< Leviticus 11 >
1 The Lord told Moses and Aaron,
Yahweh akazungumza na Musa na Aroni, akasema,
2 “Give these instructions to the Israelites. These are the animals you are allowed to eat:
“Sungumzeni na watu wa Israeli muwaambie, 'Hivi ndivyo viumbe vyenye uhai ambavyo mwaweza kula miongoni mwa wanyama walioko juu ya nchi.
3 any animal that both has a divided hoof and also chews the cud.
Mnaweza kula mnyama yeyote aliye na kwato zenye kugawanyika na ambaye pia hucheua.
4 However, if it either chews the cud, or has a divided hoof, then you may not eat it. These include: the camel, which though it chews the cud doesn't have a divided hoof, so it is unclean for you.
Hata hivyo, kuna baadhi ya wanyama ambao ama hawacheui au hana kwato zilizogawanyika, nanyi msiwale hao, wanyama kama ngamia, kwa sababu yeye hucheua lakini hana kwato zilizogawanyika. Kwa hiyo ngamia ni najisi kwenu.
5 The rock hyrax, which though it chews the cud doesn't have a divided hoof, so it is unclean for you.
Pimbi pia: kwa sababu yeye hucheua lakini hana kwato zilizogawanyika mara mbili, huyo pia ni najisi kwenu.
6 The hare, which though it chews the cud doesn't have a divided hoof, so it is unclean for you.
Na sungura pia: kwa sababu yeye hucheua lakini hana kwato zilizogawanyika mara mbili, huyu naye ni najisi kwenu.
7 The pig, which though it has a divided hoof doesn't chew the cud, so it is unclean for you.
Na nguruwe pia: ingawaje yeye anazo kwato zilizogawanyika lakini hacheui, kwa hiyo yeye ni najisi kwenu.
8 You are not to eat their meat or touch their bead bodies. They are unclean for you.
Msile aina yoyote ya nyama yao, wala msiiguse mizoga yao. Hao ni najisi kwenu.
9 You are allowed to eat any creature with fins and scales that lives in the water, whether in the sea or in fresh water.
Nao wanyama waishio majini mnaoweza kuwala ni wale wote walio na mapezi na magamba, iwe waliomo baharini au mitoni.
10 But you are not allowed to eat any of the many creatures that don't have fins and scales that live in the water, whether in the sea or in fresh water.
Lakini viumbe wote hai wasio na mapezi na magamba waliomo baharini au mitoni, pamoja na wale waendao majini na viumbe hai waliomo majini —watakuwa chukizo kwenu.
11 They are repulsive. You must not eat their meat, and you must treat their dead bodies as repulsive.
Kwa kuwa watakuwa chukizo, msile nyama yao, pia mizoga yao sharti itakuwa chukizo.
12 All such water creatures that don't have fins and scales are to be repulsive to you.
Chochote kisichokuwa na mapezi au magamba kilichomo majini ni lazima kiwe chukizo kwenu.
13 As for the birds, these must not be eaten because they are repulsive: eagle, griffon vulture, bearded vulture,
Nao ndege mtakaowachukia na msiopaswa kuwala ni hawa wafuatao: tai, furukombe, kipungu,
14 buzzard, kite and similar birds of prey,
mwewe mwekundu, aina yoyote ya kipanga,
16 tawny owl, long-eared owl, gulls, any kind of hawk,
kiruka-njia, kipasuasanda, Shakwe, na aina yoyote ya mwewe.
17 little owl, fish owl, eagle owl,
Ni lazima pia bundi mdogo na bundi mkubwa muwaone kuwa chukizo, mnandi,
18 barn owl, desert owl, Egyptian vulture,
bundi mweupe na mwari,
19 storks and any kind of heron, hoopoe, and bats.
korongo na ina zote za koikoi, huduhudi na popo pia.
20 All flying insects that crawl are repulsive to you.
Wadudu wote wenye mabawa wanatembea kwa miguu minne kwenu ni machukizo.
