< Job 38 >

1 Then the Lord answered Job out of the whirlwind,
Kisha Bwana akamjibu Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli. Akasema:
2 “Who is this who questions my wisdom by talking so ignorantly?
“Nani huyu atiaye mashauri yangu giza kwa maneno yasiyo na maarifa?
3 Prepare yourself, be strong, for I am going to question you, and you must answer me.
Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza swali, nawe unijibu.
4 Where were you when I laid the foundation of the earth? Tell me, if you have such knowledge!
“Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia? Niambie, kama unafahamu.
5 Who decided its dimensions? Don't you know? Who stretched out a measuring line?
Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake? Hakika wewe unajua! Ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?
6 What do its foundations rest upon? Who laid its cornerstone,
Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini, au ni nani aliyeweka jiwe la pembeni,
7 when the stars of the morning sang together and all the angels shouted for joy.
wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, na malaika wote walipokuwa wakipiga kelele kwa furaha?
8 Who laid down the boundaries of the sea when it was born?
“Ni nani aliyeifungia bahari milango ilipopasuka kutoka tumbo,
9 Who clothed it with clouds, and wrapped it in a blanket of deep darkness?
nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake, na kuyafungia katika giza nene,
10 I set its limits, marking its borders.
nilipoamuru mipaka yake, na kuiweka milango yake na makomeo mahali pake,
11 I said, ‘You may come here, but no farther. Here is where your proud waves stop.’
niliposema, ‘Unaweza kufika mpaka hapa wala si zaidi; hapa ndipo mawimbi yako yenye kiburi yatakapokomea’?
12 During your lifetime, have you ever ordered the morning to begin?
“Umepata kuiamrisha asubuhi ipambazuke, au kuyaonyesha mapambazuko mahali pake,
13 Have you ever told the dawn where to appear that it might take hold of the corners of the earth and shake the wicked out?
yapate kushika miisho ya dunia, na kuwakungʼuta waovu waliomo?
14 The earth is changed like clay under a seal; its features stand out like a crumpled garment.
Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi chini ya lakiri; sura yake hukaa kama ile ya vazi.
15 The ‘light’ of the wicked is taken away from them; their acts of violence are stopped.
Waovu huzuiliwa nuru yao, nao mkono wao ulioinuliwa huvunjwa.
16 Have you entered the sources of the sea? Have you explored their hidden depths?
“Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari? Au kutembea mahali pa ndani pa vilindi?
17 Have you been shown where the gates of death are? Have you seen the gates of utter darkness?
Umewahi kuonyeshwa malango ya mauti? Umewahi kuiona milango ya uvuli wa mauti?
18 Do you know how far the earth extends? Tell me if you know all this!
Je, wewe unafahamu ukubwa wa dunia? Niambie kama unajua haya yote.
19 In which direction does light live? Where does darkness dwell?
“Njia ya kufika kwenye makao ya nuru ni ipi? Nako maskani mwa giza ni wapi?
20 Can you take them home? Do you know the way to where they live?
Je, unaweza kuvirudisha kwenye makao yake? Unajua njia za kufika maskani mwake?
21 Of course you know, because you were already born then! You've lived so long!
Hakika unajua, kwa kuwa ulikuwa umeshazaliwa! Kwani umeishi miaka mingi!
22 Have you been to where the snow is kept? Have you seen where the hail is held?
“Je, umeshawahi kuingia katika ghala za theluji, au kuona ghala za mvua ya mawe,
23 I have stored them up for the time of trouble, for the day of war and battle.
ambazo nimeziweka akiba kwa ajili ya wakati wa taabu, na kwa ajili ya wakati wa vita na mapigano?
24 Do you know the way to where light comes from, or to where the east wind blows over the earth?
Ni ipi njia iendayo mahali umeme wa radi unapotawanyiwa, au mahali upepo wa mashariki unaposambaziwa juu ya dunia?
25 Who cuts a channel for the rain to flow? Who creates a path for the thunderbolt?
Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi na njia ya umeme wa radi,
26 Who brings rain to an uninhabited land, to a desert where nobody lives,
ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu, jangwa lisilo na yeyote ndani yake,
27 to water a parched wasteland to make the green grass grow?
ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa, na majani yaanze kumea ndani yake?
28 Does the rain have a father? Who was the father of the dewdrops?
Je, mvua ina baba? Ni nani baba azaaye matone ya umande?
29 Who was the mother of ice? Does the frost of the air have a mother?
Barafu inatoka tumbo la nani? Ni nani azaaye ukungu kutoka mbinguni,
30 Water turns into rock-hard ice; its surface freezes solid.
wakati maji yawapo magumu kama jiwe, wakati uso wa vilindi vya maji unapoganda?
31 Can you tie together the stars of the Pleiades? Can you loosen the belt of the Orion constellation?
“Je, waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia? Waweza kulegeza kamba za Orioni?
32 Can you guide the stars of Mazzaroth at the right time? Can you direct the Great Bear constellation and its other stars?
Waweza kuyaongoza makundi ya nyota kwa majira yake, au kuongoza Dubu na watoto wake?
33 Do you know the laws of the heavens? Can you apply them to the earth?
Je, unajua sheria zinazotawala mbingu? Waweza kuweka utawala wa Mungu duniani?
34 Can you shout to the clouds and command them to pour rain down on you?
“Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni, na kujifunika mwenyewe na gharika ya maji?
35 Can you send out bolts of lightning and direct them, so that they can answer you saying, ‘Here we are’?
Je, wewe hutuma umeme wa radi kwenye njia zake? Je, hutoa taarifa kwako kukuambia, ‘Sisi tuko hapa’?
36 Who has placed wisdom inside people? Who has given understanding to the mind?
Ni nani aliyeujalia moyo hekima au kuzipa akili ufahamu?
37 Who is clever enough to count the clouds? Who can turn heaven's water jars on their sides
Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu? Ni nani awezaye kuinamisha magudulia ya mbinguni
38 when the dust has baked into a solid mass?
wakati mavumbi yawapo magumu, na mabonge ya udongo kushikamana pamoja?
39 Can you hunt prey for the lion? Can you feed the lion cubs
“Je, utamwindia simba jike mawindo, na kuwashibisha simba wenye njaa
40 as they crouch down in their dens and lie in wait in the bushes?
wakati wao wamejikunyata mapangoni mwao, au wakivizia kichakani?
41 Who provides food for the raven when its young cry out to God, weak from starvation?
Ni nani ampaye kunguru chakula wakati makinda yake yanamlilia Mungu, yakizungukazunguka kwa ajili ya kukosa chakula?

< Job 38 >