< Habakkuk 1 >
1 This is the message that Habakkuk saw in vision.
Neno alilopokea nabii Habakuki.
2 Lord, how long do I have to cry out for help and you don't listen? I cry out, “Violence!” but you don't save us from it.
Ee Bwana, hata lini nitakuomba msaada, lakini wewe husikilizi? Au kukulilia, “Udhalimu!” Lakini hutaki kuokoa?
3 Why do you force me to see this wickedness and suffering? Why do you just observe such destruction and violence? Arguments and fighting happen right in front of me!
Kwa nini unanifanya nitazame dhuluma? Kwa nini unavumilia makosa? Uharibifu na udhalimu viko mbele yangu; kuna mabishano na mapambano kwa wingi.
4 As a result the law is paralyzed, and justice never wins. The wicked crowd out those who do right so that the course of justice is perverted.
Kwa hiyo sheria imepotoshwa, nayo haki haipo kabisa. Waovu wanawazunguka wenye haki, kwa hiyo haki imepotoshwa.
5 Look around at the nations, watch and be surprised and amazed. Something is going to happen in your time that you wouldn't believe even if you were told.
“Yatazame mataifa, uangalie na ushangae kabisa. Kwa sababu katika siku zako nitafanya kitu ambacho hungeamini, hata kama ungeambiwa.
6 Watch! I am raising up the Babylonians, a cruel and brutal people who will march across the world to seize other lands.
Nitawainua Wakaldayo, watu hao wakatili na wenye haraka, ambao hupita dunia yote kuteka mahali pa kuishi pasipo pao wenyewe.
7 They are fearsome and terrifying, and so proud of themselves that they set their own rules.
Ni watu wanoogopwa na wanaotisha; wenyewe ndio sheria yao, na huinua heshima yao wenyewe.
8 Their horses are faster than leopards and fiercer than hungry wolves. Their cavalry charges, racing in from far away. Like eagles, they swoop down to eat their prey.
Farasi wao ni wepesi kuliko chui, na wakali kuliko mbwa mwitu wakati wa machweo. Askari wapanda farasi wao huenda mbio; waendesha farasi wao wanatoka mbali. Wanaruka kasi kama tai ili kurarua;
9 Here they come, all intent on violence. Their armies advance in frontal assault as rapidly as the desert wind, capturing so many prisoners they are like sand.
wote wanakuja tayari kwa fujo. Makundi yao ya wajeuri yanasonga mbele kama upepo wa jangwani, na kukusanya wafungwa kama mchanga.
10 They mock kings and scoff at rulers. They laugh in scorn at fortresses—they pile up earth ramps and capture them.
Wanawabeza wafalme, na kuwadhihaki watawala. Wanaicheka miji yote iliyozungushiwa maboma; wanafanya malundo ya udongo na kuiteka hiyo miji.
11 Then they sweep on by like the wind and are gone. They are guilty because their own strength is their god.
Kisha wanapita kasi kama upepo na kusonga mbele: watu wenye hatia, ambao nguvu zao ndio mungu wao.”
12 Haven't you existed from eternity past? You are Lord my God, my Holy One, you do not die. Lord, you appointed them to execute judgment; God our Rock, you sent them to punish us.
Ee Bwana, je, wewe sio wa tangu milele? Mungu wangu, Uliye Mtakatifu wangu, hatutakufa. Ee Bwana, umewachagua wao ili watekeleze hukumu; Ee Mwamba, umewaamuru watuadhibu.
13 Your eyes are too pure to look upon evil; you cannot stand the sight of wrong. So why do you put up with untrustworthy people? Why are you silent when the wicked destroy those who do less evil than they do?
Macho yako ni safi mno hata yasiweze kuutazama uovu, wala huwezi kuvumilia makosa. Kwa nini basi unawavumilia wadanganyifu? Kwa nini unakuwa kimya wakati waovu wanawameza wale wenye haki kuliko wao wenyewe?
14 You make people become like fish in the sea, or like crawling insects, that have no ruler.
Umewafanya watu kama samaki baharini, kama viumbe wa bahari wasio na mtawala.
15 They drag everyone up with hooks, they pull them out with nets, catching them in dragnets. Then they happily celebrate.
Adui mwovu anawavuta wote kwa ndoana, anawakamata katika wavu wake, anawakusanya katika juya lake; kwa hiyo anashangilia na anafurahi.
16 They worship their nets as if they were gods, making sacrifices and burning incense to them, because by their nets they live in luxury, eating rich food.
Kwa hiyo anatoa kafara kwa wavu wake, na kuchoma uvumba kwa juya lake, kwa kuwa kwa wavu wake anaishi kwa starehe, na anafurahia chakula kizuri.
17 Will they keep on unsheathing their swords forever, killing nations without mercy?
Je, aendelee kuwatoa walio katika wavu wake, akiangamiza mataifa bila huruma?