21 But you can eat the following kinds of flying insects that crawl: those that have jointed legs they use to jump.
Lakini manaweza kula wadudu wenye mabawa wanaotembea kwa miguu minne ya kurukia ardhini yenye vifundo.
22 So in this category you can eat any kind of locust, bald locust, cricket, or grasshopper.
Na manaweza kula kula aina zote za nzige, senene, parare, au panzi.
23 All other flying insects that crawl are repulsive to you,
Lakini wadudu wote warukao wenye miguu minne ni chulkizo kwenu.
24 and will make you unclean. If you touch their dead bodies you will be unclean until the evening,
Nanyi mtakuwa najisi hata jioni kutokana na wanyama hawa endapo mtagusa mizogo yao.
25 and if you pick up one of their dead bodies you must wash your clothes, and you will be unclean until the evening.
Na yeyote atakayeokota mojawapo wa mizoga yao ni lazima atazifua ngua zake naye atakuwa najisi hata jioni.
26 Every animal with hooves that are not divided, or that does not chew the cud, is unclean for you. If you touch any of them you will be unclean.
Mnyama yeyote ambaye anazo kwato ziliachana ambazo hazikugawanyika kabisa au hacheui huyo ni najisi kwenu. Yeyote awagusaye atakuwa najisi.
27 Any four-legged animal that walks on its paws are unclean for you. If you touch their dead bodies you will be unclean until the evening,
Mnyama yeyote anayetembea kwa vitanga vyake miongoni mwa wanyama waendao kwa miguu yote minne ni najisi kwenu. Yeyote agusaye mzoga kama huo atakuwa najisi hata jioni.
28 and if you pick up one of their dead bodies you must wash your clothes, and you will be unclean until the evening. They are unclean for you.
Na yeyote aokotaye mzoga kama huo ni zazima atazifua nguo zake na kuwa najisi hata jioni. Wanyama hawa watakuwa najisi kwenu.
29 The following animals that run along the ground are unclean for you: rats, mice, any kind of large lizard,
Kuhusiana na wanyama wataambaao juu ya ardhi, hawa ndiyo walio najisi kwenu: kicheche, panya, aina zote za mijusi mikubwa, guruguru,
30 gecko, monitor lizard, wall lizard, skinks, and chameleon.
kenge, mijusi ya ukutani, goromoe, na kinyonga.
31 These animals that run along the ground are unclean for you. If you touch a dead one of them you will be unclean until the evening.
Wanyama hawa wote ambao hutambaa, hawa ndiyo watakuwa najisi kwenu. Yeyote awagusaye atakuwa njisi hata jioni.
32 Anything that one of them dies and lands on becomes unclean. Whatever it is—something made of wood, clothing, leather, sackcloth, or any work tool—it must be washed with water and will be unclean until the evening. Then it will become clean.
Na iwapo mmoja wao anakufa na kuanguka juu ya chombo, chombo hicho kitakuwa najisi, ama kiwe kimetengenezwa kwa mbao, nguo, ngozi, au gunia. Kiwe chombo cha namna gani na kiwe kwa matumizi gani, ni lazima kitalowekwa katika maji nacho kitakuwa najisi hata jio. Kisha kitakuwa safi.
33 If one of them falls into a clay pot, all that's in it becomes unclean. You must smash the pot.
Kwa hiyo kila chungu ambacho mnyama najisi atakiangukia juu yake au ndani yake, chochote kilichomo kwenye chungu hicho kitakuwa najisi, na ni lazima mtakivunja chungu hicho.
34 If water from that pot touches any food, that food becomes unclean, and any drink from a pot like that also becomes unclean.
Vyakula vyote ambavyo ni safi na kilichuhusiwa kuliwa, lakini kikaingiwa na maji kutoka kwenye chungu najisi kilichoanguka, nacho kitakuwa najisi.
35 Anything that one of their dead bodies falls on becomes unclean. If it's an oven or a stove, it must be smashed. It is permanently unclean for you.
Na kitu chochote kinachoweza kunywewa kutoka kwenye chungu kama hicho kitakuwa najisi. Kila kitu kitakachoangukiwa juu yake na kipande cha mzoga wa mnyama najisi nacho kitakuwa najisi, ama liwe ni jiko au vyungu vya kupikia. Ni najisi na ni lazima kiwe najisi kwenu.
