< Job 3 >
1 After this Job began speaking, cursing the day of his birth.
Baada ya hayo, Ayubu akafunua kinywa chake na kuilani siku aliyozaliwa.
3 “Wipe out the day I was born, and the night when it was announced that a boy had been conceived.
“Na ipotelee mbali siku niliyozaliwa mimi, usiku uliosema, 'Mimba ya mtoto wa kiume imetungwa.'
4 Turn that day to darkness. God above should not remember it. Don't let light shine on it.
Siku hiyo na iwe giza; Mungu toka juu asiifikilie, wala mwanga usiiangazie.
5 Take it back, darkness and death-shadow. A black cloud should overshadow it. It should be as terrifying as the darkness of an eclipse during the day.
Ishikwe na giza na giza la mauti liwe lake. Wingu na likae juu yake; kila kitu kiifanyacho siku kuwa giza kweli na kiitishe.
6 Blot out that night as if it never existed. Don't count it on the calendar. Don't let it have a day in any month.
Usiku huo, na ukamatwe na giza tororo. Usihesabiwe miongoni mwa siku za mwaka; na usiwekwe katika hesabu ya miezi.
7 Let that night be childless, with no sounds of happiness heard.
Tazama, usiku huo na uwe tasa; na sauti ya shangwe isiwe ndani yake.
8 Those who place curses on certain days should curse it, those who have the power to raise Leviathan.
Na wailani siku hiyo, hao wafahamuo namna ya kumuamsha lewiathani.
9 Its early morning stars should stay dark. Looking for light, may none come, may it not see the glimmer of dawn
Nyota za mapambazuko yake zitiwe giza. Siku hiyo iutafute mwanga, lakini isiupate; wala makope ya mapambazuko isiyaone,
10 for it did not shut my mother's womb to prevent me from seeing trouble.
kwasababu haikuifunga milango ya tumbo la mama yangu, na kwasababu haikunifichia taabu machoni pangu.
11 Why wasn't I stillborn? Why didn't I die at birth?
Kwanini si-kufa wakati lipotokeza katika tumbo la uzazi? Kwanini sikuitoa roho yangu hapo mama aliponizaa?
12 Why was there a lap for me to lie on, or breasts for me to suck?
kwanini magoti yake yalinipokea? Kwanini maziwa yake yanipokee hata ninyonye?
13 For now I would be lying down in peace. I would be sleeping and at rest,
Kwa sasa ningelikuwa nimelala chini kimya kimya. Ningelala usingizi na kupata pumziko
14 along with the kings of this world and their officials whose palaces now lie in ruins,
pamoja na wafalme na washauri wa dunia, ambao walijijengea makaburi ambayo sasa ni magofu.
15 or with noblemen who collected gold and filled their houses with silver.
Au Ningelikuwa nimelala pamoja na wakuu wenye dhahabu, waliozijaza nyumba zao fedha.
16 Why wasn't I a miscarriage, buried in secret, a baby who never saw the light?
Au pengine ningekuwa sijazaliwa, kama watoto wachanga wasio uona mwanga kabisa.
17 There in the grave the wicked give no more trouble, and those whose strength is gone have their rest.
Huko waovu huacha kusumbua; huko waliochoka hupumzika.
18 There prisoners take it easy—they don't hear the commands of their oppressors.
Huko wafungwa kwa pamoja hupata amani; hawaisikii sauti ya msimamizi wa watumwa.
19 Both small and great are there, and slaves are freed from their masters.
Wote wadogo na watu maarufu wako huko; mtumishi yuko huru kwa bwana wake huko.
20 Why does God give life to those who are suffering, living bitterly miserable lives,
Kwa nini yeye aliye mashakani kupewa mwanga? Kwa nini hao wenye uchungu moyoni kupewa uhai,
21 those who are waiting for death that does not come and who are looking for death more desperately than hunting for treasure?
ambao hutamani mauti lakini hawapati; ambao huyachimbulia mauti zaidi ya kutafuta hazina iliyofichika?
22 They're so incredibly happy when the reach the grave!
Kwa nini kupewa mwanga ambao hushangilia mno na kufurahi walionapo kaburi?
23 Why is light given to someone who doesn't know where they're going, someone God has fenced in?
Kwanini kupewa mwanga mtu ambaye njia zake zimefichika, mtu ambaye Mungu amemzungushia uwa?
24 My groans are the bread I eat; my raging tears are the water I drink.
Kwa kuwa kushusha kwangu pumzi kwatokea badala ya kula; kuugua kwangu kumemiminika kama maji.
25 For all that I feared has happened to me; everything that I dreaded has come upon me.
Maana jambo lile niliogopalo limenipata; nalo linitialo hofu limenijilia.
26 I have no peace, no quiet, no rest. All that comes is rage.”
Mimi sioni raha, sipati utulivu, na sipati pumziko; badala yake huja taabu.”