< Joshua 18 >
1 The land had been subdued and lay before them. The Israelites gathered together at Shiloh and set up the Tent of Meeting.
Kisha kusanyiko lote la watu wa Israeli walikusanyika pamoja hapo Shilo. Walilijenga hema la kukutania hapo na waliishinda nchi mbele yao.
2 However, seven of the Israelite tribes had not received their land allocations.
Kulikuwa na makabila saba miongoni mwa watu wa Israeli ambayo yalikuwa bado hayajapewa urithi wao.
3 So Joshua asked the Israelites, “How long will you go on being reluctant to go and take possession of the land that the Lord gave your forefathers?
Yoshua aliwaambia watu wa Israeli, “Je mtaacha mpaka lini katika kuingia nchi ambayo Yahweh, Mungu wa baba zenu, amewapeni ninyi?
4 Choose three men from each tribe and I will send them out to explore the land. Then they can write a description regarding the land allocations and bring it to me.
Chagueni ninyi wenyewe watu watatu kutoka katika kila kabila, na nitawatuma. Wataenda na kuipeleleza nchi juu na chini. Wataandika maelezo pamoja na maelekezo kuhusu urithi wao, na kisha watarudi kwangu.
5 They are to divide the land into seven parts, up to the boundary of Judah's land in the south and Joseph's land in the north.
Wataigawanya nchi katika sehemu saba. Yuda itasalia katika eneo lao upande wa kusini, na nyumba ya Yusufu itaendelea katika himaya yao katika upande wa kaskazini.
6 Once you have written the description the land, dividing it in seven parts, you will bring it to me here and I will cast lots for you in the presence of the Lord our God.
Mtaigawanya nchi katika sehemu saba na kisha mtaniletea maelezo hayo hapa kwangu. Nami nitapiga kura kwa ajili yenu hapa mbele za Yahweh Mungu wetu.
7 But the Levites do not receive a share, for their role as priests of the Lord is their allocation. Also, Gad, Reuben, and the half-tribe of Manasseh have already received their allocation that Moses, the servant of the Lord, gave them on the east side of the Jordan.”
Walawi hana sehemu miongoni mwenu, kwa kuwa ukuhani wa Yahweh ni urithi wao. Makabila ya Gadi, Rubeni na nusu ya kabila la Manase wameshapokea urithi wao ng'ambo ya Yordani. Huu ni urithi ambao Musa mtumishi wa Yahweh aliwapa wao.
8 As the men started out on their way to explore the land. Joshua told them, “Go throughout the land and write a description of what you find. Then return to me and I will cast lots for you in the presence of the Lord here in Shiloh.”
Hivyo, watu waliinuka na wakaenda. Yoshua akawaamuru wale walioenda kuandika maelezo ya nchi, akisema, “Pandeni juu na mshuke chini katika nchi na andikeni maelezo kuhusu nchi na kisha mrejee kwangu. Nitapiga kura kwa ajili yenu hapa mbele za Yahweh huko Shilo.
9 So the men went and explored the land and wrote down on a scroll a description of the seven parts, recording the towns in each part. Then they returned to Joshua at the camp in Shiloh
Watu walienda na walitembea juu na chini katika nchi na wakaandika maelezo kuihusu nchi hiyo juu ya gombo kwa miji yake katika sehemu saba, kwa kutaja miji, kila mmoja katika sehemu moja. Kisha wakarudi kwa Yoshua katika kambi huko Shilo.
10 where Joshua cast lots for them in the presence of the Lord. There Joshua divided the land up and allotted the different parts to the remaining Israelite tribes.
Kisha Yoshua akapiga kura kwa ajili yao huko Shilo mbele za Yahweh. Na hapo Yoshua akaigawa nchi kwa watu wa Israeli, kila kabila lilipewa sehemu ya nchi.
11 The first lot cast went to the tribe of Benjamin, by families. The land allotted lay between that of the tribe of Judah and the tribe of Joseph.
Katika kabila la Benyamini, ugawanaji wa nchi ulifanyika kwa kupewa kwa koo zao. Eneo la nchi waliyopewa lilikuwa kati ya wazawa wa Yuda na wazawa wa Yusufu.
12 Their boundary began at the Jordan, and went north of the slope of Jericho, west through the hill country, coming out at the wilderness of Beth-aven.
Katika upande wa kusini, mpaka wao ulianzia katika Yordani. Mpaka ulipanda hata sehemu ya juu kaskazini mwa Yeriko, na kisha ukapita katikati ya nchi ya milima upande wa magharibi. Huko ukafika hadi nyika ya Bethi Aveni.
13 Then the boundary went south to Luz (or Bethel) and on down to Ataroth-addar on the mountain south of Lower Beth-horon.
