< Isaiah 48 >
1 Listen to this, descendants of Jacob, called by the name of Israel, and who come from the lineage of Judah. Listen, you people who swear by the name of the Lord, or who invoke the God of Israel, but not truly or sincerely.
“Sikilizeni hili, ee nyumba ya Yakobo, ninyi mnaoitwa kwa jina la Israeli, na mnaotoka katika ukoo wa Yuda, ninyi mnaoapa kwa jina la Bwana, mnaomwomba Mungu wa Israeli, lakini si katika kweli au kwa haki;
2 You say you're from the “Holy City,” and claim you're trusting in the God of Israel, whose name is the Lord Almighty.
ninyi mnaojiita raiya wa mji mtakatifu, na kumtegemea Mungu wa Israeli, Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake:
3 I predicted long ago what was going to happen—I said it and let people know. Then suddenly I decided to act, and it all came true.
Nilitoa unabii mambo ya kwanza tangu zamani, kinywa changu kiliyatangaza na kuyafanya yajulikane; kisha ghafula nikayatenda, nayo yakatokea.
4 I know how stubborn you are, with necks as unbending as iron and foreheads as hard as bronze.
Kwa kuwa nalijua jinsi ulivyokuwa mkaidi; mishipa ya shingo yako ilikuwa chuma, kipaji chako cha uso kilikuwa shaba.
5 I predicted these things to you long ago, before they happened. I explained them to you so that you couldn't say “My idol did this,” or “My image and my metal god ordered this to happen.”
Kwa hiyo nilikuambia mambo haya tangu zamani, kabla hayajatokea nilikutangazia ili usije ukasema, ‘Sanamu zangu zilifanya hayo; kinyago changu cha mti na mungu wangu wa chuma aliyaamuru.’
6 You've heard all I predicted, and seen it happen. Won't you admit it? Now I'm going to tell you new things, secrets you don't know anything about.
Umesikia mambo haya; yaangalie hayo yote. Je, hutayakubali? “Kuanzia sasa na kuendelea nitakueleza mambo mapya, juu ya mambo yaliyofichika usiyoyajua.
7 These are brand-new, not something from the past. Before today you won't have heard anything about them, so you can't say, “Oh yes, I know about that.”
Yameumbwa sasa, wala si tangu zamani; hukupata kuyasikia kabla ya siku ya leo. Hivyo huwezi kusema, ‘Naam, niliyajua hayo.’
8 No, you've never heard that, and you've never known that! Nobody's told you about that before! I know how deviously you operate—you're called “rebels from birth”!
Hujayasikia wala kuyaelewa, tangu zamani sikio lako halikufunguka. Ninafahamu vyema jinsi ulivyo mdanganyifu, uliitwa mwasi tangu kuzaliwa kwako.
9 But because of my nature I am delaying my punishment; and because of my reputation, I'm not going to destroy you.
Kwa ajili ya Jina langu mwenyewe ninaichelewesha ghadhabu yangu, kwa ajili ya sifa zangu nimeizuia isikupate, ili nisije nikakukatilia mbali.
10 Look how I've refined you, but not like silver—I chose you in the furnace of trouble.
Tazama, nimekusafisha, ingawa si kama fedha, nimekujaribu katika tanuru ya mateso.
11 The reason I'm doing this is because of who I am, yes, because of my very nature. I won't let my reputation be damaged—I won't let anyone else have it.
Kwa ajili yangu mwenyewe, kwa ajili yangu mwenyewe, nafanya hili. Jinsi gani niliache Jina langu lichafuliwe? Sitautoa utukufu wangu kwa mwingine.
12 Listen to me, Jacon, and Israel, the one I called. Only I am God. I am the first, and I am the last.
“Ee Yakobo, nisikilize mimi, Israeli, ambaye nimekuita: Mimi ndiye; mimi ndimi mwanzo na mwisho.
13 I laid the foundations of the earth with my own hands; I personally spread out the heavens. When I call the stars, they all take their positions.
Mkono wangu mwenyewe uliweka misingi ya dunia, nao mkono wangu wa kuume umezitanda mbingu; niziitapo, zote husimama pamoja.
14 Everyone gather round and listen. Which of your “gods” told you anything like this? The one the Lord loves will carry out the Lord's wishes against Babylon—he will attack the Babylonians.
“Kusanyikeni, ninyi nyote, msikilize: Ni ipi miongoni mwa hizo sanamu ambayo imetabiri vitu hivi? Watu wa Bwana waliochaguliwa na kuungana watatimiza kusudi lake dhidi ya Babeli; mkono wa Mungu utakuwa dhidi ya Wakaldayo.
15 I myself have spoken. I have called him to do this, and he will be successful in what he does.
Mimi, naam, Mimi, nimenena; naam, nimemwita yeye. Nitamleta, naye atafanikiwa katika lile nililomtuma.
16 Come close to me, and listen to this. From the very beginning I haven't spoken in secret; I am always there right when it happens. Now the Lord God and his Spirit has sent me to tell you this:
“Nikaribieni na msikilize hili: “Tangu tangazo la kwanza sikusema kwa siri; wakati litokeapo, nitakuwako hapo.” Sasa Bwana Mwenyezi amenituma, kwa Roho wake.
17 This is what the Lord says, your Redeemer, the Holy One of Israel, I am the Lord your God. I am the one who teaches you what is good for you, who leads you along the way you should go.
Hili ndilo asemalo Bwana, Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli: “Mimi ni Bwana, Mungu wako, nikufundishaye ili upate faida, nikuongozaye katika njia ikupasayo kuiendea.
18 If you had only listened carefully to what I told you! Then your blessings would have flowed like a river, and goodness would have washed over you like the waves of the sea.
Laiti ungesikiliza kwa makini maagizo yangu, amani yako ingekuwa kama mto, haki yako kama mawimbi ya bahari.
19 Your children, your descendants, would have been like all those grains of sand. They wouldn't have had to be destroyed, wiped out before me.
Wazao wako wangekuwa kama mchanga, watoto wako kama chembe zake zisizohesabika; kamwe jina lao lisingefutiliwa mbali, wala kuangamizwa kutoka mbele zangu.”
20 Leave Babylon! Run away from Babylonia with happy shouts! Let everyone know, telling the whole earth, “The Lord has redeemed his servant Jacob!”
Tokeni huko Babeli, kimbieni kutoka kwa Wakaldayo! Tangazeni hili kwa kelele za shangwe na kulihubiri. Lipelekeni mpaka miisho ya dunia; semeni, “Bwana amemkomboa mtumishi wake Yakobo.”
21 They weren't thirsty when he led them through the desert—he made water come out of the rock for them. He split the rock open and water poured out.
Hawakuona kiu alipowaongoza kupita jangwani; alifanya maji yatiririke kutoka kwenye mwamba kwa ajili yao; akapasua mwamba na maji yakatoka kwa nguvu.
22 The wicked have no peace, says the Lord.
“Hakuna amani kwa waovu,” asema Bwana.