< John 16 >

1 I've told you this so you won't give up your trust in me.
Nimewaambia mambo haya ili msiweze kukwazwa.
2 They will expel you from the synagogues—in fact the time is coming when those who kill you will think they are doing God a service.
Watawatoa nje ya masinagogi; hakika saa inakuja ambayo kila atakayewaua atafikiri kuwa anafanya kazi njema kwa ajili ya Mungu.
3 They'll do this because they have never known the Father or me. I've told you this so that when these things happen, you'll remember what I told you.
Watawatendea mambo haya kwa sababu hawamfahamu Baba wala hawanifahamu mimi.
4 I didn't need to tell you this right at the beginning because I was going to be with you.
Nimewaambia mambo haya ili kwamba wakati ukifika wa haya kutokea, mnaweza kuyakumbuka na jinsi nilivyowaambia muweze wao. Sikuwaambia kuhusu mambo haya tangu mwanzo kwa sababu nilikuwa pamoja nanyi.
5 But now I'm going to the one who sent me, and yet not one of you is asking me, ‘Where are you going?’
Japokuwa, sasa naenda kwa yule aliyenituma; lakini hakuna kati yenu anayeniuliza, “Unaenda wapi?”
6 Of course, now that I've told you, you're full of grief.
Kwa sababu nimesema maneno haya kwenu, huzuni imejaa mioyoni mwenu.
7 But I'm telling you the truth: it's better for you that I go away, for if I don't the Comforter won't come to you. If I go away, I will send him to you.
Hata hivyo, nawaambia ukweli: ni vyema kwenu nikiondoka; kwa maana nisipoondoka, mfariji hatakuja kwen; lakini nikienda ntamtuma kwenu.
8 When he comes, he will convince those in the world that they have wrong ideas regarding sin, about what is right, and about judgment:
Akija, huyo mfariji ataubitisha ulimwengu kuhusiana na dhambi, kuhusiana na haki na kuhusiana na hukumu.
9 Sin, for they don't trust in me.
Kuhusiana na dhambi, kwa sababu hawakuniamini mimi,
10 What is right, for I'm going to the Father and you won't see me any longer.
kuhusiana na haki, kwa sababu naenda kwa baba, na hamtaniona tena;
11 Judgment, for the ruler of this world has been condemned.
na kuhusiana na hukumu kwa sababu mkuu wa ulimwengu huu amehukumiwa.
12 There's much more I want to explain to you, but you couldn't stand it now.
Ninayo mengi ya kuwaambia, lakini hamtayaelewa sasa.
13 However, when the Spirit of truth comes, he will teach you the whole truth. He doesn't speak for himself, but he only says what he hears, and he will tell you what's going to happen.
Lakini, yeye, Roho wa kweli, akija, atawaongoza katika kweli yote; kwa kuwa hataongea kwa ajili yake mwenyewe; lakini yoyote atakayoyasikia, atayasema mambo hayo; na atayadhihirisha kwenu mambo yatakayokuja.
14 He brings me glory for he teaches you whatever he receives from me.
Yeye atanitukuza mimi, kwa sababu atayachukua mambo yangu na atayatangaza kwenu.
15 All that belongs to the Father is mine. This is why I said that the Spirit teaches you whatever he receives from me.
Vitu vyote alivyonavyo Baba ni vyangu; kwa hiyo, nimesema kwamba Roho atachukua mambo yangu na atayadhihirisha kwenu.
16 In a little while you won't see me anymore, but then a little while after that you will see me.”
Bado muda mfupi, hamtaniona tena; na baada ya muda mfupi tena, mtaniona.”
17 Some of his disciples said to one another, “What does he mean, ‘In a little while you won't see me, but a little while after that you will see me’? and ‘For I'm going to the Father’?”
Baadhi ya wanafunzi wake wakaambizana, “Ni nini anachotuambia, “muda mfupi, na hamtaniona tena,' na, kisha, mda mfupi mtaniona,' na, 'kwa sababu naenda kwa Baba?”
18 They were asking, “What does he mean by ‘in a little while’? We don't know what he's talking about.”
Kwa hiyo wakasema, “Ni kitu gani anachosema, 'Bado mda mfupi'? Hatujui asemavyo.”
