< Joshua 19 >
1 The second lot cast went to the tribe of Simeon, by families. The land was within the land allotted to the tribe of Judah.
Kura ya pili ikaangukia kabila la Simeoni, ukoo kwa ukoo. Urithi wao ulikuwa ndani ya eneo la Yuda.
2 Their allocation included Beersheba, Sheba, Moladah,
Ulijumuisha: Beer-Sheba (au Sheba), Molada,
3 Hazar-shual, Balah, Ezem,
Hasar-Shuali, Bala, Esemu,
4 Eltolad, Bethul, Hormah,
Eltoladi, Bethuli, Horma,
5 Ziklag, Beth-marcaboth, Hazar-susah,
Siklagi, Beth-Markabothi, Hasar-Susa,
6 Beth-lebaoth, and Sharuhen—thirteen towns with their associated villages.
Beth-Lebaothi na Sharuheni; hii ilikuwa miji kumi na mitatu pamoja na vijiji vyake.
7 Also: Ain, Rimmon, Ether, and Ashan—four towns with their associated villages,
Pia Aini, Rimoni, Etheri, na Ashani; hii ilikuwa miji minne na vijiji vyake,
8 as well as all the villages around these towns as far as Baalath-beer (or Ramah of the Negev). This was the land allotted to the tribe of Simeon, by families.
pamoja na vijiji vyote vinavyoizunguka miji hii mpaka Baalath-Beeri (ambayo ndiyo Rama iliyo katika Negebu). Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Simeoni ukoo kwa ukoo.
9 The allocation of the tribe of Simeon was part of that given to the tribe of Judah, since what the tribe of Judah had received was too large for them.
Urithi wa Wasimeoni ulitolewa kutoka fungu la Yuda, kwa kuwa fungu la Yuda lilikuwa kubwa kuliko walivyohitaji. Hivyo kabila la Simeoni lilipewa urithi wao ndani ya eneo la Yuda.
10 The third lot cast went to the tribe of Zebulun, by families. The boundary of their allocation began at Sarid,
Kura ya tatu ikaangukia kabila la Zabuloni, ukoo kwa ukoo: Mpaka wa urithi wao uliendelea hadi Saridi.
11 and then went west past Maralah, touched Dabbeshah, and then the brook near Jokneam.
Kuelekea upande wa magharibi ukafika Marala, ukagusa Dabeshethi, na kuendelea mpaka kwenye bonde karibu na Yokneamu.
12 Going the other way from Sarid, the boundary headed east to the border of Kislot-tabor, on to Daberath, and then up to Japhia.
Ukageuka mashariki, kuanzia Saridi kuelekea mawio ya jua hadi kwenye nchi ya Kisiloth-Tabori, na kwenda hadi Daberathi, kupanda Yafia.
13 From there it ran east to Gath-hepher, Eth-kazin, and on to Rimmon, and turned towards Neah.
Kisha ukaendelea mashariki hadi Gath-Heferi na kufika Eth-Kasini, ukatokea Rimoni na kugeuka kuelekea Nea.
14 There the boundary turned north to Hannathon, ending at the valley of Iphtah-el.
Huko mpaka ukazungukia upande wa kaskazini hadi Hanathoni na kuishia katika Bonde la Ifta-Eli.
15 The towns included: Kattath, Nahalal, Shimron, Idalah, and Bethlehem—twelve towns with their associated villages.
Miji mingine iliyojumuishwa ni Katathi, Nahalali, Shimroni, Idala na Bethlehemu. Kulikuwa na miji kumi na miwili pamoja na vijiji vyake.
16 This was the allocation—the land, towns, and villages—given to the tribe of Zebulun, by families.
Miji hii na vijiji vyake ilikuwa ndio urithi wa Zabuloni, ukoo kwa ukoo.
17 The fourth lot cast went to the tribe of Issachar, by families.
Kura ya nne ikamwangukia Isakari, ukoo kwa ukoo.
18 Their land included these towns: Jezreel, Kesulloth, Shunem,
Eneo lao lilijumuisha: Yezreeli, Kesulothi, Shunemu,
19 Hapharaim, Shion, Anaharath,
Hafaraimu, Shioni, Anaharathi,
20 Rabbith, Kishion, Ebez,
Rabithi, Kishioni, Ebesi,
21 Remeth, En-gannim, En-haddah, and Beth-pazzez.
Remethi, En-Ganimu, En-Hada na Beth-Pasesi.
22 The boundary also reached the towns of Tabor, Shahazumah, and Beth-shemesh, and ended at the Jordan River—sixteen towns with their associated villages.
Mpaka ule ukagusa Tabori, Shahasuma na Beth-Shemeshi, na ukaishia kwenye Yordani. Ilikuwa miji kumi na sita, pamoja na vijiji vyake.
23 This was the allocation—the land, towns, and villages—given to the tribe of Zebulun, by families.
Miji hii pamoja na vijiji vyake ilikuwa urithi wa kabila la Isakari, ukoo kwa ukoo.
24 The fifth lot cast went to the tribe of Asher, by families.
Kura ya tano ikaangukia kabila la Asheri, ukoo kwa ukoo.
25 Their allocation included the towns of Helkath, Hali, Beten, Acshaph,
Eneo lao lilijumuisha: Helkathi, Hali, Beteni, Akishafu,
26 Allammelech, Amad, and Mishal. Their boundary reached Carmel and Shihor-libnat in the west.
Alameleki, Amadi na Mishali. Upande wa magharibi mpaka uligusa Karmeli na Shihor-Libnathi.
