< Job 26 >

1 Job replied,
Kisha Ayubu akajibu:
2 “How helpful you have been to this feeble man that I am. How supportive you have been to the weak.
“Tazama jinsi ulivyomsaidia mtu asiye na uwezo! Jinsi ulivyouokoa mkono ulio dhaifu!
3 What good advice you have given to this ignorant man, demonstrating you have so much wisdom.
Ni shauri gani ulilompa yeye asiye na hekima? Nayo ni busara gani kubwa uliyoonyesha!
4 Who helped you speak these words? Who inspired you to say such things?
Ni nani aliyekusaidia kutamka maneno hayo? Nayo ni roho ya nani iliyosema kutoka kinywani mwako?
5 The dead tremble, those beneath the waters.
“Wafu wako katika maumivu makuu, wale walio chini ya maji na wale waishio ndani yake.
6 Sheol lies naked before God, Abaddon is uncovered. (Sheol h7585)
Mauti iko wazi mbele za Mungu; Uharibifu haukufunikwa. (Sheol h7585)
7 He stretches the northern sky over empty space; he hangs the world on nothing.
Hutandaza anga la kaskazini mahali patupu; naye huiningʼiniza dunia mahali pasipo na kitu.
8 He gathers the rain in his storm clouds which do not break under the weight.
Huyafungia maji kwenye mawingu yake, hata hivyo mawingu hayapasuki kwa uzito wake.
9 He veils his throne; covering it with his clouds.
Huufunika uso wa mwezi mpevu, akitandaza mawingu juu yake.
10 On the surface of the waters he set a boundary; he set a limit dividing light from darkness.
Amechora mstari wa upeo juu ya uso wa maji, ameweka mpaka wa nuru na giza.
11 The pillars of heaven tremble; they shake with fear at his rebuke.
Nguzo za mbingu nazo zatetemeka, zinatishika anapozikemea.
12 He calmed the sea with his power; because he knew what to do he crushed Rahab.
Kwa nguvu zake aliisukasuka bahari; kwa hekima yake alimkata Rahabu vipande vipande.
13 The breath of his voice made the heavens beautiful; with his hand he pierced the gliding serpent.
Aliisafisha anga kwa pumzi yake; kwa mkono wake alimchoma joka aendaye mbio.
14 This is just a little of all he does—what we hear of him is hardly a whisper, so who can understand his thunderous power?”
Haya ni mambo madogo tu katika matendo yake; tazama jinsi ulivyo mdogo mnongʼono tunaousikia kumhusu! Ni nani basi awezaye kuelewa ngurumo za nguvu zake?”

< Job 26 >