< Job 11 >

1 Then Zophar the Naamathite began speaking and said,
Ndipo Sofari Mnaamathi alijibu na kusema,
2 “So many words be answered, shouldn't they? Or is a person proved right by doing a lot of talking?
“Huo wingi wa maneno haupaswi kujibiwa? Mtu huyu, aliyejaa maneno mengi awe wa kuaminiwa?
3 Should all your babbling force people to keep quiet? When you mock, shouldn't someone make you feel ashamed?
Kujivuna kwako kunapaswa kuwafanya wengine wabaki wamenyamaza? Wakati unapoyadhihaki mafundisho yetu, hakuna awaye yote atakayekufanya wewe ujisikie mwenye aibu?
4 You said, ‘What I teach is the pure truth,’ and ‘in God's eyes I am clean.’
Kwa kuwa wewe unasema kwa Mungu, 'Imani yangu ni safi, Mimi sina waa lolote machoni pako.'
5 If only God would speak up and tell you directly,
Lakini, laiti, Mungu huyo angesema na kufungua midomo yake dhidi yako;
6 because then he would explain to you the secrets of wisdom. True wisdom has many sides to it. God's treatment of you is far better than your guilt deserves.
hivyo angekuonyesha wewe siri za hekima! Kwa kuwa yeye ni mkuu katika ufahamu. Tena tambua huyo Mungu anataka kutoka kwako kidogo kuliko uovu wako unavyostahili.
7 Can you find out the mysteries of God? Can you discover all the wisdom of the Almighty?
Je, wewe unaweza kumfahamu Mungu kwa kumtafuta yeye? Unaweza kumtambua aliye mkuu kwa ukamilifu?
8 It is greater than the heavens—what can you do? It is deeper than Sheol—what can you know? (Sheol h7585)
Upeo uko juu kama mbingu; unaweza kufanya nini wewe? Ni wenye kina kirefu kuliko kuzimu; waweza kufahamu nini wewe? (Sheol h7585)
9 It extends farther than the earth, and wider than the sea.
Vipimo vyake ni virefu kuliko nchi, na vipana kuliko bahari.
10 If God comes and imprisons someone, or assembles the court for judgment, who can stop him?
kama yeye akipita kati na kumyamazisha mtu yeyote, kama yeye akimwita mtu yeyote hukumuni, tena ni nani anayeweza kumzuia yeye?
11 For God knows who are deceivers—when he sees someone sin, he pays attention to it.
Kwa maana anawajua watu waongo; wakati anapoona uovu, hawezi yeye kuukumbuka?
12 Stupid people will become wise when wild donkeys are born tame!
Lakini watu wapumbavu hawana ufahamu; wataupata wakati punda mwitu atakapozaa mtu.
13 But if you repent and spread out your hands to pray to him,
Lakini ikiwa umeuelekeza moyo wako kwa haki na umeunyosha mkono wako karibu na Mungu;
14 if you get rid of your sins and don't let wickedness continue in your life,
ikiwa huo uovu ulikuwa katika mikono yako, lakini hivyo tena unauweka mbali nawe, na haukuruhusu kutokuwa mwenye haki kukaa hemani mwako.
15 then you would be able to hold your head high in innocence, you will be firm and unafraid.
Ndipo kwa hakika ungeinua juu uso wako bila ishara ya aibu; Ni dhahiri, ungethibitika na usingeogopa.
16 You will forget your misery, remembering it only as water under the bridge.
Wewe ungesahau mateso yako; ungeyakumbuka hayo tu kama maji ambayo yametiririka mbali.
17 Your life will shine brighter than the noonday sun; even darkness will be like the morning.
Maisha yako yangekuwa angavu kuliko adhuhuri; japokuwa kulikuwa na giza, litakuwa kama asubuhi.
18 You will have confidence because there is hope; you will be protected and rest in safety.
Ungekuwa salama kwa sababu kuna tumaini; ni dhahiri, wewe utapata usalama juu yako na utachukua pumziko lako katika usalama.
19 You will lie down to sleep with no one to frighten you, and many will come asking for your favor.
Pia ungelala chini katika pumziko, na hakuna ambaye angekufanya wewe uogope; hakika wengi wangetafuta upendeleo wako.
20 But the eyes of the wicked will fail, they will not be able to escape, and their only hope is in death.”
Lakini macho ya watu waovu yatashindwa; hawatakuwa na njia ya kukimbia; tumaini lao la pekee litakuwa pumzi yao ya mwisho ya uhai.

< Job 11 >