< Job 3 >

1 After this Job began speaking, cursing the day of his birth.
Baada ya jambo hili, Ayubu akafumbua kinywa chake na kuilaani siku ya kuzaliwa kwake.
2 He said,
Kisha akasema:
3 “Wipe out the day I was born, and the night when it was announced that a boy had been conceived.
“Siku ya kuzaliwa kwangu na ipotelee mbali, nao usiku ule iliposemekana, ‘Mtoto wa kiume amezaliwa!’
4 Turn that day to darkness. God above should not remember it. Don't let light shine on it.
Siku ile na iwe giza; Mungu juu na asiiangalie; nayo nuru isiiangazie.
5 Take it back, darkness and death-shadow. A black cloud should overshadow it. It should be as terrifying as the darkness of an eclipse during the day.
Giza na kivuli kikuu kiikalie tena; wingu na likae juu yake; weusi na uifunike nuru yake.
6 Blot out that night as if it never existed. Don't count it on the calendar. Don't let it have a day in any month.
Usiku ule na ushikwe na giza kuu; usihesabiwe katika siku za mwaka, wala usihesabiwe katika siku za mwezi wowote.
7 Let that night be childless, with no sounds of happiness heard.
Usiku ule na uwe tasa; sauti ya furaha na isisikike ndani yake.
8 Those who place curses on certain days should curse it, those who have the power to raise Leviathan.
Wale wazilaanio siku wailaani hiyo siku, wale walio tayari kumwamsha Lewiathani.
9 Its early morning stars should stay dark. Looking for light, may none come, may it not see the glimmer of dawn
Nyota zake za alfajiri na ziwe giza; nao ungojee mwanga bila mafanikio, wala usiuone mwonzi wa kwanza wa mapambazuko,
10 for it did not shut my mother's womb to prevent me from seeing trouble.
kwa sababu huo usiku haukunifungia mlango wa tumbo la mama yangu, ili kuyaficha macho yangu kutokana na taabu.
11 Why wasn't I stillborn? Why didn't I die at birth?
“Kwa nini sikuangamia wakati wa kuzaliwa? Kwa nini sikufa nilipokuwa ninatoka tumboni?
12 Why was there a lap for me to lie on, or breasts for me to suck?
Kwa nini pakawa na magoti ya kunipokea na matiti ili nipate kunyonyeshwa?
13 For now I would be lying down in peace. I would be sleeping and at rest,
Kwa maana sasa ningekuwa nimepumzika kwa amani. Ningekuwa nimelala na kupumzika
14 along with the kings of this world and their officials whose palaces now lie in ruins,
pamoja na wafalme na washauri wa dunia, waliojijengea mahali ambapo sasa ni magofu,
15 or with noblemen who collected gold and filled their houses with silver.
pamoja na watawala waliokuwa na dhahabu, waliozijaza nyumba zao kwa fedha.
16 Why wasn't I a miscarriage, buried in secret, a baby who never saw the light?
Au kwa nini sikufichwa ardhini kama mtoto aliyezaliwa mfu, kama mtoto mchanga ambaye kamwe hakuuona mwanga?
17 There in the grave the wicked give no more trouble, and those whose strength is gone have their rest.
Huko waovu huacha kusumbua na huko waliochoka hupumzika.
18 There prisoners take it easy—they don't hear the commands of their oppressors.
Wafungwa nao hufurahia utulivu wao, hawasikii tena sauti ya kukemea ya kiongozi wa watumwa.
19 Both small and great are there, and slaves are freed from their masters.
Wadogo na wakubwa wamo humo, na mtumwa ameachiwa huru kutoka kwa bwana wake.
20 Why does God give life to those who are suffering, living bitterly miserable lives,
“Mbona nuru inawaangazia wale walio taabuni, na hao wenye uchungu kupewa uhai,
21 those who are waiting for death that does not come and who are looking for death more desperately than hunting for treasure?
wale wanaotamani kifo ambacho hakiji, wale watafutao kufa zaidi ya kutafuta hazina iliyofichwa,
22 They're so incredibly happy when the reach the grave!
ambao hujawa na furaha, na hushangilia wafikapo kaburini?
23 Why is light given to someone who doesn't know where they're going, someone God has fenced in?
Kwa nini uhai hupewa mtu ambaye njia yake imefichika, ambaye Mungu amemzungushia boma?
24 My groans are the bread I eat; my raging tears are the water I drink.
Kwa maana kulia kwangu kwa uchungu kwanijia badala ya chakula; kusononeka kwangu kunamwagika kama maji.
25 For all that I feared has happened to me; everything that I dreaded has come upon me.
Lile nililokuwa naliogopa limenijia; lile nililokuwa ninalihofia limenipata.
26 I have no peace, no quiet, no rest. All that comes is rage.”
Sina amani, wala utulivu; sina pumziko, bali taabu tu.”

< Job 3 >