< Jeremiah 42 >
1 Then all the army commanders, together with Johanan son of Kareah, Jezaniah son of Hoshaiah, and everyone from the least to the most important came to
Ndipo maafisa wote wa jeshi, pamoja na Yohanani mwana wa Karea, na Yezania mwana wa Hoshaya, na watu wote kuanzia aliye mdogo kabisa hadi aliye mkuu sana wakamjia
2 Jeremiah the prophet and said, “Please listen to our request.
Yeremia nabii na kumwambia, “Tafadhali sikia maombi yetu na umwombe Bwana Mungu wako kwa ajili ya watu hawa wote waliosalia. Kwa kuwa kama unavyoona sasa, ingawa wakati fulani tulikuwa wengi, sasa tumesalia wachache tu.
3 Pray to the Lord your God for all of us. As you can see there's only a few of us left compared to how many there were before. In your prayer please ask the Lord your God to tell where to go and what to do.”
Omba ili Bwana Mungu wako atuambie twende wapi na tufanye nini.”
4 “I'll do as you ask,” Jeremiah replied. “I will definitely pray to the Lord your God as you've requested, and I'll tell you everything he says. I won't keep anything back from you.”
Nabii Yeremia akajibu, “Nimewasikia. Kwa hakika nitamwomba Bwana Mungu wenu kama mlivyoomba. Nitawaambia kila kitu asemacho Bwana, wala sitawaficha chochote.”
5 Then they said to Jeremiah, “May the Lord be a true and faithful witness against us if we don't do everything that the Lord your God tells you we should.
Kisha wakamwambia Yeremia, “Bwana na awe shahidi wa kweli na mwaminifu kati yetu kama hatutafanya sawasawa na kila kitu Bwana Mungu wako atakachokutuma utuambie.
6 Good or bad, we will obey what the Lord our God says, the one we're asking you to speak to. That way everything will go well with us, because we will be obeying what the Lord our God says.”
Likiwa jema au likiwa baya, tutamtii Bwana Mungu wetu, ambaye tunakutuma kwake, ili mambo yote yawe mema kwetu, kwa maana tutamtii Bwana Mungu wetu.”
7 Ten days later a message from the Lord came to Jeremiah.
Baada ya siku kumi, neno la Bwana likamjia Yeremia.
8 He summoned Johanan, all the army commanders, and everyone from the least to the most important.
Kwa hiyo akawaita pamoja Yohanani mwana wa Karea, na maafisa wote wa jeshi waliokuwa pamoja naye na watu wote kuanzia mdogo kabisa hadi aliye mkuu sana.
9 Jeremiah told them, This what the Lord, the God of Israel, says to those of who you sent to me to present your request:
Akawaambia, “Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye mlinituma kuwasilisha maombi yenu:
10 If you will stay right here in this country, then I will build you up and I won't tear you down; I will plant you and I won't uproot you; because I'm very sad about the disaster I have brought down on you.
‘Kama mkikaa katika nchi hii, nitawajenga wala sitawabomoa, nitawapanda wala sitawangʼoa, kwani ninahuzunishwa na maafa niliyowapiga nayo.
11 I know you fear the king of Babylon, but you don't need to be afraid of him, declares the Lord. I am with you to save you and rescue you from him.
Msimwogope mfalme wa Babeli, ambaye sasa mnamwogopa. Msimwogope, asema Bwana, kwa kuwa niko pamoja nanyi, nami nitawaokoa na kuwaponya kutoka mikononi mwake.
12 I will be merciful to you, so that he will be merciful to you and will let you stay in your own country.
Nitawaonea huruma ili naye awe na huruma nanyi na kuwarudisha katika nchi yenu.’
13 But if you say, “We won't stay here in this country,” and by doing so disobey what the Lord your God says;
“Hata hivyo, kama mkisema, ‘Hatutakaa katika nchi hii,’ hivyo mkaacha kumtii Bwana Mungu wenu,
14 or if you say instead, “No, we're going to Egypt to live there, where we won't experience war or hear trumpets sounding or go hungry;”
nanyi kama mkisema, ‘Hapana, tutakwenda kuishi Misri, mahali ambapo hatutaona vita au kusikia sauti ya tarumbeta au kuwa na njaa ya chakula,’
15 then listen to what the Lord says, you survivors from Judah! This is what the Lord Almighty, the God of Israel, says: If you're absolutely determined to go to Egypt and live there,
basi sikieni neno la Bwana, enyi mabaki ya Yuda. Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: ‘Ikiwa mmekusudia kwenda Misri na kufanya makazi huko,
16 then the war you're so frightened of will catch up with you there, and the famine you're so terrified of will chase after you into Egypt, and you will die there.
basi ule upanga mnaouogopa utawapata huko, na njaa mnayoihofia itawafuata huko Misri, nanyi mtafia huko.
17 Everyone who decides to go to Egypt and live there will die by war and famine and disease. Not a single one will survive or escape the disaster I will bring down on them.
Naam, wote waliokusudia kwenda kuishi Misri watakufa kwa upanga, njaa na tauni; hakuna hata mmoja wao atakayenusurika au kuokoka maafa nitakayoyaleta juu yao.’
18 This is what the Lord Almighty, the God of Israel, says: In the same way that my furious anger was poured out on the people living in Jerusalem, so will my anger be poured out on you if you go to Egypt. People will be horrified at what happens to you, and you will become a curse word, an insult, an expression of condemnation. You won't ever see your homeland again.
Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: ‘Kama vile hasira yangu na ghadhabu yangu ilivyomwagwa juu ya wale walioishi Yerusalemu, ndivyo ghadhabu yangu itakavyomwagwa juu yenu mtakapokwenda Misri. Mtakuwa kitu cha kulaania na cha kutisha, cha kulaumia na cha kushutumia, nanyi kamwe hamtaona mahali hapa tena.’
19 “The Lord has told you, survivors from Judah, ‘Don't go to Egypt,’” Jeremiah concluded. “Be absolutely clear about this warning I'm giving you today!
“Enyi mabaki ya Yuda, Bwana amewaambia, ‘Msiende Misri.’ Hakikisheni jambo hili: Ninawaonya leo
20 You've made a big mistake that will cost you your lives by sending me to the Lord your God, asking, ‘Pray to the Lord our God for us, and let us know everything the Lord our God says and we'll do it.’
kwamba mmefanya kosa kubwa mioyoni mwenu mliponituma kwa Bwana Mungu wenu na kusema, ‘Mwombe Bwana Mungu wetu kwa ajili yetu, nawe utuambie kila kitu atakachosema, nasi tutafanya.’
21 I have told you today what he said, but you have not obeyed everything the Lord your God sent me to tell you.
Nimewaambieni leo, lakini bado ninyi hamtaki kumtii Bwana Mungu wenu katika yote aliyonituma niwaambie.
22 So you should know that without question you're going to die by war and famine and disease in Egypt where you want to go and live.”
Basi sasa, hakikisheni jambo hili: Mtakufa kwa upanga, njaa na tauni mahali ambapo mnataka kwenda kuishi.”