< Job 38 >
1 Then the Lord answered Job out of the whirlwind,
Ndipo Yahweh alimwita Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kumwambia,
2 “Who is this who questions my wisdom by talking so ignorantly?
“Huyu ni nani aletaye giza katika mipango kwa njia ya maneno bila maarifa?
3 Prepare yourself, be strong, for I am going to question you, and you must answer me.
Basi sasa jifunge kiunoni mwako kama mwanaume kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
4 Where were you when I laid the foundation of the earth? Tell me, if you have such knowledge!
Wewe ulikuwa wapi wakati nilipoitandaza misingi ya dunia? Niambie, kama unao ufahamu zaidi.
5 Who decided its dimensions? Don't you know? Who stretched out a measuring line?
Je ni nani aliyeamuru vipimo vyake? Niambie, kama unajua, ni nani alivinyosha vipimo juu yake?
6 What do its foundations rest upon? Who laid its cornerstone,
Misingi yake ilitandazwa juu ya nini? Ni nani aliyeliweka jiwe lake la pembeni
7 when the stars of the morning sang together and all the angels shouted for joy.
wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja na wana wote wa Mungu walipopiga kelele kwa furaha?
8 Who laid down the boundaries of the sea when it was born?
Ni nani huifunga bahari kwa milango wakati inapofurika, kana kwamba inatoka katika tumbo,
9 Who clothed it with clouds, and wrapped it in a blanket of deep darkness?
wakati nilipoyafanya mawingu kuwa ni mavazi yake, na giza nene kuwa mkanda wake wa kujifungia?
10 I set its limits, marking its borders.
Hapo ilikuwa wakati nilipoweka bahari mpaka wangu, na nilipoweka makomeo yake na milango,
11 I said, ‘You may come here, but no farther. Here is where your proud waves stop.’
na wakati nilipoiambia, 'Unaweza kuja hapa kutoka mbali, lakini si zaidi; na hapa ndipo nitauweka mpaka kwa fahari ya mawimbi yako.'
12 During your lifetime, have you ever ordered the morning to begin?
Je tangu mwanzo wa siku zako, ulishawahi kuigiza asubuhi ianze, na kuyafanya mapambazuko yajue sehemu yake katika mpangilio wa vitu,
13 Have you ever told the dawn where to appear that it might take hold of the corners of the earth and shake the wicked out?
ili kwamba ishikilie sehemu za dunia ili watu waovu watikiswe mbali nayo.
14 The earth is changed like clay under a seal; its features stand out like a crumpled garment.
Dunia imebadilishwa katika mwonekano kama udongo unavyobadilika chini ya muhuri; vitu vyote husimama juu yake dhahiri kama cha kibindo cha nguo.
15 The ‘light’ of the wicked is taken away from them; their acts of violence are stopped.
'Mwanga' wao umeondolewa kutoka kwa watu waovu; na mkono wao ulioinuliwa umevunjwa.
16 Have you entered the sources of the sea? Have you explored their hidden depths?
Je umeshaenda kwenye vyanzo vya maji ya bahari? Je umeshatembea sehemu za chini kabisa za kilindi?
17 Have you been shown where the gates of death are? Have you seen the gates of utter darkness?
Je malango ya mauti yamefunuliwa kwako? Je umeshaona malango ya uvuli wa mauti?
18 Do you know how far the earth extends? Tell me if you know all this!
Je umeifahamu dunia katika upana wake? Niambie kama unayajua yote hayo.
19 In which direction does light live? Where does darkness dwell?
Je iko wapi njia ya sehemu ya kupumzikia kwa mwanga, na kama ilivyo kwa giza, iko wapi sehemu yake?
20 Can you take them home? Do you know the way to where they live?
Je unaweza kuuongoza mwanga na giza katika sehemu zake za kazi? Waweza kuitambua njia ya kurudi katika nyumba zao?
21 Of course you know, because you were already born then! You've lived so long!
Bila shaka unajua, kwa kuwa ulizaliwa wakati huo; hesabu ya siku zako ni kubwa sana!
