< Jeremiah 39 >

1 In the tenth month of the ninth year of the reign of Zedekiah king of Judah, Nebuchadnezzar king of Babylon and his whole army arrived at Jerusalem and besieged it.
Hivi ndivyo Yerusalemu ilivyotwaliwa: Katika mwaka wa tisa wa utawala wa Mfalme Sedekia wa Yuda, katika mwezi wa kumi, Nebukadneza mfalme wa Babeli akiwa na jeshi lake lote alifanya vita dhidi ya Yerusalemu na akauzunguka mji.
2 On the ninth day of the fourth month of the eleventh year of Zedekiah's reign, the city wall was broken through.
Katika siku ya tisa ya mwezi wa nne wa mwaka wa kumi na moja wa utawala wa Sedekia, ukuta wa mji ulibomolewa.
3 All the officials of the king of Babylon came in and took over the city, making their headquarters at the Middle Gate. They were Nergal-sharezer of Samgar, Nebo-sarsekim the Rabsaris, Nergal-sharezer the Rabmag, and all the other officials of the king of Babylon.
Kisha maafisa wote wa mfalme wa Babeli wakaja na kuketi kwenye Lango la Kati, nao ni: Nergal-Shareza wa Samgari, Nebo-Sarsekimu afisa mkuu, Nergal-Shareza afisa mwenye cheo cha juu, na maafisa wengine wote wa mfalme wa Babeli.
4 When Zedekiah king of Judah and all the defenders saw them there, they ran away. They escaped from the city during the night through the king's garden, passing through the gate between the two walls, and took the road to the Arabah.
Mfalme Sedekia wa Yuda na askari wote walipowaona, wakakimbia na kuondoka mjini usiku kwa njia ya bustani ya mfalme, kupitia lango lililokuwa kati ya kuta mbili, wakaelekea Araba.
5 But the Babylonian army chased after them and caught up with Zedekiah in the plains of Jericho. They captured him and brought him before Nebuchadnezzar king of Babylon at Riblah in the land of Hamath, where he put him on trial and punished him.
Lakini jeshi la Wakaldayo likawafuatia na kumpata Sedekia katika sehemu tambarare za Yeriko. Wakamkamata na kumpeleka kwa Nebukadneza mfalme wa Babeli huko Ribla, katika nchi ya Hamathi, mahali ambapo alimtangazia hukumu.
6 The king of Babylon had Zedekiah's sons killed as Zedekiah watched, and he also executed all of Judah's leaders there in Riblah.
Huko Ribla, mfalme wa Babeli aliwachinja wana wa Sedekia mbele ya macho yake, na pia akawaua wakuu wote wa Yuda.
7 Then he had Zedekiah's eyes gouged out, and had him bound with bronze chains and taken away to Babylon.
Kisha akayangʼoa macho ya Sedekia na kumfunga kwa pingu za shaba na kumpeleka Babeli.
8 The Babylonians burned down the king's palace and the people's houses, and they demolished Jerusalem's city walls.
Jeshi la Wakaldayo likachoma moto jumba la kifalme na nyumba za watu, na kuzibomoa kuta za Yerusalemu.
9 Then Nebuzaradan the commander of the guard carried off to Babylon the rest of the people who had stayed in the city, together with those who had deserted and gone over to him.
Nebuzaradani kiongozi wa walinzi wa mfalme akawachukua na kuwapeleka uhamishoni Babeli watu waliokuwa wamebaki ndani ya mji, pamoja na wale waliokuwa wamejisalimisha kwake, na watu wengine wote.
10 But he left behind in the land of Judah some of the poorest people who didn't have any property. He gave them vineyards and fields at that time.
Lakini Nebuzaradani kiongozi wa walinzi aliwabakiza baadhi ya watu maskini katika nchi ya Yuda, ambao hawakuwa na kitu. Naye wakati huo akawapa mashamba ya mizabibu na mashamba mengine.
11 Nebuchadnezzar king of Babylon had given orders to Nebuzaradan the commander of the guard regarding Jeremiah, saying,
Basi, Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuwa ametoa maagizo kuhusu Yeremia kupitia Nebuzaradani kiongozi wa walinzi wa mfalme akisema:
12 “Go and get Jeremiah and watch out that nothing bad happens to him. Do whatever he wants.”
“Mchukue umtunze. Usimdhuru, lakini umfanyie chochote anachotaka.”
13 So Nebuzaradan the commander of the guard, Nebushazban the Rabsaris, Nergal-sharezer the Rabmag, and all the army captains of the king of Babylon
Basi Nebuzaradani kiongozi wa walinzi, Nebushazbani afisa mkuu, Nergal-Shareza afisa wa cheo cha juu, na maafisa wengine wote wa mfalme wa Babeli
14 took Jeremiah from the guard's courtyard, and they handed him over to Gedaliah son of Ahikam, the son of Shaphan, to take him home. Jeremiah stayed there with his own people.
wakatuma watu kumwondoa Yeremia kutoka ua wa walinzi. Wakamkabidhi kwa Gedalia mwana wa Ahikamu mwana wa Shafani, ili amrudishe nyumbani kwake. Kwa hiyo akabaki miongoni mwa watu wake mwenyewe.
15 During the time that Jeremiah had been kept prisoner in the guard's courtyard, a message from the Lord had come to him:
Wakati Yeremia alipokuwa amezuiliwa katika ua wa walinzi, neno la Bwana lilimjia kusema:
16 “Go and tell Ebed-melech the Cushite that this is what the Lord Almighty, the God of Israel, says: I am about to keep my promise I made against this city—to harm it and not to help it—you'll see it for yourself when it happens.
“Nenda ukamwambie Ebed-Meleki Mkushi, ‘Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Ninakaribia kutimiza maneno yangu dhidi ya mji huu kwa njia ya maafa, wala si kwa kuwafanikisha. Wakati huo hayo yatatimizwa mbele ya macho yako.
17 But when that day comes I'm going to save you, declares the Lord. You won't be handed over to the people you're afraid of.
Lakini siku hiyo nitakuokoa, asema Bwana; hutatiwa mikononi mwa wale unaowaogopa.
18 I promise to rescue you so that you're won't be killed. Your reward will be your life, because you trusted in me, declares the Lord.”
Nitakuokoa; hutaanguka kwa upanga, lakini maisha yako yatakuwa salama, kwa sababu unanitumaini, asema Bwana.’”

< Jeremiah 39 >