< Genesis 36 >
1 The following is the genealogy of Esau (also known as Edom).
Hivi ndivyo vizazi vya Esau (aliyeitwa pia Edom).
2 Esau married two Canaanite women: Adah, daughter of Elon the Hittite, and Oholibamah, daughter of Anah, and granddaughter of Zibeon the Hivite.
Esau akachukua wakeze kutoka kwa Wakanaani. Hawa walikuwa wake zake: Ada binti Eloni Mhiti; Oholibama binti Ana, mjukuu wa Zibeoni Mhivi; na
3 In addition he married Basemath, daughter of Ishmael and sister of Nebaioth.
Basemathi, binti Ishmaeli, dada wa Nebayothi.
4 Adah had a son for Esau named Eliphaz. Basemath had Reul.
Ada akamzaa Elifazi kwa Esau, na Basemathi akamzaa Reueli.
5 Oholibamah had Jeush, Jalam, and Korah. These were the sons of Esau, who were born to him in Canaan.
Oholibama akamzaa Yeushi, Yalamu, na Kora. Hawa walikuwa wana wa Esau waliozaliwa kwake katika nchi ya Kananaani.
6 Esau took his wives, sons and daughters, and everyone in his household, together with his livestock, all his other animals, and all the possessions he had gained while in Canaan, and went to live in a country far away from his brother Jacob.
Esau akawachukua wakeze, wanawe, binti zake, na watu wote wa nyumba yake, mifugo wake - wanyama wake wote, na mali yake yote, aliyokuwa amekusanya katika nchi ya Kanaani, na akaenda katika nchi iliyoko mbali kutoka kwa Yakobo nduguye.
7 He did this because the land they were living in couldn't support both of them with all their livestock.
Alifanya hivi kwa sababu mali zao zilikuwa nyingi sana kwa wao kuishi pamoja. Nchi waliyokuwa wamekaa isingeweza kuwafaa kwa mifugo yao.
8 Esau settled down in the hill country of Seir.
Hivyo Esau, aliyejulikana pia kama Edomu, akakaa katika nchi ya kilima Seiri.
9 The following is the genealogy of Esau, father of the Edomites, who lived in the hill country of Seir:
Hivi ndivyo vizazi vya Esau, babu wa Waedomu katika nchi ya mlima Seiri.
10 These were the names of Esau's sons: Eliphaz, son of Esau's wife Adah, and Reuel, son of Esau's wife Basemath.
Haya yalikuwa majina ya wana wa Esau: Elifazi mwana wa Ada, mkewe Esau; Reueli mwana wa Basemathi, mkewe Esau.
11 The sons of Eliphaz were: Teman, Omar, Zepho, Gatam, and Kenaz.
Wana wa Elifazi walikuwa Temani, Omari, Zefo, Gatamu, na Kenazi.
12 Timna, the concubine of Esau's son Eliphaz, had Amalek for Eliphaz. These were the descendants of Esau's wife Adah.
Timna, suria wa Elifazi, mwana wa Esau, akamzaa Amaleki. Hawa walikuwa wajukuu wa Ada, mkewe Esau.
13 These were the sons of Reuel: Nahath, Zerah, Shammah, and Mizzah. They were the descendants of Esau's wife Basemath.
Hawa walikuwa wana wa Reueli: Nahathi, Zera, Shama, na Miza. Hawa walikuwa wajukuu wa Basemathi, mkewe Esau.
14 These were the sons of Esau's wife Oholibamah, daughter of Anah and granddaughter of Zibeon, whom she had for Esau: Jeush, Jalam, and Korah.
Hawa walikuwa wana wa Oholibama, mkewe Esau, aliyekuwa binti Ana na mjukuu wa Zibeoni. Alimzalia Esau Yeushi, Yalamu, na Kora.
15 These were the tribal leaders of Esau's sons. The tribal leaders of the sons of Eliphaz (Esau's firstborn) were Teman, Omar, Zepho, Kenaz,
Hizi zilikuwa koo kati ya vizazi vya Esau: uzao wa Elifazi, mzaliwa wa kwanza wa Esau: Temani, Omari, Zefo, Kenazi, Kora,
16 Korah, Gatam, and Amalek. They were the tribal leaders of Eliphaz in the country of Edom, and they were the descendants of Adah.
Gatamu, na Amaleki. Hivi vilikuwa vizazi vya koo kutoka kwa Elifazi katika nchi ya Edomu. Walikuwa wajukuu wa Ada.
17 These were the sons of Esau's son Reuel: tribal leaders Nahath, Zerah, Shammah, and Mizzah. They were the tribal leaders descended from Reuel in the country of Edom, and they were the descendants of Esau's wife Basemath.
Hizi zilikuwa koo kutoka kwa Reueli, mwana wa Esau: Nahathi, Zera, Shama, Miza. Hizi zilikuwa koo kutoka kwa Reueli katika nchi ya Edomu. Walikuwa wajukuu wa Basemathi, mkewe Esau.
18 These were the sons of Esau's wife Oholibamah: tribal leaders Jeush, Jalam, and Korah; they were the tribal leaders descended from Esau's wife Oholibamah, daughter of Anah.
Hizi zilikuwa koo za Oholibama, mkewe Esau: Yeushi, Yalamu, Kora. Hizi ni koo zilizotoka kwa Oholibama mkewe Esau, binti Ana.
19 All these were the sons of Esau (also called Edom), and they were their tribal leaders.
Hawa walikuwa wana wa Esau na koo zao.
