< Jeremiah 19 >
1 This is what the Lord says: Go and buy a clay jar from a potter. Take some of the elders of the people and leaders of the priests with you,
Hili ndilo asemalo Bwana: “Nenda ukanunue gudulia la udongo kutoka kwa mfinyanzi. Wachukue baadhi ya wazee wa watu na wa makuhani
2 and go through the Broken Pottery Gate to the valley of Ben-hinnom. Announce this message I'm giving you.
na mtoke mwende mpaka kwenye Bonde la Ben-Hinomu, karibu na ingilio la Lango la Vigae. Huko tangaza maneno ninayokuambia,
3 Tell them, Listen to what the Lord says, kings of Judah and people living in Jerusalem. This is what the Lord Almighty, the God of Israel, says: I am going to bring down on this place such a disaster that it will make the ears of anyone who hears about it ring.
nawe useme, ‘Sikieni neno la Bwana, enyi wafalme wa Yuda na watu wa Yerusalemu. Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Sikilizeni! Nitaleta maafa mahali hapa, ambayo yatafanya masikio ya kila mmoja atakayesikia habari zake yawashe.
4 My people have deserted me and have made this a place where foreign gods are worshiped. They have burned incense in it to other gods that they and their forefathers and the kings of Judah never knew anything about. They have filled this place with the blood of innocent people.
Kwa kuwa wameniacha na kupafanya mahali hapa kuwa pa miungu ya kigeni. Wameiteketezea sadaka miungu ambayo wao wala baba zao wala wafalme wa Yuda kamwe hawakuijua, nao wamelijaza eneo hili kwa damu isiyo na hatia.
5 They have built pagan shrines to Baal where they burn their children in the fire as offerings to Baal. This is something I never commanded or even mentioned. I never even thought of such a thing!
Wamejenga mahali pa juu pa kuabudia miungu pa Baali ili kuteketeza wana wao katika moto kama sadaka kwa Baali, kitu ambacho sikukiamuru wala kukitaja, wala hakikuingia akilini mwangu.
6 So watch out! The time is coming, declares the Lord, when instead of Topheth and the Valley of Hinnom this place will be called the Valley of Killing.
Hivyo jihadharini, siku zinakuja, asema Bwana, wakati watu hawatapaita tena mahali hapa Tofethi ama Bonde la Ben-Hinomu, bali Bonde la Machinjo.
7 Right here in this place I'm going to spoil the plans of Judah and Jerusalem. I will let their enemies who want to kill them come and do exactly that. Their dead bodies will be food for birds of prey and wild animals.
“‘Nitaiharibu mipango ya Yuda na Yerusalemu mahali hapa. Nitawafanya waanguke kwa upanga mbele ya adui zao, katika mikono ya wale watafutao uhai wao, nami nitaitoa mizoga yao kuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wa nchi.
8 I'm going to make this city desolate, a place that is mocked. Everyone who passes by will be horrified, shocked by all its damage.
Nitauharibu mji huu na kuufanya kitu cha kudharauliwa. Wote wapitao karibu watashangaa na kuudhihaki kwa sababu ya majeraha yake yote.
9 The siege brought by their enemies who want to kill them will be so terrible that I will make them eat each other, even their own sons and daughters.
Nitawafanya wao kula nyama ya wana wao na binti zao; kila mmoja atakula nyama ya mwenzake wakati wa dhiki ya kuzungukwa na jeshi lililowekwa juu yao na adui wanaotafuta uhai wao.’
10 Then smash the jar in front of the people with you.
“Kisha livunje lile gudulia wale walio pamoja nawe wakiwa wanaangalia,
11 Tell them: this is what the Lord Almighty says: I'm going to smash this nation and this city, just like a clay jar is smashed so it can't ever be repaired. People will bury their dead in Topheth until it's full.
uwaambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: Nitalivunja taifa hili na mji huu kama gudulia hili la mfinyanzi lilivyovunjwa, nalo haliwezi kutengenezeka tena. Watawazika waliokufa huko Tofethi hata isiwepo nafasi zaidi.
12 This is what I'm going to do to this place and to the people who live here, declares the Lord. I will turn this city into Topheth.
Hivi ndivyo nitakavyopafanya mahali hapa na kwa wale waishio ndani yake, asema Bwana. Nitaufanya mji huu kama Tofethi.
13 All the houses of Jerusalem and the palaces of the kings of Judah will become unclean just like Topheth, because they are all the houses whose rooftops they used to burn incense to the sun, moon, and stars, and poured out drink offerings to other gods.
Nyumba zilizoko Yerusalemu na zile za wafalme wa Yuda zitatiwa unajisi kama mahali hapa, Tofethi: yaani nyumba zote ambazo walifukiza uvumba juu ya mapaa yake kwa jeshi lote la angani, na kumimina dhabihu za vinywaji kwa miungu mingine.’”
14 Jeremiah returned from Topheth, where the Lord had sent him to deliver this message. He went and stood in the court of the Lord's Temple and announced to everyone,
Kisha Yeremia akarudi kutoka Tofethi, mahali ambapo Bwana alikuwa amemtuma kutoa unabii, akasimama katika ua wa Hekalu la Bwana na kuwaambia watu wote,
15 This is what the Lord Almighty, the God of Israel, says: Watch out! I am about to bring down on this city and on all its surrounding villages every disaster I warned them about, because they have stubbornly refused to listen to what I say.
“Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: ‘Sikilizeni! Nitaleta juu ya mji huu pamoja na vijiji vinavyouzunguka kila maafa niliyosema dhidi yake, kwa sababu wamekuwa na shingo ngumu, na hawakuyasikiliza maneno yangu.’”