na kufunga mlango wa nyumba kwa siku saba.
39 On the seventh day the priest will return and inspect the house again. If the mold has spread on the walls,
Ndipo kuhani atarudi tena katika siku ya saba na kuichunguza kuona kama ukungu umeenea katika kuta za nyumba.
40 he will order the affected stones to be removed and disposed of in an unclean area outside the town.
Kama hivyo, ndipo kuhani ataamuru kwamba wayaondoe mawe ambayo ukungu umepatikana na yatupwe katika sehemu najisi nje ya mji.
41 Then he will order the all the plaster inside of the house to be scraped off and dumped in an unclean area outside the town.
Yeye atataka kuta zote za ndani ya nyumba zikwanguliwe, na lazima achukue vitu vilivyochafuliwa na hivyo vilivyokwanguliwa nje ya mji na kuvitupa kwenye eneo lisilosafi.
42 Different stones must be used to replace the ones removed, and new plaster will be needed replaster the house.
Lazima wayachukue mawe mengine na kuyaweka katika sehemu ya mawe yaliyoondolewa, na lazima watumie udongo mpya kupigia lipu nyumba.
43 If the mold returns and affects the house again even after the stones have been removed and the house has been scraped and replastered,
Kama ukungu unakuja tena na unaingia katika nyumba ambayo mawe yameondolewa na kuta zimekwanguliwa na kupigwa lipu upya,
44 the priest must come and inspect it. If he sees the mold has spread in the house, it is a harmful mold; the house is unclean.
ndipo kuhani lazima aje aingie ndani na kuchunguza nyumba kuona kama ukungu umeenea ndani ya nyumba. Kama hivyo, huo ni ukungu mbaya, na nyumba ni najisi.
45 It must be demolished, and all its stones, timbers, and plaster must be taken and dumped in an unclean area outside the town.
Nyumba hiyo lazima iangushwe chini. Hayo mawe, mbao, na lipu yote ndani ya nyumba lazima vibebwe kupelekwa nje ya mji kwenye sehemu najisi.
46 Anyone who goes into the house during any time that it is sealed will be unclean until the evening.
Kwa nyongeza, yeyote anaenda ndani ya nyumba wakati imefungwa atakuwa najisi mpaka jioni.
47 Anyone who sleeps or eats in the house must wash their clothes.
Na yeyote aliyelala ndani ya nyumba lazima afue nguo zake, na yeyote aliyekula ndani ya nyumba lazima afue nguo zake.
48 However, if when the priest comes and inspects it and finds that the mold hasn't reappeared after the house was replastered, he shall declare the house clean because the mold is gone.
Kama kuhani akaingia hiyo kuichunguza kuona ikiwa ukungu umeenea katika nyumba baada ya nyumba kupigwa lipu, ndipo, kama ukungu umetoweka, ataitangaza nyumba hiyo kuwa ni safi.
49 He will bring two birds, cedar wood, crimson thread, and hyssop to make the house clean.
Ndipo kuhani lazima achukue ndege wawili kuitakasa nyumba, na mti wa mwelezi, na sufu nyekundu, na hisopo.
50 He will kill one of the birds over a clay pot filled with fresh water.
Atamuua ndege mmojawapo katika maji masafi kwenye dumu la udongo.
51 He will dip the live bird, the cedar wood, crimson thread, and hyssop, in the blood of the bird that was killed and the fresh water, and sprinkle the house seven times.
Atachukua mti wa mwerezi, hisopo, sufu nyekundu na ndege aliyehai, na kuvichovya kwenye damu ya ndege aliyekufa, kwenye maji safi, na kunyunyizia nyumba mara saba.
52 He will make the house clean with the bird's blood, the fresh water, the live bird, the cedar wood, the hyssop, and the crimson thread.
Ataitakasa nyumba kwa damu ya ndege na maji safi, pamoja na ndege aliyehai, mti wa mwerezi, hisopo, na sufu nyekundu. Lakini atamwachia ndege aliyehai aende nje ya mji mashambani.
53 Then he will let the live bird fly away outside the town. This is how he will make the house right, and it will be clean.
Kwa njia hii lazima afanye upatanisho kwaajili ya nyumba, na itakuwa safi.
54 These are the regulations for any infectious skin disease, for a scabby infection,
Hii ni sheria kwa aina zote za athari ya ugonjwa wa ngozi na vitu vyote vinavyosababisha ugonjwa kama huo, na kwaajili ya kuwashwa,
55 for mold on clothing and in a house,
na kwa ukungu kwenye mavazi na nyumba,
56 as well as for a swelling, rash, or spot.
kwaajili ya uvimbe, kwaajili ya vipele, madoa,
57 They are used to decide whether something is clean or unclean. These are the regulations regarding skin diseases and mold.”
kutambua wakati wowote tatizo hili ni najisi au lini limetakaswa. Hii ni sheria kwaajili ya athari za ugonjwa wa ukungu.

< Leviticus 14 >