< Jeremiah 50 >
1 This is the Lord's message that he told Jeremiah the prophet to give about Babylon and the country of Babylonia.
Hili ndilo neno alilosema Bwana kupitia nabii Yeremia kuhusu Babeli na nchi ya Wakaldayo:
2 Tell everyone the news! Hold up a sign and shout it out, don't hold back! Tell them, Babylon has fallen! Her god Bel is humiliated; the power of her god Marduk is broken; all Babylon's idols are humiliated and their power is broken.
“Tangazeni na mhubiri katikati ya mataifa, twekeni bendera na mkahubiri; msiache kitu chochote, bali semeni, ‘Babeli utatekwa; Beli ataaibishwa, Merodaki atajazwa na hofu kuu. Sanamu zake zitaaibishwa na vinyago vyake vitajazwa hofu kuu.’
3 A northern nation will come and attack her and turn the country into a wasteland. No one will live there—both people and animals will desert it.
Taifa kutoka kaskazini litamshambulia, na kuifanya nchi yake ukiwa. Hakuna hata mmoja atakayeishi ndani yake, watu na wanyama wataikimbia.
4 That's the time when the people of Israel and Judah will join together, weeping as they go to worship the Lord their God, declares the Lord.
“Katika siku hizo, wakati huo,” asema Bwana, “watu wa Israeli pamoja na watu wa Yuda wataenda wakilia ili kumtafuta Bwana Mungu wao.
5 They will ask the way to Zion, and start going in that direction. They will arrive and commit themselves to the Lord in an everlasting agreement that won't ever be forgotten.
Wataiuliza njia iendayo Sayuni na kuelekeza nyuso zao huko. Watakuja na kuambatana na Bwana katika agano la milele ambalo halitasahaulika.
6 My people are sheep that are lost, led astray by their shepherds, making them wander aimlessly in the mountains. They go from place to place in the mountains and hills, forgetting where they used to rest.
“Watu wangu wamekuwa kondoo waliopotea; wachungaji wao wamewapotosha na kuwasababisha kuzurura juu ya milima. Walitangatanga juu ya mlima na kilima, na kusahau mahali pao wenyewe pa kupumzikia.
7 All those who came across them attacked them. Their enemies declared, “We're not to blame! They're the ones who sinned against the Lord, their true resting place; the Lord who was the hope of their forefathers.”
Yeyote aliyewakuta aliwala; adui zao walisema, ‘Sisi hatuna hatia, kwa kuwa wao walitenda dhambi dhidi ya Bwana, malisho yao halisi, Bwana, aliye tumaini la baba zao.’
8 Run away from the city of Babylon; get away from the country of Babylonia! Lead the way like the male goats that lead the flock.
“Kimbieni kutoka Babeli; ondokeni katika nchi ya Wakaldayo tena kuweni kama mbuzi wale waongozao kundi.
9 Look! I'm assembling a coalition of strong northern nations who will come and attack Babylon. They will line up in battle against her; she will be conquered from the north. Their arrows will be like the best warriors—they don't miss!
Kwa maana nitaamsha na kuleta dhidi ya Babeli muungano wa mataifa makubwa kutoka nchi ya kaskazini. Watashika nafasi zao dhidi yake, naye kutokea kaskazini atatekwa. Mishale yao itakuwa kama mishale ya mashujaa walio hodari, ambao hawawezi kurudi mikono mitupu.
10 Babylonia will be plundered—everyone who plunders her will have plenty of loot, declares the Lord.
Kwa hiyo Ukaldayo utatekwa nyara; wote wamtekao nyara watapata za kutosha,” asema Bwana.
11 Though for now you Babylonians celebrate and sing triumphantly as you plunder my special people, though for now you jump around like a frisky young cow treading out the grain, and neigh like stallions,
“Kwa sababu hushangilia na kufurahi, wewe utekaye urithi wangu, kwa sababu unachezacheza kama mtamba anayepura nafaka, na kulia kama farasi dume,
12 you are going to bring shame on your mother, you are going to disgrace the one who gave birth to you. Watch as she becomes the least important of all the nations, a wilderness, a dry desert land.
mama yako ataaibika mno, yeye aliyekuzaa atatahayari. Atakuwa mdogo kuliko mataifa mengine yote, atakuwa nyika, nchi kame na jangwa.