20 These were the sons of Seir the Horite, who were living in the country: Lotan, Shobal, Zibeon, Anah,
Hawa walikuwa wana wa Seiri Mhori, wenyeji wa nchi hiyo: Lotani, Shobali, Zibeoni, Ana,
21 Dishon, Ezer, and Dishan; they were the tribal leaders of the Horites, the descendants of Seir in the land of Edom.
Dishoni, Ezeri, na Dishani. Hizi zilikuwa koo the Wahori, wenyeji wa Seiri katika nchi ya Edomu.
22 The sons of Lotan were Hori and Hemam. Timna was Lotan's sister.
Wana wa Lotani walikuwa Hori na Hemani, na Timna alikuwa dada wa Lotani.
23 These were the sons of Shobal: Alvan, Manahath, Ebal, Shepho, and Onam.
Hawa walikuwa wana wa Shobali: Alvani, Manahathi, Ebali, Shefo, na Onamu.
24 These were the sons of Zibeon: Aiah and Anah. (This was the Anah who discovered the hot springs in the desert while he was looking after the donkeys of his father Zibeon.)
Hawa walikuwa wana wa Zibeoni: Aia na Ana. Huyu ndiye Ana aliyeona chemichemi za moto nyikani, alipokuwa akichunga punda wa Zibeoni babaye.
25 These were the children of Anah: Dishon and Oholibamah, daughter of Anah.
Hawa walikuwa watoto wa Ana: Dishoni na Oholibama, binti Ana.
26 These were the sons of Dishon: Hemdan, Eshban, Ithran, and Cheran.
Hawa walikuwa wana wa Dishoni: Hemdani, Eshbani, Ithrani, na Kerani.
27 These were the sons of Ezer: Bilhan, Zaavan, and Akan.
Hawa walikuwa wana wa Ezeri: Bilhani, Zaavani, na Akani.
28 These were the sons of Dishan: Uz and Aran.
Hawa walikuwa wana wa Dishani: Uzi na Arani.
29 These were the tribal leaders of the Horites: tribal leaders Lotan, Shobal, Zibeon, Anah,
Hizi zilikuwa koo za Wahori: Lotani, Shobali, Zibeoni, na Ana,
30 Dishon, Ezer, and Dishan. They were the tribal leaders of the Horites listed according to their tribes in the country of Seir.
Dishoni, Ezeri, Dishani: hizi zilikuwa koo za Wahori, kulingana na ukoo ulivyoorodheshwa katika nchi ya Seiri.
31 These were the kings who ruled in the land of Edom before there was any king who ruled over the Israelites:
Hawa walikuwa wafalme waliomiliki katika nchi ya Edomu kabla ya mfalme yeyote kumilika juu ya Waisraeli:
32 Bela, son of Beor, ruled in Edom and the name of his town was Dinhabah.
Bela mwana wa Beori, alitawala huko Edomu, na jina la mji wake lilikuwa Dinhaba.
33 When Bela died, Jobab, son of Zerah from Bozrah, took over as king.
Bela alipofariki, kisha Yobabu mwana wa Zera kutoka Bozra, akatawala mahali pake.
34 When Jobab died, Husham from the land of the Temanites took over as king.
Yobabu alipofariki, Hushamu aliyekuwa wa nchi ya Watemani, akatawala mahali pake.
35 When Husham died, Hadad, son of Bedad, took over as king. He was the one who defeated the Midianites in the country of Moab, and the name of his town was Avith.
Hushamu alipofariki, Hadadi mwana wa Bedadi aliyewashinda Wamidiani katika nchi ya Moabu, akatawala mahali pake. Jina la mji wake lilikuwa Avithi.
36 When Hadad died, Samlah from Masrekah took over as king.
Hadadi alipofariki, kisha Samla wa Masreka akatawala mahali pake.
37 When Samlah died, Shaul from Rehoboth on the Euphrates took over as king.
Samla alipofariki, kisha Shauli wa Rehobothi kando ya mto alitawala mahali pake.
38 When Shaul died, Baal-hanan, son of Achbor, took over as king.
Shauli alipofariki, kisha Baali Hanani mwana wa Akbori akatawala mahali pake.
39 When Baal-hanan, son of Achbor, died, Hadad took over as king. The name of his town was Pau, and his wife's name was Mehetabel, daughter of Matred, daughter of Me-zahab.
Baali Hanani mwana wa Akbori, alipokufa, kisha Hadari akatawala mahali pake. Jina la mji wake lilikuwa Pau. Jina la mkewe lilikuwa Mehetabeli, binti Matredi, mjukuu wa Me Zahabu.
40 These were the names of the tribal leaders descended from Esau, according to their families and where they lived, listed by name: tribal leaders Timna, Alvah, Jetheth,
Haya ndiyo yalikuwa majina ya wakuu wa koo kutoka uzao wa Esau, kwa kufuata koo zao na maeneo yao, kwa majina yao: Timna, Alva, Yethethi,
41 Oholibamah, Elah, Pinon,
Oholibama, Ela, Pinoni,
43 Magdiel, and Iram. These were the tribal leaders of Edom, listed according to the places where they lived in the country. Esau was the ancestor of the Edomites.
Magdieli, na Iramu. Hawa walikuwa wakuu wa ukoo wa Edomu, kwa kufuata makao yao katika nchi waliyomiliki. Nao ni Esau, baba wa Waedomu.