Kutoka hapo mpaka ulipita upande wa kusini katika mwelekeo wa Luzi (sehemu ile ile inayoitwa Betheli). Kisha mpaka ukashuka chini hata Atarothi Adda, karibu na mlima uliolekea kusini mwa Bethi Horoni.
14 Here the boundary turned south along the western side of the mountain facing Beth-horon, finishing at Kiriath-baal (or Kiriath-jearim), a town of the tribe of Judah. This was the western boundary.
Kisha mpaka ukaendelea upande mwingine: katika upande wa magharibi uligeukia upande wa kusini, ulienda mbele kuukabili mlima ulio ng'ambo ya Bethi Horoni. Mpaka huu ulikomea huko Kiriathi Baali ( ambao ndio Kiriathi Yearimu), mji ambao ulikuwa ni wa kabila la Yuda. Na huu ndio ulikuwa ni mpaka katika upande wa magharibi.
15 The southern boundary began at the edge of Kiriath-jearim. It ran to the spring at Nephtoah,
Katika upande wa kusini, mpaka ulianzia nje tu ya Kiriathi Yearimu. Mpaka uliendelea kutoka Efroni hata chemichemi ya maji ya Neftoa.
16 and then down to the foot of the mountain that faces the valley of Ben-hinnom, at the north end of the valley of Rephaim. Then it went down the valley of Hinnom, along the slope near the Jebusite town, south towards En-rogel.
Kisha mpaka ulishuka chini hadi mpaka wa mlima ambao ulikuwa mkabala ya bonde la Beni Hinomu, ambalo lililokuwa katika upande wa kaskazini mwishoni mwa bonde la Refaimu. Kisha ulishuka chini kuelekea bonde la Hinomu, sehemu ya kusini mwa mteremko wa Wayebusi, na uliendelea kushuka chini hadi Eni Rogeli.
17 From there it headed north to En-shemesh and on to Geliloth, opposite the heights of Adummim, and then on down to the Stone of Bohan (Reuben's son).
Ulizunguka upande wa kaskazini, kuelekea mwelekeo wa Eni Shemeshi, na kutoka hapa ulienda hadi Gelilothi, ambao ulikuwa mkabala na mwinuko wa Adumimu. Kisha ulishuka chini kuelekea Jiwe la Bohani mwana wa Rubeni.
18 Then it went along the ridge opposite the Jordan Valley to the north, and then down into the Jordan Valley itself.
Ulipita kuelekea upande wa kaskazini wa bega la Bethi Araba na chini kuelekea Araba.
19 From there it ran along the north slope of Beth-hoglah, ending at the north bay of the Salt Sea, the southern end of the Jordan. This was the southern boundary.
Mpaka ulipita hadi upande wa bega la kaskazini la Bethi Hogla. Mpaka ulikome katika ghuba ya kaskazini mwa Bahari ya Chumvi, katika upande wa kusini mwishoni mwa Yordani. Huu ulikuwa ni mpaka wa upande wa kusini.
20 The eastern boundary was the Jordan. These were the boundaries around the land of the tribe of Benjamin, by families.
Yordani ulikuwa mpaka wake katika upande wa mashariki. Na huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Benyamini, na walipewa kwa kila ukoo wao, mpaka baada ya mpaka, kwa kuizunguka nchi yote.
21 These were the towns of the tribe of Benjamin, according to families: Jericho, Beth-hoglah, Emek-keziz,
Kwa hiyo sasa miji ya kabila la Benyamini kufuatana na koo zao ilikuwa ni Yeriko,
22 Beth-arabah, Zemaraim, Bethel,
Bethi Hogla, Emeki Kezizi, Bethi Araba, Zemaraimu, Betheli,
24 Kephar-ammoni, Ophni, and Geba—twelve towns with their associated villages.
Kefari Amoni, Ofini, na Geba. Ilikuwa ni miji kumi na miwili, pamoja na vijiji vyake.
25 In addition: Gibeon, Ramah, Beeroth,
Kulikuwa pia na miji ya Gibeoni, Rama, Beerothi,
26 Mizpah, Kephirah, Mozah,
Mizpe, Kefira, Moza,
27 Rekem, Irpeel, Taralah,
Rekemu, Iripeeli, Tarala,
28 Zela, Haeleph, Jebus (or Jerusalem), Gibeah, and Kiriath-jearim—fourteen towns with their associated villages. This was the land allotted to the tribe of Benjamin, by families.
Zela, Haelefu, Yebusi (ambao ndio Yerusalemu), Gibea, na Kiriathi. Kulikuwa na miji kumi na nne, pamoja na vijiji vyake. Huu ulikuwa ni urithi wa Benyamini kufuatana na koo zao.