< Jeremiah 12 >

1 Lord, when I complain to you, you always show yourself to be in the right. Even so I still want to present my case to you. Why is it that wicked people do so well? Why do those who are unfaithful to you live so comfortably?
Wewe daima u mwenye haki, Ee Bwana, niletapo mashtaka mbele yako. Hata hivyo nitazungumza nawe kuhusu hukumu yako: Kwa nini njia ya waovu inafanikiwa? Kwa nini wasio waaminifu wote wanaishi kwa raha?
2 You planted them, and they've taken root, grown, and produced fruit. They're always talking about you but they don't think of you, even for a moment.
Umewapanda, nao wameota, wanakua na kuzaa matunda. Daima u midomoni mwao, lakini mbali na mioyo yao.
3 But you know me, Lord, you see me, and examine what I think about you. Drag off these people like sheep to be slaughtered; keep them apart for the time when they're killed.
Hata hivyo unanijua mimi, Ee Bwana; unaniona na kuyachunguza mawazo yangu kukuhusu wewe. Wakokote kama kondoo wanaokwenda kuchinjwa! Watenge kwa ajili ya siku ya kuchinjwa!
4 How long will the land have to mourn and the grass in every field be dried up because of the evil of the people who live there? The animals and birds have died out because the people have said, “He doesn't know what's going to happen to us.”
Je, nchi itakaa katika hali ya kuomboleza mpaka lini, na majani katika kila shamba kunyauka? Kwa sababu wale waishio ndani yake ni waovu, wanyama na ndege wameangamia. Zaidi ya hayo, watu wanasema, “Bwana hataona yatakayotupata sisi.”
5 The Lord says, Once you've become worn out in a foot race against men, how would you win racing against horses? If you trip up in open ground, how would you do in the tangled undergrowth beside the Jordan?
“Ikiwa umeshindana mbio na watu kwa mguu na wakakushinda, unawezaje kushindana na farasi? Ikiwa unajikwaa kwenye nchi ambayo ni salama, utawezaje kwenye vichaka kando ya Yordani?
6 Even your own brothers and your father's family have betrayed you; they have publicly criticized you. Don't trust them when they talk nicely to you!
Ndugu zako, watu wa jamaa yako mwenyewe: hata wao wamekusaliti; wameinua kilio kikubwa dhidi yako. Usiwaamini, ingawa wanazungumza mema juu yako.
7 I have given up on my people; I have abandoned the nation I chose. I have handed over the ones I truly love to their enemies.
“Nitaiacha nyumba yangu, nitupe urithi wangu; nitamtia yeye nimpendaye mikononi mwa adui zake.
8 They've turned into a wild lion, roaring at me—that's why I hate them.
Urithi wangu umekuwa kwangu kama simba wa msituni. Huningurumia mimi, kwa hiyo ninamchukia.
9 My people are like a spotted bird of prey to me with other birds of prey circling to attack it. Go and bring all the wild animals to eat up the carcass.
Je, urithi wangu haukuwa kama ndege wa mawindo wa madoadoa ambaye ndege wengine wawindao humzunguka na kumshambulia? Nenda ukawakusanye pamoja wanyama wote wa mwituni; walete ili wale.
10 Many shepherds have come and destroyed my vineyard; they have trampled down the crops in my field. They have turned my pleasant land into an empty wasteland.
Wachungaji wengi wataliharibu shamba langu la mizabibu na kulikanyaga shamba langu; watalifanya shamba langu zuri kuwa jangwa la ukiwa.
11 They have made it into a desert; it mourns before me, lying desolate. The whole country is a wasteland, but no one cares.
Litafanywa kuwa jangwa, lililokauka na kuachwa ukiwa mbele zangu; nchi yote itafanywa jangwa kwa sababu hakuna hata mmoja anayejali.
12 The destructive armies have crossed all the bare desert hills for the Lord's sword destroys from one end of the country to the other. No one has any peace.
Juu ya miinuko yote ilivyo kama jangwani mharabu atajaa, kwa maana upanga wa Bwana utawala, kuanzia ncha moja ya nchi hadi nyingine; hakuna hata mmoja atakayekuwa salama.
13 My people sowed wheat but harvested thorns. They wore themselves out but gained no benefit. You should be ashamed of such a poor harvest, caused by the Lord's furious anger.
Watapanda ngano lakini watavuna miiba; watajitaabisha lakini hawatafaidi chochote. Kwa hiyo beba aibu ya mavuno yako kwa sababu ya hasira kali ya Bwana Mungu.”
14 This is what the Lord says: When it comes these evil nearby nations who attack the country that I gave to my people Israel, I'm going to uproot them from their land. I'm also going to uproot the people of Judah from among them.
Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa habari ya majirani zangu wote wabaya wanaonyangʼanya urithi ambao ninawapa watu wangu Israeli, nitawangʼoa kutoka nchi zao, nami nitaingʼoa nyumba ya Yuda kutoka katikati yao.
15 However, once I have uprooted them, I will have mercy on them again, and bring each one back to their property and their land.
Lakini baada ya kuwangʼoa, nitawahurumia tena na kumrudisha kila mmoja wao kwenye urithi wake mwenyewe na kwenye nchi yake mwenyewe.
16 If they will honestly learn the ways of my people and respect me, making their vows to me, just as they once taught my people to swear by Baal, then they will do well among my people.
Ikiwa watajifunza vyema njia za watu wangu na kuapa kwa Jina langu, wakisema, ‘Hakika kama Bwana aishivyo,’ hata kama wakati fulani walifundisha watu wangu kuapa kwa Baali, ndipo watakapofanywa imara katikati ya watu wangu.
17 But if they refuse to obey, then I will not only uproot that nation but I will completely destroy it, declares the Lord.
Lakini kama taifa lolote halitasikiliza na kutii, nitalingʼoa kabisa na kuliangamiza,” asema Bwana.

< Jeremiah 12 >