< Joshua 20 >

1 Then the Lord told Joshua,
Baada ya hayo, Yahweh akamwambia Yoshua,
2 “Tell the Israelites, ‘Assign sanctuary towns, as I instructed you through Moses.
“Waambia watu wa Israeli, na kusema, 'Chagueni miji ya makimbilio ambayo niliwaambia kupitia kwa Musa.
3 Then any man who kills somebody by accident, unintentionally, can run there and they will be protected from those who wish to take revenge.
Fanyeni hivi ili mtu akiua mtu bila kukusudia aweze kwenda huko. Miji hii itakuwa ni sehemu ya kukimbilia kutoka kwa mtu yeyote yule anayetaka kulipiza kisasi kwa damu ya mtu aliyeuliwa.
4 When he gets to one of these towns, he shall state his case to the elders at the town gates. They must allow him to enter, and they will also arrange a place for him to stay.
Atakimbilia kwa mji mmoja miongoni mwa miji hiyo na atasimama mlangoni mwa lango la mji, na ataeleza kesi yake kwa wazee wa mji ule. Kisha watamwingiza ndani ya mji na watampatia sehemu yake ya kuishi miongoni mwao.
5 If the one seeking revenge comes looking for the man, they must not hand the one who committed manslaughter over to him, because he killed someone unintentionally and without deliberate hatred.
Na kama mtu akija akataka kulipiza kisasi kwa damu ya mtu yule ambaye aliuliwa, ndipo watu wa mji hawatatakiwa kumtoa kwa wenye mamlaka mtu huyo aliyeua. Hawaruhusiwi kufanya hivyo kwasababu alimwua jirani bila kukusudia na hakuwa na chuki naye hapo awali.
6 He shall remain in that town until he has received a public trial and a verdict has been given, and until the death of the high priest of the time. Then he is free to return to his home, back to the town from where he ran away.’”
Ni lazima akae katika mji ule mpaka pale atakapokuwa amesimama mbele ya kusanyiko kwa ajili ya kuhukumiwa, hadi pale atakapokufa mtu yule anayetumika katika nafasi ya kuhani mkuu katka siku hizo. Na kisha mtu yule aliyeua bila kukusudia aweza kurudi nyumbani kwake, katika mji ule ulikotoka.
7 So they assigned the following sanctuary towns: Kedesh of Galilee, in the hill country of Naphtali; Shechem, in the hill country of Ephraim; and Kiriath-arba (or Hebron), in the hill country of Judah.
Kwahiyo, Waisraeli wakaichaguia Kedeshi iliyoko Galilaya katika nchi ya milima ya Nafutali, Shekemu katika nchi ya milima ya Efraimu, na Kiriathi Arba (ambayo ndio Herbroni) katika nchi ya milima ya Yuda.
8 On the other side of the Jordan, east of Jericho, they assigned: Bezer, in the wilderness on the plateau, from the tribe of Reuben; Ramoth in Gilead, from the tribe of Gad; and Golan in Bashan, from the tribe of Manasseh.
Katika ng'ambo ya Yordani mashariki mwa Yeriko, walichagua mji wa Bezeri huko nyikani katika nyanda za kabila la Rubeni; na Ramothi Gileadi kutoka kabila la Gadi; na Golani katika Bashani, kutoka katika kabila la Manase.
9 These were the assigned towns for all the Israelites, as well as for the foreigners living among them. Anyone who unintentionally killed someone could go there so they would not be killed by those who wished to take revenge before they had received a public trial and been given a guilty verdict.
Hii ni miji iliyochaguliwa kwa ajili ya watu wote wa Israeli na kwa ajili ya wageni wanaoishi miongoni mwao, ili kwamba mtu yeyote amwuaye mtu bila kukusudia aweza kukimbilia huko kwa ajili ya kupata usalama. Mtu huyu hatakufa kwa mkono wa mtu yule anayetake kulipiza kisasi cha damu iliyomwagwa, mpaka hapo kwanza mtuhumiwa atakaposimama mbele ya kusanyiko la watu.

< Joshua 20 >