< John 7 >
1 After this, Jesus spent his time going from place to place in Galilee. He did not want to do so in Judea because the Jews were out to kill him.
Baada ya hayo, Yesu alikuwa akitembea katika Galilaya. Hakutaka kutembea mkoani Yudea kwa sababu viongozi wa Wayahudi walikuwa wanataka kumwua.
2 But as it was almost time for the Jewish festival of the Tabernacles,
Sikukuu ya Vibanda ya Wayahudi ilikuwa imekaribia.
3 his brothers told him, “You ought to leave and go to Judea so your followers will be able to see what miracles you can do.
Basi ndugu zake wakamwambia, “Ondoka hapa uende Yudea ili wanafunzi wako wazione kazi unazozifanya.
4 No one who wants to be famous keeps what they do hidden. If you can do such miracles, then show yourself to the world!”
Mtu hafanyi mambo kwa siri kama anataka kujulikana kwa watu. Maadam unafanya mambo haya, basi, jidhihirishe kwa ulimwengu.”
5 For even his own brothers really didn't believe in him.
(Hata ndugu zake hawakumwamini!)
6 Jesus told them, “This is not my time to go, not yet; but you can go whenever you want, for any time's the right time for you.
Basi, Yesu akawaambia, “Wakati wangu ufaao haujafika bado. Lakini kwenu ninyi kila wakati unafaa.
7 The world has no reason to hate you, but it does hate me, because I make it clear that its ways are evil.
Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi, lakini mimi wanichukia kwa sababu mimi nauambia wazi kwamba matendo yake ni maovu.
8 You go on to the festival. I'm not going to this festival because this is not the right time for me, not yet.”
Ninyi nendeni kwenye sikukuu hiyo. Mimi siendi kwenye sikukuu hiyo, maana saa yangu ifaayo haijafika.”
9 After saying this he stayed behind in Galilee.
Alisema hayo kisha akabaki huko Galilaya.
10 After his brothers left to go to the festival, Jesus also went, but not openly—he stayed out of sight.
Baada ya ndugu zake kwenda kwenye sikukuu, Yesu naye alikwenda, lakini hakuenda kwa hadhara bali kwa siri.
11 Now at the festival the Jewish leaders were searching for him and kept on asking, “Where is he?”
Viongozi wa Wayahudi walikuwa wanamtafuta kwenye sikukuu hiyo; Wakauliza: “Yuko wapi?”
12 Many people in the crowds were complaining about him. Some said, “He's a good man,” while others argued, “No! He deceives people.”
Kulikuwa na minong'ono mingi katika umati wa watu. Baadhi yao walisema, “Ni mtu mwema.” Wengine walisema, “La! Anawapotosha watu.”
13 But no one dared to speak openly about him because they were afraid of what the Jewish leaders would do to them.
Hata hivyo hakuna mtu aliyethubutu kusema, habari zake hadharani kwa kuwaogopa viongozi wa Wayahudi.
14 When the festival was halfway through Jesus went to the Temple and began to teach.
Sikukuu hiyo ilipofikia katikati, Yesu naye alikwenda Hekaluni, akaanza kufundisha.
15 The Jewish leaders were very surprised, and asked, “How does this man have so much learning when he hasn't been educated?”
Basi, Wayahudi wakashangaa na kusema “Mtu huyu amepataje elimu naye hakusoma shuleni?”
16 Jesus answered, “My teaching is not from me but from the one who sent me.
Hapo Yesu akawajibu, “Mafundisho ninayofundisha si yangu, bali ni yake yeye aliyenituma.
17 Anyone who chooses to follow what God wants will know if my teaching comes from God or if I'm only speaking for myself.
Mtu anayependa kufanya yale anayotaka Mungu, atajua kama mafundisho yangu yametoka kwa Mungu, au mimi najisemea tu mwenyewe.
18 Those who speak for themselves want to glorify themselves, but someone who glorifies the one who sent him is truthful and not deceitful.
Yeye anayejisemea tu mwenyewe anatafuta sifa yake mwenyewe; lakini anayetafuta sifa ya yule aliyemtuma, huyo ni mwaminifu, na ndani yake hamna uovu wowote.