13 Because of Lord's angry punishment, she will be deserted, completely desolate. Everyone who passes by will be horrified at what has happened to Babylon, and sneer at all her wounds.
Kwa sababu ya hasira ya Bwana hatakaliwa na mtu, lakini ataachwa ukiwa kabisa. Wote watakaopita Babeli watatiwa hofu na kudhihaki kwa sababu ya majeraha yake yote.
14 All you archers, line up ready for battle around Babylon. Shoot at her! Don't save your arrows, because she has sinned against the Lord.
“Shikeni nafasi zenu kuzunguka Babeli, enyi nyote mvutao upinde. Mpigeni! Msibakize mshale wowote, kwa kuwa ametenda dhambi dhidi ya Bwana.
15 Shout war-cries against her from every side! She holds up her hands in surrender. Her towers have collapsed; her walls are demolished. This is the Lord paying her back, so you too can pay her back—do the same to her as she did to others.
Piga kelele dhidi yake kila upande! Anajisalimisha, minara yake inaanguka, kuta zake zimebomoka. Kwa kuwa hiki ni kisasi cha Bwana, mlipizeni kisasi; mtendeeni kama alivyowatendea wengine.
16 Stop the sower from sowing in the country of Babylon, and stop the harvester swinging the sickle to reap the grain. Under the threat of the enemies' swords, everyone runs home to their own people, they go back to where they came from.
Katilieni mbali mpanzi kutoka Babeli, pamoja na mvunaji na mundu wake akivuna. Kwa sababu ya upanga wa mdhalimu kila mmoja na arejee kwa watu wake mwenyewe, kila mmoja na akimbilie kwenye nchi yake mwenyewe.
17 The Israelites are a flock that's been chased and scattered by lions. The first on the attack was the king of Assyria; then lastly Nebuchadnezzar king of Babylon crushed their bones.
“Israeli ni kundi lililotawanyika ambalo simba wamelifukuzia mbali. Wa kwanza kumla alikuwa mfalme wa Ashuru, wa mwisho kuponda mifupa yake alikuwa Nebukadneza mfalme wa Babeli.”
18 So this is what the Lord Almighty, the God of Israel, says: I'm going to punish the king of Babylon and his country just like I punished the king of Assyria.
Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: “Nitamwadhibu mfalme wa Babeli na nchi yake kama nilivyomwadhibu mfalme wa Ashuru.
19 I will lead the Israelites back to their pasturelands, to feed on Carmel and Bashan, to satisfy their appetites on the hills of Ephraim and Gilead.
Lakini nitamrudisha Israeli katika malisho yake mwenyewe naye atalisha huko Karmeli na Bashani; njaa yake itashibishwa juu ya vilima vya Efraimu na Gileadi.
20 This will be when the guilt and the sins of Israel and Judah will be looked for, but none will be found, because I will forgive those people who remain that I'm looking after, declares the Lord.
Katika siku hizo, wakati huo,” asema Bwana, “uchunguzi utafanyika kwa ajili ya kosa la Israeli, lakini halitakuwepo, kwa ajili ya dhambi za Yuda, lakini haitapatikana hata moja, kwa kuwa nitawasamehe mabaki nitakaowaacha.
21 Go and attack the land of Merathaim, and the people living in Pekod. Kill them with swords, set them apart for destruction, along with everything they leave behind. Make sure you do everything I have ordered you to do, declares the Lord.
“Shambulieni nchi ya Merathaimu na wale waishio huko Pekodi. Wafuatieni, waueni na kuwaangamiza kabisa,” asema Bwana. “Fanyeni kila kitu nilichowaamuru.
22 The noise of battle is heard in the country, the noise of terrible destruction.
Kelele ya vita iko ndani ya nchi, kelele ya maangamizi makuu!
23 See how the hammer of the whole earth is lying broken in pieces in the ground! The nations look with horror on what Babylon has become!