22 Have you been to where the snow is kept? Have you seen where the hail is held?
Je ulishaingia katika ghala ya barafu, au umeshaiona ghala ya mawe ya mvua,
23 I have stored them up for the time of trouble, for the day of war and battle.
vitu hivi nimeviweka kwa ajili ya siku za mateso, kwa siku za mapigano na vita?
24 Do you know the way to where light comes from, or to where the east wind blows over the earth?
Je iko wapi njia ya mshindo wa mwanga hutokea au je upepo husambazwa kutoka mashariki juu ya dunia?
25 Who cuts a channel for the rain to flow? Who creates a path for the thunderbolt?
Ni nani aliyezitengeneza mifereji ya gharika ya mvua, au ni nani aliyezifanya njia za milipuko ya radi,
26 Who brings rain to an uninhabited land, to a desert where nobody lives,
na kuifanya mvua inyeshe juu ya nchi ambazo hakuna mtu aishiye ndani yake, na juu ya jangwa, ambayo ndani yake hakuna mtu yeyote,
27 to water a parched wasteland to make the green grass grow?
kwa kusudi la kutimiza mahitaji ya mikoa iliyo kame na yenye ukiwa, na kuyastawisha majani mororo?
28 Does the rain have a father? Who was the father of the dewdrops?
Je kuna baba wa mvua? Ni nani aliyeyafanya matone ya umande?
29 Who was the mother of ice? Does the frost of the air have a mother?
Je barafu ilitoka katika tumbo la nani? Na ni nani aliyeizaa theluji nyeupe katika anga?
30 Water turns into rock-hard ice; its surface freezes solid.
Maji hujificha menyewe na kuwa kama jiwe; sehemu za juu za vilindi huwa kama barafu.
31 Can you tie together the stars of the Pleiades? Can you loosen the belt of the Orion constellation?
Je unaweza kuzifunga minyororo ya Kilimia, au kuvifungua vifundo vya Orioni?
32 Can you guide the stars of Mazzaroth at the right time? Can you direct the Great Bear constellation and its other stars?
Je unaweza kuziongoza nyota kutokea katika nyakati zake? Je waweza kuongoza dubu pamoja na watoto wake?
33 Do you know the laws of the heavens? Can you apply them to the earth?
Je unazijua sheria za anga? Wewe uliweza kuanzisha sheria za anga juu ya dunia?
34 Can you shout to the clouds and command them to pour rain down on you?
Je waweza kupaza sauti yako hadi mawinguni, ili kwamba maji mengi ya mvua yakufunike?
35 Can you send out bolts of lightning and direct them, so that they can answer you saying, ‘Here we are’?
Je waweza kuagiza miali ya mwanga ili itokee, na kukwambia, 'Sisi tupo hapa'?
36 Who has placed wisdom inside people? Who has given understanding to the mind?
Ni nani ameweka hekima katika mawingu au ni nani ameweka ufahamu kwa ukungu?
37 Who is clever enough to count the clouds? Who can turn heaven's water jars on their sides
Nani anaweza kuyahesabu mawingu kwa maarifa yake? Na ni nani awezaye kuvimwaga viriba vya anga
38 when the dust has baked into a solid mass?
wakati mavumbi yanapoungana kuwa kitu kigumu na mabonge ya dunia yanaposhikama kwa pamoja?
39 Can you hunt prey for the lion? Can you feed the lion cubs
Je waweza kuwinda mawindo kwa ajili ya simba jike au kutosheleza hamu ya watoto wadogo wa simba
40 as they crouch down in their dens and lie in wait in the bushes?
wakati wanapokwaruza kwaruza katika pango lao na kukaa katika kificho ili kulala katika hali ya kuvizia?
41 Who provides food for the raven when its young cry out to God, weak from starvation?
Ni nani aletaye mawindo kwa ajili ya kunguru wakati ambapo watoto wao wanapomlilia Mungu na kutangatanga kwa kukosa chakula?