< Hebrews 1 >
1 God, who in the past spoke to our forefathers through the prophets at various times and in many ways,
Zamani Mungu alisema na baba zetu kwa njia ya manabii mara nyingi na kwa njia mbalimbali,
2 has in these last days spoken to us through his Son. God appointed the Son heir of everything, and made the universe through him. (aiōn )
lakini katika siku hizi za mwisho anasema nasi kwa njia ya Mwanawe, ambaye amemweka kuwa mrithi wa vitu vyote, na ambaye kupitia kwake aliuumba ulimwengu. (aiōn )
3 The Son is the radiant glory of God, and the visible expression of his true character. He sustains everything by his powerful command. When he had provided cleansing for sin he sat down at the right hand of the Majesty in heaven.
Mwana ni mngʼao wa utukufu wa Mungu na mfano halisi wa nafsi yake, akivihifadhi vitu vyote kwa neno lake lenye uweza. Akiisha kufanya utakaso kwa ajili ya dhambi, aliketi mkono wa kuume wa Aliye Mkuu huko mbinguni.
4 He was placed much higher than the angels since he received a greater name than them.
Kwa hiyo alifanyika bora kuliko malaika, kama jina alilorithi lilivyo bora kuliko lao.
5 God never said to any angel, “You are my Son; today I have become your Father,” or “I will be a Father to him, and he will be a Son to me.”
Kwa maana ni malaika yupi ambaye wakati wowote Mungu alipata kumwambia, “Wewe ni Mwanangu; leo mimi nimekuzaa?” Au tena, “Mimi nitakuwa Baba yake, naye atakuwa Mwanangu?”
6 Also, when he brought his firstborn Son into the world, he said, “Let all God's angels worship him.”
Tena, Mungu amletapo mzaliwa wake wa kwanza ulimwenguni, anasema, “Malaika wote wa Mungu na wamsujudu.”
7 Regarding the angels, he says, “He makes his angels winds, and his servants flames of fire,”
Anenapo kuhusu malaika asema, “Huwafanya malaika wake kuwa pepo, watumishi wake kuwa miali ya moto.”
8 but about the Son he says, “Your throne, God, lasts forever and ever, and justice is the ruling scepter of your kingdom. (aiōn )
Lakini kwa habari za Mwana asema, “Kiti chako cha enzi, Ee Mungu, kitadumu milele na milele, nayo haki itakuwa fimbo ya utawala ya ufalme wako. (aiōn )
9 You love what is right, and hate what is lawless. That is why God, your God, has placed you above everyone else by anointing you with the oil of joy.”
Umependa haki na kuchukia uovu; kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekuweka juu ya wenzako kwa kukupaka mafuta ya furaha.”
10 “You, Lord, laid the foundations of the earth in the beginning. The heavens are the product of your hands.
Pia asema, “Hapo mwanzo, Ee Bwana, uliweka misingi ya dunia, nazo mbingu ni kazi ya mikono yako.
11 They will come to an end, but you will continue. They will wear out like clothes do,
Hizo zitatoweka, lakini wewe utadumu; zote zitachakaa kama vazi.
12 and you will roll them up like a cloak. Like clothes, they will be changed, but you never change, and your life never ends.”
Utazikungʼutakungʼuta kama joho, nazo zitachakaa kama vazi. Lakini wewe hubadiliki, nayo miaka yako haikomi kamwe.”
13 But he never said to any angel, “Sit at my right hand until I place your enemies in subjection under your feet.”
Je, ni kwa malaika yupi ambaye Mungu amepata kumwambia wakati wowote, “Keti mkono wangu wa kuume, hadi nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako”?
14 What are the angels? They are beings that serve, sent out to help those who will receive salvation.
Je, malaika wote si roho watumikao, waliotumwa kuwahudumia wale watakaourithi wokovu?