Tazama jinsi nyundo ya dunia yote ilivyovunjika na kuharibika! Tazama jinsi Babeli ilivyokuwa ukiwa miongoni mwa mataifa!
24 Babylon, I set a trap for you, and you were caught before you realized it. You were hunted down and captured because you fought against the Lord.
Nimetega mtego kwa ajili yako, ee Babeli, nawe ukakamatwa kabla haujafahamu; ulipatikana na ukakamatwa kwa sababu ulimpinga Bwana.
25 In his anger the Lord opened his armory to bring out his weapons, for this is what the Lord God Almighty is doing in the country of Babylonia.
Bwana amefungua ghala lake la silaha na kuzitoa silaha za ghadhabu yake, kwa kuwa Bwana Mwenyezi Mwenye Nguvu Zote anayo kazi ya kufanya katika nchi ya Wakaldayo.
26 Come and attack her from every side! Open her granaries; collect the loot you take from her like piles of grain. Set her apart for destruction; don't leave any survivors.
Njooni dhidi yake kutoka mbali. Zifungueni ghala zake za nafaka; mlundikeni kama lundo la nafaka. Mwangamizeni kabisa na msimwachie mabaki yoyote.
27 Kill all her young bulls with the sword; let them be slaughtered. What a disaster for them, because their time has come when they're punished.
Waueni mafahali wake wachanga wote; waacheni washuke machinjoni! Ole wao! Kwa kuwa siku yao imewadia, wakati wao wa kuadhibiwa.
28 (Listen to the refugees and survivors who have returned from Babylonia, announcing in Zion, “The Lord our God is paying them back for what happened to his Temple.”)
Wasikilizeni watoro na wakimbizi kutoka Babeli wakitangaza katika Sayuni jinsi Bwana, Mungu wetu alivyolipiza kisasi, kisasi kwa ajili ya Hekalu lake.
29 Call up the archers to attack Babylon, yes, all of them! Completely surround her—don't let anyone escape. Pay her back for what she's done, because in her pride she defied the Lord, Israel's Holy One.
“Waiteni wapiga mishale dhidi ya Babeli, wote wale wavutao upinde. Pigeni kambi kumzunguka kabisa, asitoroke mtu yeyote. Mlipizeni kwa matendo yake; mtendeeni kama alivyotenda. Kwa kuwa alimdharau Bwana, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
30 As a result her young men will be killed in the streets; all her soldiers will die that day, declares the Lord.
Kwa hiyo, vijana wake wanaume wataanguka barabarani; askari wake wote watanyamazishwa siku ile,” asema Bwana.
31 Watch out, because I'm against you, you arrogant people! declares the Lord God Almighty. Your time has come when I will punish you.
“Tazama, niko kinyume nawe, ewe mwenye majivuno,” asema Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, “kwa kuwa siku yako imewadia, yaani, wakati wako wa kuadhibiwa.
32 You arrogant people will trip and fall. Nobody will be there to pick you up. I'm going to set fire to your towns and burn up everything around you.
Mwenye majivuno atajikwaa na kuanguka, wala hakuna yeyote atakayemuinua; nitawasha moto katika miji yake, utakaowateketeza wote wanaomzunguka.”
33 This is what the Lord Almighty says: The people of Israel and Judah are being mistreated. All who captured them are holding onto them, refusing to let them go.
Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Watu wa Israeli wameonewa, nao watu wa Yuda pia. Wote waliowateka wamewashikilia sana, wanakataa kuwaachia waende.
34 But the one who rescues them is powerful; the Lord Almighty is his name. He will defend them and their cause, so he may bring peace on earth, but trouble to the people of Babylon.
Lakini Mkombozi wao ana nguvu; Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake. Atatetea kwa nguvu shauri lao ili alete raha katika nchi yao, lakini ataleta msukosuko kwa wale waishio Babeli.
35 A sword is raised to attack the Babylonians, declares the Lord, ready to attack those who live in Babylon, and her officials and wise men.
“Upanga dhidi ya Wakaldayo!” asema Bwana, “dhidi ya wale waishio Babeli na dhidi ya maafisa wake na watu wenye busara!