19 Jesus realized that they wanted to ask him about this. So he asked them, “Are you wondering about my comment, ‘In a little while you won't see me, but a little while after that you will see me’?
Yesu aliona kuwa walitamani kumuuliza, naye akawaambia, “Mnajiuliza wenyewe kuhusu hili, nilivyosema, 'Bado muda mfupi, hamtaniona tena; na baada ya muda mfupi mtaniona'?
20 I tell you the truth, you will weep and mourn, but the world will rejoice. You will grieve, but your grief will turn into joy.
Amin, amin, nawaambia, mtalia na kuomboleza, lakini ulimwengu utashangilia, mtakuwa na huzuni lakini huzuni yenu itageuka kuwa furaha.
21 A woman in labor suffers pain because her time has come, but once the baby is born, she forgets the agony because of the joy that a child has been brought into the world.
Mwanamke anakuwa na huzuni wakati anapokuwa na uchungu kwa sababu wakati wa kujifungua umefika; lakini anapojifungua mtoto, hakumbuki tena maumivu kwa sababu ya furaha yake kwamba mtoto amezaliwa duniani.
22 Yes, you're grieving now, but I will see you again; and you will rejoice, and no one can take away your joy.
Ninyi pia mna huzuni sasa, lakini nitawaona tena; na mioyo yenu itafurahi na hakuna atakayeweza kuiondoa furaha yenu.
23 When that time comes you won't need to ask me for anything. I tell you the truth, the Father will give you whatever you ask in my name.
Siku hiyo hamtaniuliza maswali. Amin, Amin, nawaambia, Mkiomba lolote kwa Baba, atawapa kwa jina langu.
24 Until now you haven't asked for anything in my name, so ask and you shall receive, and your happiness will be complete.
Mpaka sasa hamjaomba lolote kwa jina langu; ombeni, nanyi mtapokea ili kwamba furaha yenu ikamilike.
25 I've been talking to you using picture language. But soon I won't use such picture language any more when I speak to you. Instead I'll explain the Father to you very plainly.
Nimezungumza na ninyi kwa lugha isiyoeleweka, lakini saa inakuja ambapo sitazungumza kwa lugha isiyoeleweka lakini badala yake nitawaambia waziwazi kuhusu Baba.
26 At that time you will ask in my name. I'm not saying to you that I will plead with the Father on your behalf,
Siku hiyo mtaomba kwa jina langu, na siwaambii kwamba nitaomba kwa Baba kwa ajili yenu;
27 for the Father himself loves you—because you love me and believe that I came from God.
Kwa kuwa Baba mwenyewe anawapenda kwa sababu mmenipenda mimi na kwa sababu mmeniamini kuwa nimetoka kwa Baba.
28 I left the Father and came into the world; now I leave the world and return to my Father.”
Nilitoka kwa Baba na nimekuja ulimwenguni; tena, naondoka ulimwenguni na ninaenda kwa Baba”.
29 Then the disciples said, “Now you're talking very plainly and not using picture language.
Wanafunzi wake wakamwambia, “Unaona, sasa unaongea wazi wazi na hautumii mafumbo.
30 Now we're certain that you know everything, and that in order to know what questions people are thinking you don't need to ask them. This convinces us that you came from God.”
Sasa, tunajua kwamba unajua mambo yote, na hauhitaji mtu yoyote akuulize maswali. Kwa sababu hii tunaamini kuwa unatoka kwa Mungu.
31 “Are you really convinced now?” Jesus asked.
Yesu akawajibu, “Sasa mmeamini?”
32 “The time is coming—in fact it's just about to happen—when you will be scattered, each of you to your own homes, leaving me all alone. But I'm not really alone, for the Father is with me.
Tazama, saa inakuja, ndiyo na hakika imefika, ambapo mtatawanyika kila mmoja na kwa wa kwao mtaniacha mwenyewe. Lakini siko peke yangu kwa sababu Baba yupo nami.
33 I've told you all this so that you may have peace because you are one with me. You will suffer in this world, but be brave—I have defeated the world!”
Nawaambia mambo haya ili kwamba ndani yangu muwe na amani. Duniani mna matatizo, lakini jipeni moyo, nimeushinda ulimwengu.

< John 16 >