36 On the other hand, if it's a spring or cistern containing water then it will remain clean, but if you touch one of these dead bodies in it you will be unclean.
Chemchemi au kisima cha maji ya kunywa yanapokusanyika patabaki kuwa safi iwapo kiumbe najisi kama hicho kitaangukia humo. Lakini ikiwa yeyote anaugusa mzoga wa mnyama aliye najisi uliomo ndani ya maji, yeye atakuwa najisi.
37 Similarly, if one of their dead bodies falls on any seed used for sowing, the seed remains clean;
Iwapo sehehemu yoyote ya mzoga wa mnyama aliyenajisi inaangukia juu ya mbegu zozote zilizo kwa ajili ya kupanda. Mbegu hizo zitakuwa bado zingali safi.
38 but if the seed has been soaked in water and one of their dead bodies falls on it, it is unclean for you.
Lakini kama maji yanawekwa juu ya mbegu, na kama sehemu ya mzoga unaangukia juu yake, nazo zitakuwa najisi kwenu.
39 If an animal that you are allowed to eat dies, anyone who touches the dead body will be unclean until the evening.
Iwapo mnyama yeyote awezaye kuliwa anakufa, naye yeyote amgusaye atakuwa najisi hata jioni.
40 If you eat anything from the dead body you must wash your clothes and you will be unclean until the evening. If you pick up the dead body you must wash your clothes and you will be unclean until the evening.
Na yeyote alaye chochote cha mzoga huo atalazimika kufua nguo zake naye atakuwa anjisi hata jioni. Na yeyote aokotaye mzoga kama huo atafua nguo zake na kuwa najisi hata jioni.
41 Every animal that crawls along the ground is repulsive—you must not eat it.
Kila mnyama atambaaye juu ya ardhi atakuwa chukizo; hatakuwa wa kuliwa.
42 Don't eat any animal that crawls along the ground, whether it moves on its belly or walks on four feet or many feet. All such animals are repulsive.
Chochote kitambaacho kwa kujivuta juu ya tumbo lake, na chochote kitembeacho kwa miguu yake yote minne, au chochote kilicho na miguu mingi—wanyama wote ambao hutambaa juu ya nchi, hawa msiwale, kwa sababu watakuwa machukizo.
43 Don't defile yourselves by any such crawling animal. Don't make yourselves unclean or defiled by them,
Msijinajisi wenyewe kwa kiumbe chochote nnajisi kitaambacho; msijinasi wenyewe kwavyo, ili kwamba msije mkachafuliwa navyo.
44 because I am the Lord your God; so dedicate yourselves and be holy, because I am holy. Don't defile yourselves by any animal that crawls along the ground.
Kwa kuwa Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu. Nanyi lazima muwe watakatifu, kwa hiyo na iweni watakatifu, kwa sababu Mimi ni mtakatifu. Haiwapasi kujichafua kwa aina yoyote ya kiendacho juu ya nchi.
45 I am the Lord who led you out of Egypt so that I could be your God. So be holy, because I am holy.
Kwa kuwa Mimi ndimi Yahweh, aliyewaleta ninyi kutoka nchi ya Misri, ili niwe Mungu wenu. Kwa hiyo lazima muwe watakatifu, kwa kuwa Mimi ni mtakatifu.
46 These are the regulations about animals, birds, everything that lives in the water, and all animals that crawl along the ground.
Hii ndiyo sheria kuhusu wanyama, ndege, kila kiumbe hai kiendacho majini, na ya kila kiumbe kitambaacho juu ya nchi,
47 You must recognize the difference between unclean and clean, between those animals that can be eaten and those that can't.”
kwa jili ya kilie kinachopaswa kutofautishwa kati ya kilicho najisi na kilicho safi, na kati ya vitu vilivyokufa na vilivyo hai ambavyo vyaweza kuliwa na vitu vyenye uihai visivyoweza kuliwa.”