36 A sword is raised to attack her false prophets, and they will become fools. A sword is raised to attack her soldiers, and they will be terrified.
Upanga dhidi ya manabii wake wa uongo! Watakuwa wapumbavu. Upanga dhidi ya mashujaa wake! Watajazwa na hofu kuu
37 A sword is raised to attack her horses and chariots, along with all the foreign soldiers with her, and they will become like frightened women. A sword is raised to attack her stores of treasure, and they will be plundered.
Upanga dhidi ya farasi na magari yake ya vita pamoja na askari wake wote wa kigeni katika safu zake! Wao watakuwa kama wanawake. Upanga dhidi ya hazina zake! Hizo zitatekwa nyara.
38 A drought has hit her rivers, and they will dry up. For it's a country full of pagan images. These horrible idols drive their worshipers mad.
Ukame juu ya maji yake! Nayo yatakauka. Kwa kuwa ni nchi ya sanamu, wao wanaenda wazimu kwa ajili ya sanamu.
39 Consequently desert animals and hyenas will live there, and it will be a home for owls. It will be uninhabited forever—it won't be lived in from one generation to the next.
“Kwa hiyo, viumbe vya jangwani na fisi wataishi humo, nao bundi watakaa humo. Kamwe haitakaliwa tena wala watu hawataishi humo kutoka kizazi hadi kizazi.
40 In the same way that God destroyed Sodom and Gomorrah and their neighboring towns, declares the Lord, no one will live there, no one will stay there.
Kama vile Mungu alivyoangamiza Sodoma na Gomora pamoja na miji iliyokuwa jirani nayo,” asema Bwana, “vivyo hivyo hakuna mtu yeyote atakayeishi humo. Naam, hakuna mtu yeyote atakayekaa humo.
41 Look! An army is advancing from the north. A great nation and many kings are coming against you from the distant lands.
“Tazama! Jeshi linakuja kutoka kaskazini; taifa kubwa na wafalme wengi wanaamshwa kutoka miisho ya dunia.
42 They're carrying bows and javelins. They are cruel and merciless. When they shout it's like the sea roaring. They ride on horses and attack in formation against you, people of Babylon.
Wamejifunga pinde na mikuki; ni wakatili na wasio na huruma. Wanatoa sauti kama bahari inayonguruma wanapoendesha farasi zao; wanakuja kama watu waliojipanga tayari kwa vita ili kukushambulia, ee Binti Babeli.
43 The king of Babylon has heard the news and he's terrified. He's overcome with fear, in pain like a woman in labor.
Mfalme wa Babeli amesikia habari kuwahusu, nayo mikono yake imelegea. Uchungu umemshika, maumivu kama ya mwanamke katika utungu wa kuzaa.
44 Watch out! I'm going to come like a lion from the tangled undergrowth beside the Jordan to attack the animals grazing the green pasture. In fact I'm going to chase the Babylonians from their land very quickly. Who will I choose to conquer them? Who is like me? Who can challenge me? Which leader could oppose me?
Kama simba anayepanda kutoka vichaka vya Yordani kuja kwenye nchi ya malisho mengi, ndivyo nitamfukuza Babeli kutoka nchi yake ghafula. Ni nani aliye mteule, nitakayemweka kwa ajili ya jambo hili? Ni nani aliye kama mimi, na ni nani awezaye kunipinga? Tena ni mchungaji yupi awezaye kusimama kinyume nami?”
45 So listen to what the Lord has planned to do to Babylon and the country of Babylonia: Their children will be dragged away like lambs from the flock, and because of them their pasture will become a wasteland.
Kwa hiyo, sikia kile Bwana alichokipanga dhidi ya Babeli, kile alichokusudia dhidi ya nchi ya Wakaldayo: Aliye mchanga katika kundi ataburutwa mbali. Yeye ataharibu kabisa malisho yao kwa sababu yao.
46 The sound of Babylon's capture will make the earth shake; their cries will be heard throughout the nations.
Kwa sauti ya kutekwa kwa Babeli, dunia itatetemeka; kilio chake kitasikika pote miongoni mwa mataifa.