< Genesis 5 >

1 This is the record of Adam's descendants. When God created human beings, he made them to be like him.
Hii ni orodha ya vizazi vya Adamu. Katika siku ambayo Mungu alimuumba mtu, aliwaumba katika mfano wake mwenyewe.
2 He created them male and female, and blessed them. On the day he created them he called them “human.”
Mwanaume na mwanamke aliwaumba. Akawabariki na akawaita Adam wakati walipoumbwa.
3 When Adam was 130, he had a son who was like him, made in his image; and he named him Seth.
Wakati Adamu alipokuwa ameishi miaka 130, akamzaa mwana katika sura yake mwenyewe, kwa mfano wake, na akamuita jina lake Sethi.
4 Adam lived another 800 years after Seth was born, and had other sons and daughters.
Baada ya Adamu kumzaa Sethi, aliishi miaka mia nane. Akawazaa wana wengi waume na wake.
5 Adam lived a total of 930 years, and then he died.
Adamu akaishi miaka 930 kisha akafariki.
6 When Seth was 105, he had Enosh.
Wakati Sethi alipokuwa ameishi miaka 105, akamzaa Enoshi.
7 Seth lived another 807 years after Enosh was born, and had other sons and daughters.
Baada ya kumzaa Enoshi, akaishi miaka 807 na akawazaa wana wengi waume na wake.
8 Seth lived a total of 912 years, and then he died.
Sethi akaishi miaka 912 kisha akafariki.
9 When Enosh was 90, he had Kenan.
Wakati Enoshi alipokuwa ameishi miaka tisini, akamzaa Kenani.
10 Enosh lived another 815 years after Kenan was born, and had other sons and daughters.
Baada ya kumzaa Kenani, Enoshi aliishi miaka 815. Akazaa wana wengi wa ume na wake.
11 Enosh lived a total of 905 years, and then he died.
Enoshi aliishi miaka 905 na kisha akafariki.
12 When Kenan was 70, he had Mehalalel.
Wakati Kanani alipokuwa ameishi miaka sabini, akamzaa Mahalaleli.
13 Kenan lived another 840 years after Mehalalel was born, and had other sons and daughters.
Baada ya kumzaa Mahalaleli, Kenani aliishi miaka 840. Akawazaa wana wengi wa ume na wake.
14 Kenan lived a total of 910 years, and then he died.
Kenani aliishi miaka 910, na kisha akafariki.
15 When Mahalalel was 65, he had Jared.
Mahalaleli alipokuwa ameishi miaka sitini na tano, alimzaa Yaredi.
16 After Jared was born, Mahalalel lived another 830 years and had other sons and daughters.
Baada ya kumzaa Yaredi, Mahalaleli aliishi miaka 830. Akazaa wana wengi wa ume na wake.
17 Mahalalel lived a total of 895 years, and then he died.
Mahalaleli aliishi miaka 895 na kisha akafariki.
18 When Jared was 162, he had Enoch.
Yaredi alipokuwa ameishi miaka 162, alimzaa Henoko.
19 After Enoch was born, Jared lived 800 years and had other sons and daughters.
Baada ya kumzaa Henoko, Yaredi aliishi miaka mianane. Akazaa wana wengi waume na wake.
20 Jared lived a total of 962 years, and then he died.
Yaredi aliishi miaka 962 na kisha akafariki.
21 When Enoch was 65, he had Methuselah.
Henoko alipokuwa ameishi miaka sitini na tano, akamzaa Methusela.
22 He had a close relationship with God. After Methuselah was born, Enoch lived another 300 years and had other sons and daughters.
Henoko akaenenda na Mungu miaka miatatu baada ya kumzaa Methusela. Aliwazaa wana wengi wa ume na wake.
23 Enoch lived a total of 365 years.
Henoko aliishi miaka 365.
24 Enoch had such a close relationship with God that he didn't die, he just wasn't there anymore, because God took him.
Henoko alienenda na Mungu, na kisha alitoweka, kwa kuwa Mungu alimtwaa.
25 When Methuselah was 187, he had Lamech.
Wakati Methusela alipokuwa ameishi miaka 187, alimzaa Lameki.
26 After Lamech was born, Methuselah lived another 782 years and had other sons and daughters.
Baada ya kumzaa Lameki, Methusela aliishi miaka 782. Akawazaa wana wengi wa ume na wake.
27 Methuselah lived a total of 969 years, and then he died.
Methusela aliishi miaka 969. Kisha akafariki.
28 When Lamech was 182, he had a son.
Wakati Lameki alipokuwa ameishi miaka 182, alimzaa mwana.
29 He named him Noah, with the explanation, “He will provide relief for us from all the hard manual labor we need to do in cultivating the ground the Lord has cursed.”
Akamuita jina lake Nuhu, akisema, “Huyu ndiye atatupatia pumziko kutoka katika kazi yetu na kutoka katika kazi ya taabu ya mikono yetu, ambayo lazima tuifanye kwa sababu ya ardhi ambayo Yahwe ameilaani.”
30 After Noah was born, Lamech lived another 595 years and had other sons and daughters.
Lameki aliishi miaka 595 baada ya kumzaa baba wa Nuhu. Akazaa wanawengi wa ume na wake.
31 Lamech lived a total of 777 years, and then he died.
Lameki aliishi miaka 777. Kisha akafariki.
32 Noah was 500 before he had Shem, Ham, and Japheth.
Baada ya Nuhu kuishi miaka miatano, akamzaa Shemu, Hamu, na Yafethi.

< Genesis 5 >