< Genesis 3 >
1 The serpent was more cunning than any of the other wild animals that the Lord God had made. He asked Eve, “Did God really say that you can't eat fruit from every tree in the garden?”
Basi nyoka alikuwa mwerevu kuliko wanyama wote wa porini ambao Bwana Mungu aliwafanya. Nyoka akamwambia mwanamke, “Ati kweli Mungu alisema, ‘Kamwe msile matunda ya mti wowote wa bustanini’?”
2 Eve replied to the serpent, “We can eat from the trees in the garden, but not the fruit from the tree in the middle of the garden.
Mwanamke akamjibu nyoka, “Tunaweza kula matunda ya miti iliyoko bustanini,
3 God told us, ‘You mustn't eat from that tree, or even touch it, otherwise you'll die.’”
lakini Mungu alisema, ‘Kamwe msile tunda la mti ulio katikati ya bustani, wala kuugusa, la sivyo mtakufa.’”
4 “You certainly won't die,” the serpent told Eve.
Lakini nyoka akamwambia mwanamke, “Hakika hamtakufa.
5 “It's because God knows that as soon as you eat it, you'll see things differently, and you'll be like God, knowing both what is good and what is evil.”
Kwa maana Mungu anajua ya kuwa wakati mtakapoyala, macho yenu yatafumbuliwa, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya.”
6 Eve saw that the fruit of the tree appeared good to eat. It looked very attractive. She really wanted it so she could become wise. So she took some of its fruit and ate it, and she gave some to her husband, who was with her, and he ate it too.
Mwanamke alipoona ya kuwa tunda la mti huo lilikuwa zuri kwa chakula na la kupendeza macho, tena linatamanika kwa kujipatia hekima, basi akachuma katika matunda yake, akala, pia akampa mumewe, aliyekuwa pamoja naye, naye akala.
7 Immediately they saw everything differently and realized they were naked. So they sewed fig leaves together to cover themselves up.
Ndipo macho yao wote wawili yakafumbuliwa, wakajiona kwamba walikuwa uchi; hivyo wakashona majani ya mtini, wakajifunika.
8 Later they heard the Lord walking in the garden in the evening when the breeze was blowing. Adam and Eve went and hid out of sight of the Lord God among the trees of the garden.
Ndipo yule mwanaume na mkewe, waliposikia sauti ya Bwana Mungu alipokuwa akitembea bustanini jioni, wakajificha kutoka mbele za Bwana Mungu katikati ya miti ya bustani.
9 The Lord God called out to Adam, “Where are you?”
Lakini Bwana Mungu akamwita Adamu, “Uko wapi?”
10 “I heard you walking in the garden and I was afraid because I was naked, so I hid,” he replied.
Naye akajibu, “Nilikusikia katika bustani nikaogopa kwa sababu nilikuwa uchi, hivyo nikajificha.”
11 “Who told you that you were naked?” asked the Lord God. “Did you eat fruit from the tree I ordered you not to?”
Mungu akamuuliza, “Ni nani aliyekuambia ya kuwa ulikuwa uchi? Je, umekula matunda ya mti niliokuamuru usile?”
12 “It was the woman you gave me who gave me the fruit from the tree, and I ate it,” Adam replied.
Adamu akasema, “Huyu mwanamke uliyenipa awe pamoja nami alinipa sehemu ya tunda kutoka kwenye huo mti, nami nikala.”
13 The Lord God asked Eve, “Why have you done this?” “The serpent tricked me, and so I ate it,” she replied.
Ndipo Bwana Mungu akamuuliza mwanamke, “Ni nini hili ambalo umelifanya?” Mwanamke akajibu, “Nyoka alinidanganya, nami nikala.”
14 Then the Lord God told the serpent, “Because of what you've done, you are cursed more than any of the other animals. You will slide along on your belly and eat dust as long as you live.
Hivyo Bwana Mungu akamwambia nyoka, “Kwa kuwa umefanya hili, “Umelaaniwa kuliko wanyama wote wa kufugwa na wa porini! Utatambaa kwa tumbo lako na kula mavumbi siku zote za maisha yako.
15 I will make sure you and your children, and the woman and her children, are enemies. One of her children will crush your head, and you will strike his heel.”
Nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na wake, yeye atakuponda kichwa, nawe utamuuma kisigino.”
16 He told Eve, “I will make pregnancy much more difficult, and giving birth will be very painful. However, you will still desire your husband, but he will have control over you.”
Kwa mwanamke akasema, “Nitakuzidishia sana utungu wakati wa kuzaa kwako; kwa utungu utazaa watoto. Tamaa yako itakuwa kwa mumeo naye atakutawala.”
17 He told Adam, “Because you did what your wife told you, and ate fruit from the tree after I ordered you, ‘Don't eat fruit from this tree,’ the ground is now cursed because of you. You will have to work painfully hard to grow food from it throughout your whole life.
Kwa Adamu akasema, “Kwa sababu umemsikiliza mke wako na ukala kutoka kwenye mti niliokuamuru, ‘Msile tunda lake,’ “Ardhi imelaaniwa kwa sababu yako, kwa kazi ngumu utakula chakula kitokacho humo siku zote za maisha yako.
18 It will grow thorns and thistles for you, and you will have to eat wild plants.
Itazaa miiba na mibaruti kwa ajili yako, nawe utakula mimea ya shambani.
19 You will have to sweat to grow enough food to eat until you die and return to the ground. For you were made from dust and you will return to dust.”
Kwa jasho la uso wako utakula chakula chako hadi utakaporudi ardhini, kwa kuwa ulitwaliwa kutoka humo, kwa kuwa wewe u mavumbi na mavumbini wewe utarudi.”
20 Adam named his wife Eve, because she was to be the mother of all human beings.
Adamu akamwita mkewe Eva, kwa kuwa atakuwa mama wa wote walio hai.
21 The Lord God made Adam and Eve clothes from animal skins and dressed them.
Bwana Mungu akawatengenezea Adamu na mkewe mavazi ya ngozi, akawavika.
22 Then the Lord God observed, “Look, the human beings have become like one of us, knowing both what is good and what is evil. Now if they take the fruit from the tree of life and eat it, then they'll live forever!”
Kisha Bwana Mungu akasema, “Sasa mtu huyu amekuwa kama mmoja wetu, kwa kujua mema na mabaya. Sharti asiruhusiwe kunyoosha mkono wake na kuchuma pia kutoka mti wa uzima akala, naye akaishi milele.”
23 So the Lord God expelled them from the Garden of Eden. He sent Adam to cultivate the ground from which he'd been made.
Hivyo Bwana Mungu akamfukuzia mbali kutoka Bustani ya Edeni, akalime ardhi ambamo alitolewa.
24 After he drove them out, the Lord God placed on the east side of the Garden of Eden angels and a sword that flashed in every direction. They were to prevent access to the tree of life.
Baada ya kumfukuzia mbali Adamu, Mungu akaweka makerubi mashariki ya Bustani ya Edeni, pamoja na upanga wa moto ukimulika huku na huko kulinda njia ya kuuendea mti wa uzima.