19 Moses gave you the law, didn't he? Yet none of you keeps the law! Why are you trying to kill me?”
Je, Mose hakuwapeni Sheria? Hata hivyo, hakuna hata mmoja wenu anayeishika Sheria. Kwa nini mnataka kuniua?”
20 “You're demon-possessed!” the crowd replied. “No one's trying to kill you!”
Hapo watu wakamjibu, “Una wazimu wewe! Nani anataka kukuua?”
21 “I did one miracle and you're all shocked by it,” Jesus replied.
Yesu akawajibu, “Kuna jambo moja nililofanya, nanyi mnalistaajabia.
22 “However, because Moses told you to circumcise—not that it really came from Moses, but from your forefathers before him—you perform circumcision on the Sabbath.
Mose aliwapeni ile desturi ya kutahiri. (Si kwamba desturi hiyo ilitoka kwa Mose, bali ilitoka kwa mababu). Sasa ninyi humtahiri mtu hata siku ya Sabato.
23 If you circumcise on the Sabbath to make sure that the law of Moses isn't broken, why are you angry with me for healing someone on the Sabbath?
Ikiwa basi, mtu hutahiriwa hata siku ya Sabato kusudi Sheria ya Mose isivunjwe, mbona mnanikasirikia kwa sababu nimemfanya mtu kuwa mzima kabisa siku ya Sabato?
24 Don't judge by appearances; decide what is right!”
Msihukumu mambo kwa nje tu; toeni hukumu ya haki.”
25 Then some of those from Jerusalem began wondering, “Isn't this the one they're trying to kill?
Baadhi ya watu wa Yerusalemu walisema, “Je, yule mtu wanayemtafuta wamuue si huyu?
26 But see how openly he's speaking, and they're saying nothing to him. Do you think the authorities believe he's the Messiah?
Tazameni sasa! Anawaonya hadharani, wala hakuna mtu anayemwambia hata neno. Je, yawezekana kuwa viongozi wametambua kweli kwamba huyu ndiye Kristo?
27 But that's not possible because we know where he comes from. When the Messiah comes, nobody will know where he's from.”
Kristo atakapokuja hakuna mtu atakayejua mahali alikotoka, lakini sisi tunajua alikotoka mtu huyu!”
28 While he was teaching in the Temple, Jesus called out in a loud voice, “So you think you know me and where I'm from? However, I did not come for my own sake. The one who sent me is true. You don't know him,
Basi, Yesu alipokuwa anafundisha Hekaluni alipaaza sauti na kusema, “Ati mnanijua; hata nilikotoka mnakujua! Hata hivyo, sikuja kwa mamlaka yangu mwenyewe; ila yeye aliyenituma mimi ni wa kweli, nanyi hamumjui.
29 but I know him, for I come from him, and he sent me.”
Lakini mimi namjua kwa sababu nimetoka kwake, naye ndiye aliyenituma.”
30 So they tried to arrest him, but no one laid a hand on him because his time had not yet come.
Basi, watu wakataka kumtia nguvuni, lakini hakuna mtu aliyethubutu kumkamata kwa sababu saa yake ilikuwa haijafika bado.
31 However, many of the crowd did put their trust in him. “When the Messiah appears, will he do more miraculous signs than this man has done?” they said.
Wengi katika ule umati wa watu walimwamini, wakasema, “Je, Kristo akija atafanya ishara kubwa zaidi kuliko alizozifanya huyu?”
32 When the Pharisees heard the crowd whispering this about him, they and the chief priests sent guards to arrest Jesus.
Mafarisayo waliwasikia watu wakinong'ona maneno hayo juu ya Yesu. Basi, wao pamoja na makuhani wakuu wakawatuma walinzi wamtie nguvuni.
33 Then Jesus told the people, “I'll be with you just a little longer, but then I'll return to the one who sent me.
Yesu akasema, “Bado niko nanyi kwa muda mfupi, kisha nitamwendea yule aliyenituma.
34 You'll search for me but you won't find me; and you can't come where I'm going.”
Mtanitafuta lakini hamtaniona, maana pale nitakapokuwa ninyi hamwezi kufika.”
35 The Jews said to each other, “Where could he be going that we couldn't find him? Is he planning to go to those scattered among the foreigners, and teach the foreigners?
