< Judges 12 >

1 Then the Ephraimites were called up and crossed the Jordan to Zaphon. They said to Jephthah, “Why did you go and fight the Ammonites without summoning us to go with you? We're going to burn your house down with you inside it!”
Watu wa Efraimu wakaita majeshi yao, wakavuka kwenda Zafoni, wakamwambia Yefta, “Kwa nini mmekwenda kupigana na Waamoni bila kutuita ili twende pamoja nawe? Basi tutaichoma moto nyumba yako, pamoja nawe ukiwa ndani yake.”
2 “I was a man with a great fight on my hands,” Jephthah replied. “I and my people were fighting the Ammonites. When I called on you for help, you didn't come and help save me from them.
Yefta akajibu, “Mimi na watu wangu tulikuwa na ugomvi mkubwa na Waamoni, hata ingawa niliwaita hamkuniokoa katika mkono wao.
3 When I realized that you weren't going to help, I took my life in my hands and went to fight the Ammonites, and the Lord made me victorious over them. So why have you come here today to attack me?”
Nilipoona kuwa hamkunipa msaada nikauhatarisha uhai wangu na nikavuka kupigana na Waamoni. Naye Bwana akanipatia ushindi dhidi yao. Sasa kwa nini mnanijia leo ili kupigana nami?”
4 Jephthah summoned all of the men of Gilead and fought against the Ephraimites. The men of Gilead killed them because the Ephraimites taunted them, saying, “You Gileadites are nothing more than escapees living among Ephraim and Manasseh.”
Ndipo Yefta akakusanya watu wa Gileadi pamoja na kupigana na Efraimu. Wagileadi wakawashinda Efraimu, kwa kuwa Waefraimu walisema, “Ninyi Wagileadi ni watoro mliotoroka toka Efraimu na Manase.”
5 The Gileadites took control of the fords over the Jordan River that led to Ephraim's territory, and when an Ephraimite escapee from the battle would come and ask, “Let me cross over,” the Gileadites would question him, “Are you an Ephraimite?” If he answered, “No,”
Wagileadi wakaviteka vivuko vya Yordani dhidi ya hao Waefraimu, kisha ilikuwa yeyote yule aliyenusurika katika Efraimu aliposema, “Niache nivuke,” hao watu wa Gileadi walimuuliza, “Je wewe ni Mwefraimu?” Kama alijibu “Hapana,”
6 they would tell him, “Say Shibboleth.” If he was from Ephraim he would say “Sibboleth” because he couldn't pronounce it right, and they'd grab him and kill him there at the Jordan fords. A total of 42,000 were killed at that time.
walimwambia, “Sawa, sema ‘Shibolethi.’” Iwapo alitamka, “Sibolethi,” kwa sababu hakuweza kutamka hilo neno sawasawa, walimkamata na kumuua hapo kwenye vivuko vya Yordani. Waefraimu 42,000 waliuawa wakati huo.
7 Jephthah led Israel as judge for six years. Then he died and was buried in one of Gilead's towns.
Yefta akawa mwamuzi wa Waisraeli kwa muda wa miaka sita. Basi Yefta akafa, akazikwa katika mmojawapo wa miji ya Gileadi.
8 After Jephthah, Ibzan of Bethlehem led Israel as a judge.
Baada yake, Ibzani wa Bethlehemu akawa mwamuzi wa Israeli.
9 He had thirty sons and thirty daughters. He married off his daughters to men of other tribes, and he brought in thirty wives from other tribes to marry his sons. Ibzan led Israel as judge for seven years.
Alikuwa na wana thelathini na binti thelathini. Akawaoza binti zake kwa watu wengine nje ya ukoo wake, na kuwatwalia wanawe wanawake thelathini toka nje ya ukoo wake. Ibzani akawa mwamuzi wa Israeli kwa muda wa miaka saba.
10 Then Ibzan died and was buried in Bethlehem.
Ibzani akafa, akazikwa huko Bethlehemu.
11 After him, Elon the Zebulunite led Israel as judge for ten years.
Baada yake Eloni, Mzabuloni, akawa mwamuzi wa Israeli, naye akawaamua kwa muda wa miaka kumi.
12 Then he died and was buried at Aijalon in the territory of Zebulun.
Kisha Eloni akafa, akazikwa katika Aiyaloni, katika nchi ya Zabuloni.
13 After him, Abdon, son of Hillel, from Pirathon, led Israel as judge.
Baada yake, Abdoni mwana wa Hileli, Mpirathoni, akawa mwamuzi wa Israeli.
14 He had forty sons and thirty grandsons, who rode seventy donkeys. He led Israel as judge for eight years.
Naye akazaa wana arobaini na wana wa wanawe thelathini waliopanda punda sabini. Akawa mwamuzi wa Israeli kwa muda wa miaka minane.
15 Then he died and was buried at Pirathon in the territory of Ephraim, in the hill country of the Amalekites.
Ndipo Abdoni mwana wa Hileli, Mpirathoni, akafa, naye akazikwa huko Pirathoni katika Efraimu, katika nchi ya vilima ya Waamaleki.

< Judges 12 >