< Hosea 7 >

1 when I heal Israel, Ephraim's sins will be exposed, together with the evil actions of Samaria. They deal in lies; they are thieves who break into homes and rob people on the outside.
Wakati wowote ninapotaka kuponya Israeli, dhambi ya Efraimu inafunuliwa, pamoja na matendo maovu ya Samaria, kwa sababu wanafanya udanganyifu; mwizi huingia, na kundi la wanyang'anyi hushambulia mitaani.
2 But they don't realize that I remember all of their wickedness. Their sins surround them and are always before me.
Hawatambui mioyoni mwao kwamba ninakumbuka matendo yao mabaya. Sasa matendo yao huwazunguka; yapo mbele ya uso wangu.
3 They make their king happy with their wickedness, and the princes with their lies.
Kwa sababu ya uovu wao wamemfanya mfalme awe na furaha, na maofisa wao kwa uongo wao.
4 All of them are adulterers, burning with lust like an oven whose fire stays hot, even though it is not tended by the baker, having left the dough to rise after kneading.
Wote ni wazinzi, kama tanuru iliyochomwa na mwokaji, ambaye huacha kuuchochea moto tangu kukanda unga mpaka kuwa chachu.
5 On the king's birthday the princes drink so much they are sick, while he joins in with those who mock.
Siku ya mfalme wetu, viongozi walijifanya wagonjwa na ukali wa divai. Alinyoosha mkono wake kwa wale waliokuwa wakidhihaki.
6 Their minds are fired up like an oven; they go to him with their plots. All through the night their anger burns; in the morning it blazes out uncontrollably.
kwa mioyo kama tanuri, wao hupanga mipango yao ya udanganyifu. Hasira zao hulala usiku wote; asubuhi huwaka juu kama moto.
7 All of them are as hot as a burning oven, and they exhaust their leaders. All of their kings have fallen, and not one of them calls on me.
Wote wamepata moto kama tanuru, na huwaangamiza wale wanaowatawala. Wafalme wao wote wameanguka; hakuna hata mmoja wao ananiita.
8 Ephraim mixes with the foreign nations; he is as useless as half-baked bread!
Efraimu anajichanganya mwenyewe kati ya watu. Efraimu ni mkate ambayo haujawahi kugeuzwa.
9 Foreigners drain his strength, and he doesn't even realize it. His hair is turning grey and he doesn't even notice.
Wageni wamekula nguvu zake, lakini hajui. Nywele za mvi hunyunyiza juu yake, lakini hajui.
10 Israel's pride testifies against him, but for all of this he still does not return to the Lord their God or look for him.
Kiburi cha Israeli kinawashuhudia; hata hivyo, hawajarudi kwa Bwana, Mungu wao, wala hawakumtafuta licha ya hayo yote.
11 Ephraim is like a dove, foolish and without sense—calling to Egypt, then going to Assyria.
Efraimu ni kama njiwa, baradhuli na asiye na busara, humwita kwenda Misri, kisha huruka kwenda Ashuru.
12 When they go I will throw my net over them; I will bring them down like wild birds. When I hear them flocking together I will punish them.
Wakienda, nitasambaza wavu wangu juu yao, nami nitawaangusha kama ndege wa angani. Nitawaadhibu katika kusonga kwao pamoja.
13 What disaster is coming to them because they have strayed from me! Destruction is coming to them because they have rebelled against me! I wish I could redeem them, but they tell lies about me.
Ole wao! Kwa maana wamepotea kutoka kwangu. Uharibifu unawajia! Wao wameasi dhidi yangu! Napenda kuwaokoa, lakini waliongea uongo dhidi yangu.
14 They do not cry out to me with sincere minds; instead they lie on their beds howling. They assemble together and gash themselves to gain grain and new wine, but they turn away from me.
Wala hawakunililia kwa moyo wao wote, lakini wanaomboleza kwenye vitanda vyao. Wanakusanyika kwa ajili ya nafaka na divai mpya, nao wananiasi mimi.
15 I myself trained them and made them strong, but now they plot evil against me.
Ingawa niliwafundisha na kuimarisha mikono yao, sasa wanapanga mabaya dhidi yangu.
16 They turn, but not to the Most High; they are like a useless bow. Their leaders will be killed by the sword because of their cursing. Because of this they will be ridiculed in Egypt.
Wanarudi, lakini harudi kwangu, Niliye Juu. Wao ni kama upinde usiotumainika. Maofisa wao wataanguka kwa upanga kwa sababu ya udhalimu wa vinywa. Hii itakuwa ni aibu yao katika nchi ya Misri.

< Hosea 7 >