Viongozi wa Wayahudi wakasema wao kwa wao, “Mtu huyu atakwenda wapi ambapo hatutaweza kumpata? Atakwenda kwa Wayahudi waliotawanyika kati ya Wagiriki, na kuwafundisha Wagiriki?
36 What does he mean by saying, ‘You'll search for me but you won't find me; and you can't come where I'm going’?”
Ana maana gani anaposema: Mtanitafuta lakini hamtanipata, na mahali nitakapokuwa ninyi hamwezi kufika?”
37 On the last and most important day of the festival, Jesus stood up and shouted out in a loud voice, “If you're thirsty, come to me and drink.
Siku ya mwisho ya sikukuu hiyo ilikuwa siku maalum. Yesu alisimama, akasema kwa sauti kubwa, “Aliye na kiu na aje kwangu anywe.
38 If you trust in me, you will have streams of life-giving water flowing out from within you, as Scripture says.”
Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: Anayeniamini mimi, mito ya maji yenye uzima itatiririka kutoka moyoni mwake!”
39 He was referring to the Spirit that those who trusted in him would later receive. The Spirit hadn't been given yet because Jesus hadn't yet been glorified.
(Alisema hayo kumhusu Roho ambaye wale waliomwamini yeye watampokea. Wakati huo Roho alikuwa hajafika kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa bado.)
40 When they heard these words, some of the people said, “This man is definitely the Prophet!”
Baadhi ya watu katika ule umati walisikia maneno hayo, wakasema, “Kweli mtu huyu ndiye yule nabii!”
41 Others said, “He is the Messiah!” Still others said, “How can the Messiah come from Galilee?
Wengine wakasema, “Huyu ndiye Kristo!” Lakini wengine walisema, “Je, yawezekana Kristo akatoka Galilaya?
42 Doesn't Scripture say that the Messiah comes from David's lineage, and from David's home town of Bethlehem?”
Maandiko Matakatifu yasemaje? Yanasema: Kristo atatoka katika ukoo wa Daudi, na atazaliwa Bethlehemu, mji wa Daudi!”
43 So the crowd had a strong difference of opinion about him.
Basi, kukatokea mafarakano juu yake katika ule umati wa watu.
44 Some wanted to arrest him, but nobody laid a hand on him.
Baadhi ya watu walitaka kumtia nguvuni lakini hakuna aliyejaribu kumkamata.
45 Then the guards returned to the chief priests and the Pharisees who asked them, “Why didn't you bring him in?”
Kisha wale walinzi wakarudi kwa makuhani wakuu na Mafarisayo; nao wakawauliza, “Kwa nini hamkumleta?”
46 “Nobody ever spoke like this man does,” the guards replied.
Walinzi wakawajibu, “Hakuna mtu aliyepata kamwe kusema kama asemavyo mtu huyu!”
47 “Have you been fooled too?” the Pharisees asked them.
Mafarisayo wakawauliza, “Je, nanyi pia mmedanganyika?
48 “Has a single one of the rulers or Pharisees believed in him? No!
Je, mmekwisha mwona hata mmoja wa viongozi wa watu, au mmoja wa Mafarisayo aliyemwamini?
49 But this crowd that knows nothing about teachings of the law—they're damned anyway!”
Lakini umati huu haujui Sheria ya Mose; umelaaniwa!”
50 Nicodemus, who had previously gone to meet Jesus, was one of them and asked them,
Mmoja wao alikuwa Nikodemo ambaye hapo awali alikuwa amemwendea Yesu. Basi, yeye akawaambia,
51 “Does our law condemn a man without a hearing and without finding out what he actually did?”
“Je, Sheria yetu humhukumu mtu kabla ya kumsikia kwanza na kujua anafanya nini?”
52 “So you're a Galilean as well, are you?” they replied. “Check the Scriptures and you'll discover that no prophet comes from Galilee!”
Nao wakamjibu, “Je, wewe pia umetoka Galilaya? Haya, kayachunguze Maandiko Matakatifu nawe utaona kwamba Galilaya hakutoki kamwe nabii!”
53 Then they all went home,
Basi, wote wakaondoka, kila mtu akaenda zake;