< Joshua 1 >

1 After the death of Moses, the servant of the Lord, the Lord spoke to Joshua, the son of Nun, who had been Moses' assistant. He told him,
Sasa ilitokea baada ya kufa kwa Musa, mtumishi wa Yahweh, Yahweh alimwambia Yoshua, mwana wa Nuni, msaidizi mkuu wa Musa, kusema,
2 “My servant Moses has died. So go and cross the Jordan, you and all the people, and enter the country I am giving to the Israelites.
“Musa, mtumishi wangu amekufa. Sasa basi inuka, vuka mto huu wa Yordani, wewe na watu hawa wote, kuingia katika nchi ambayo ninawapa - watu waisraeli.
3 As I promised Moses, everywhere you set foot will be land I am giving to you,
Nimewapa ninyi kila sehemu ambapo nyayo za miguu yenu itakanyaga. Nimewapa ninyi, kama nilivyomwahidi Musa.
4 from the desert to Lebanon, and on up to the River Euphrates; all the land of the Hittites, and to the shore of the Mediterranean Sea to the west. This will be your territory.
kuanzia jangwani na Lebanoni, hadi mto mkubwa wa Frati, nchi yote ya Wahiti, na hata Bahari kuu, ambako jua huzama, itakuwa nchi yenu.
5 No one will be able to stand against you while you live. Just as I was with Moses, I will be with you. I will never leave you; I will never abandon you.
Hakuna mtu awaye yote atakayeweza kusimama kinyume chako siku zote za maisha yako. Nitakuwa pamoja nawe kama nilivyokuwa na Musa. Sitakupungukia wala kukuacha.
6 Be strong! Be brave! You will be the people's leader as they occupy the land I promised their ancestors that I would give them.
Uwe hodari na jasiri. Wewe utawafanya watu hawa wairithi nchi ambayo niliwaahidi baba zao kuwa ningewapa.
7 Just be strong and very brave, and be sure to obey all the law that my servant Moses instructed you to follow. Don't turn aside from it, either to the right or to the left, so that you may be successful in everything you do.
Uwe hodari na jasiri sana. uwe makini kutii sheria zote ambazo Musa mtumishi wangu alikuagiza. Usikengeuke upande wa kulia au wa kushoto, ili uweze kufanikiwa kila mahali utakapoenda.
8 Keep on reminding the people about the law. Meditate on it day and night, so you can be sure to do what it requires. Then you will be successful and prosper in what you do.
Siku zote uuongee juu ya kitabu hiki cha sheria. Utakitafakari mchana na usiku ili kwamba uweze kutii yote yaliyoandikwa humo. Kisha utastawi na kufanikiwa.
9 Don't forget what I told you: Be strong! Be brave! Don't be afraid! Don't get discouraged! For the Lord your God is with you wherever you go.”
Je si mimi niliyekuagiza? Uwe hadori na jasiri! Usiogope. Usivunjike moyo. Yahweh Mungu wako yuko pamoja nawe kila uendeko.
10 Then Joshua gave an order to those in charge of the people:
Kisha Yoshua akawaagiza viongozi wa watu,
11 “Go through the whole camp and tell the people, ‘Get everything ready, because in three days time we will cross the Jordan, to go and take the land God is giving to you to possess.’”
“Nendeni katika kambi na waagizeni watu, 'andaeni chakula kwa ajili yenu. Baada ya siku tatu mtavuka mto huu wa Yordani na kuingia ndani na kuimiliki nchi ambayo Yahweh Mungu wenu awapeni ninyi ili kuimiliki.””
12 But to the tribes of Reuben and Gad, and half of the tribe of Manasseh, Joshua said,
Yoshua akawaambia Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase,
13 “Remember what Moses, the servant of the Lord, ordered you to do: ‘The Lord your God is giving you rest, and will give you this land.’
“Kumbukeni maneno ambayo Musa, mtumishi wa Yahweh, aliwaaagiza aliposema, 'Yahweh Mungu wenu awapeni ninyi pumziko, naye awapeni ninyi nchi hii.'
14 Your wives and children, and your livestock will remain here in the land that Moses allotted you on the east side of the Jordan. But all your armed men, ready for battle, will cross over ahead of your brothers to help them,
Wake zenu, na watoto wenu na mifugo yenu itakaa katika nchi ambayo Musa aliwapa ninyi ng'ambo ya Yordani. Lakini watu wenu wa vita wataenda pamoja na ndugu zao na kuwasaidia.
15 until the Lord lets them rest, as he has let you rest, and they too have taken possession of the land that the Lord is giving to you. Then you can return and occupy your own land which Moses allotted to you on the east side of the Jordan.”
Mpaka hapo Yahweh atakapowapa ndugu zenu pumziko kama alivyowapa ninyi. Na wao pia watamiliki nchi ambayo Yahweh Mungu wenu awapeni ninyi. Kisha mtarudi katika nchi yenu na kuimiliki, nchi ambayo Musa mtumishi wa Yahweh aliwapa ninyi ng'ambo ya Yordani, mahali pa mapambazuko ya jua.”
16 They said to Joshua, “We will do everything you have ordered us to do, and we will go wherever you send us.
Nao wakamjibu Yoshua, na kusema, “Mambo yote uliyotuagiza tutayafanya, na kila mahali utakapotutuma tutaenda.
17 We will obey you just as we obeyed Moses in everything. May the Lord God be with you as he was with Moses.
Tutakutii kama tulivyomtii Musa. Yahweh Mungu wako na awe pamoja nawe tu kama aliyokuwa pamoja na Musa.
18 Anyone who rebels against what you say and doesn't follow your orders, who doesn't obey everything you command, will be put to death. So be strong! Be brave!”
Yeyote anayeasi maagizo yako na kutotii maneno yako atauawa. Uwe hodari na jasiri tu.

< Joshua 1 >