< Isaiah 16 >
1 Send lambs as tribute to the ruler of the land, from Sela through the desert, to the mountain of the daughter of Zion.
Pelekeni wana-kondoo kama ushuru kwa mtawala wa nchi, Kutoka Sela, kupitia jangwani, hadi mlima wa Binti Sayuni.
2 The Moabite women at the fords of the Arnon are like birds fluttering around when their nest is destroyed.
Kama ndege wanaopapatika waliofukuzwa kutoka kwenye kiota, ndivyo walivyo wanawake wa Moabu kwenye vivuko vya Arnoni.
3 Think about it and make a decision. Make your shadow as invisible at midday as during the night. Hide the refugees; don't betray them as they run away.
“Tupeni shauri, toeni uamuzi. Wakati wa adhuhuri, fanyeni kivuli chenu kama usiku. Waficheni watoro, msisaliti wakimbizi.
4 Let my refugees stay among you, Moab. Hide them from our enemies until the destroyer is no more, the destruction is over, and the aggressive invaders have gone.
Waacheni watoro wa Moabu wakae pamoja nanyi; kuweni mahali pao pa salama ili kuepuka mharabu.” Mtesi atafikia mwisho na maangamizi yatakoma, aletaye vita atatoweka kutoka nchi.
5 Then a kingdom will be set up based on trustworthy love, and on its throne will sit a faithful king from the line of David. He will judge fairly, and will be passionately committed to doing what is right.
Kwa upendo kiti cha enzi kitaimarishwa, kwa uaminifu mtu ataketi juu yake, yeye atokaye nyumba ya Daudi: yeye ambaye katika kuhukumu hutafuta haki, na huhimiza njia ya haki.
6 We know all about the pride of the Moabites, how terribly vain and conceited they are, completely arrogant! But their boasting is false.
Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu: kiburi chake cha kujivuna na udanganyifu, kiburi chake na ufidhuli wake, lakini majivuno yake si kitu.
7 All the Moabites grieve for Moab. They all mourn the loss of the raisin cakes of Kir-hareseth, all of them destroyed.
Kwa hiyo Wamoabu wanaomboleza, wanaiombolezea Moabu kwa pamoja. Wanaomboleza na kuhuzunika kwa ajili ya watu wa Kir-Haresethi.
8 Heshbon's fields have dried up, as have Sibmah's grapevines. The rulers of the nations have trampled down the vines that once branched out to Jazer and east towards the desert, and west as far as the sea.
Mashamba ya Heshboni yananyauka, pia na mizabibu ya Sibma. Watawala wa mataifa wamekanyaga mizabibu iliyo mizuri sana, ambayo ilipata kufika Yazeri na kuenea kuelekea jangwani. Machipukizi yake yalienea yakafika hadi baharini.
9 So I cry with Jazer for Sibmah's vines; I soak Heshbon and Elealeh with my tears. Nobody shouts in celebration over your summer fruit and your harvest any more.
Hivyo ninalia kama Yazeri aliavyo, kwa ajili ya mizabibu ya Sibma. Ee Heshboni, ee Eleale, ninakulowesha kwa machozi! Kelele za furaha kwa ajili ya tunda lako lililoiva na kwa ajili ya mavuno zimekomeshwa.
10 Joy and happiness are gone. Nobody celebrates in the harvest fields or the vineyards; nobody shouts happily. Nobody treads grapes in the winepresses. I have stopped their cheering.
Furaha na shangwe zimeondolewa kutoka mashamba ya matunda; hakuna yeyote aimbaye wala apazaye sauti katika mashamba ya mizabibu; hakuna yeyote akanyagaye zabibu shinikizoni, kwa kuwa nimekomesha makelele.
11 Heartbroken I cry for Moab like sad music on a harp; deep inside I weep for Kir-hareseth.
Moyo wangu unaomboleza kwa ajili ya Moabu kama kinubi, nafsi yangu yote kwa ajili ya Kir-Haresethi.
12 The Moabites go and wear themselves out worshiping at their high places. They go to their shrines to pray, but it does them no good.
Wakati Moabu anapojitokeza mahali pake pa juu, anajichosha mwenyewe tu; anapokwenda mahali pake pa kuabudia miungu ili kuomba, haitamfaidi lolote.
13 This is the message that the Lord has already delivered about Moab.
Hili ndilo neno ambalo Bwana ameshasema kuhusu Moabu.
14 But now the Lord speaks again, and says, In three years, just as a contract worker precisely counts years, Moab's glory will turn into something to be laughed at. Despite there being so many Moabites now, soon there will only be a few feeble people left.
Lakini sasa Bwana anasema: “Katika miaka mitatu, kama vile mtumishi aliyefungwa na mkataba angeihesabu, fahari ya Moabu na watu wake wengi watadharauliwa, nao walionusurika watakuwa wachache sana, tena wanyonge.”