27 Then it turned east towards Beth-dagon, reaching the land of Zebulun and the valley of Iphtah-el. From there it headed north to Beth-emek and Neiel, and continued north to Cabul, and on through to
Tena ukageuka mashariki kuelekea Beth-Dagoni, ukagusa Zabuloni na Bonde la Ifta-Eli, ukaenda upande wa kaskazini hadi Beth-Emeki na Neyeli, ukipitia Kabul upande wa kushoto.
28 Ebron, Rehob, Hammon, Kanah, and on up to Great Sidon.
Ukaendelea hadi Abdoni, Rehobu, Hamoni na Kana, na kufika Sidoni Kuu.
29 The boundary then turned towards Ramah and then the fortified town of Tyre, turning to Hosah and ending at the sea. Towns included Mehebel, Aczib,
Mpaka huo ukageukia nyuma kuelekea Rama na kwenda hadi kwenye mji wenye ngome wa Tiro, ukageuka kuelekea Hosa na kutokeza baharini katika eneo la Akzibu,
30 Ummah, Aphek, and Rehob—twenty-two towns with their associated villages.
Uma, Afeki na Rehobu. Ilikuwepo miji ishirini na miwili, pamoja na vijiji vyake.
31 This was the allocation—the land, towns, and villages—given to the tribe of Asher, by families.
Miji hii pamoja na vijiji vyake ilikuwa ndio urithi wa kabila la Asheri, ukoo kwa ukoo.
32 The sixth lot cast went to the tribe of Naphtali, by families.
Kura ya sita ikaangukia kabila la Naftali, ukoo kwa ukoo:
33 Their boundary began at Heleph, by the oak at Zaananim, and went across to Adami-nekeb, Jabneel, and up to Lakkum, and ending at the Jordan.
Mpaka wao uliendelea kutoka Helefi na kwenye mti mkubwa ulio katika Saananimu, ukipitia Adami-Nekebu na Yabineeli hadi Lakumu, na kuishia katika Mto Yordani.
34 Then the boundary headed west to Aznoth-tabor, and on to Hukkok. It reached the land of Zebulun on the south, the land of Asher on the west, and the Jordan on the east.
Mpaka ukaendelea magharibi kupitia Aznoth-Tabori na kutokea Hukoki. Ukagusa Zabuloni upande wa kusini, Asheri upande wa magharibi, na Yordani upande wa mashariki.
35 The fortified towns included: Ziddim, Zer, Hammath, Rakkath, Kinnereth,
Miji yenye ngome ilikuwa Sidimu, Seri, Hamathi, Rakathi, Kinerethi,
37 Kedesh, Edrei, En-hazor,
Kedeshi, Edrei, na En-Hasori,
38 Yiron, Migdal-el, Horem, Beth-anath, and Beth-shemesh—nineteen towns with their associated villages.
Ironi, Migdal-Eli, Horemu, Beth-Anathi na Beth-Shemeshi. Kulikuwa na miji kumi na tisa na vijiji vyake.
39 This was the allocation—the land, towns, and villages—given to the tribe of Naphtali, by families.
Miji hiyo pamoja na vijiji vyake ndio iliyokuwa urithi wa kabila la Naftali, ukoo kwa ukoo.
40 The seventh lot cast went to the tribe of Dan, by families.
Kura ya saba ikaangukia kabila la Dani, ukoo kwa ukoo.
41 Their allocation included the towns of Zorah, Eshtaol, Ir-shemesh,
Eneo la urithi wao lilijumuisha: Sora, Eshtaoli, Iri-Shemeshi,
42 Shaalabbin, Aijalon, Ithlah,
Shaalabini, Aiyaloni, Ithla,
44 Eltekeh, Gibbethon, Baalath,
Elteke, Gibethoni, Baalathi,
45 Jehud, Bene-berak, Gath-rimmon,
Yehudi, Bene-Beraki, Gath-Rimoni,
46 Me-jarkon, Rakkon, along with the territory opposite Joppa.
Me-Yarkoni na Rakoni, pamoja na eneo linalotazamana na Yafa.
47 However, the tribe of Dan was not able to hold on to their allotted land, so they went and attacked Leshem and captured it. They slaughtered its inhabitants and took possession of the town, settling there. They renamed Leshem as Dan, after their ancestor.
(Lakini Wadani walipata shida kulimiliki eneo lao; kwa hiyo walipanda kuishambulia Leshemu, wakaitwaa, wakawaua watu wake kwa upanga na kuukalia. Walikaa Leshemu na kuuita Dani kufuatana na jina la baba yao.)
48 This was the allocation—the land, towns, and villages—given to the tribe of Dan, by families.
Miji hii na vijiji vyake ndio iliyokuwa urithi wa kabila la Dani, ukoo kwa ukoo.
49 After they finished allotting the land and establishing its borders, the Israelites gave Joshua, son of Nun, an allocation among them.
Walipomaliza kugawanya nchi katika migawo kulingana na sehemu zao zilizowaangukia, Waisraeli wakampa Yoshua mwana wa Nuni urithi katikati yao,
50 Following the Lord's command, they gave him the town he requested—Timnath-serah in the hill country of Ephraim. He rebuilt the town and settled there.
kama vile Bwana alivyokuwa ameamuru. Walimpa mji alioutaka, ambao ni Timnath-Sera ulio katika nchi ya vilima ya Efraimu. Naye akajenga mji, akakaa huko.
51 These were the allocations distributed by Eleazar the priest, Joshua, son of Nun, and the leaders of the Israelite tribes. They were made by casting lots at Shiloh in the presence of the Lord at the entrance of the Tent of Meeting. So they finished dividing up the land.
Haya ndiyo maeneo ambayo kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa koo za kabila za Israeli waliyoyagawanya kwa kura huko Shilo mbele za Bwana penye ingilio la Hema la Kukutania. Hivyo wakamaliza kuigawanya nchi.