< Genesis 20 >

1 Abraham traveled towards the Negev, staying between Kadesh and Shur. After that he moved on to live in Gerar.
Basi Abrahamu akaendelea mbele kutoka huko hadi nchi ya Negebu na akaishi kati ya Kadeshi na Shuri. Kwa muda mfupi alikaa Gerari kama mgeni,
2 During his time there, when Abraham told people about his wife Sarah, he said, “She's my sister.” So Abimelech, king of Gerar, sent for Sarah and took her to become one of his wives.
huko Abrahamu akasema kuhusu Sara mkewe, “Huyu ni dada yangu.” Kisha Abimeleki mfalme wa Gerari akatuma Sara aletwe, naye akamchukua.
3 But God appeared to Abimelech in a dream and told him, “Listen! You're going to die because the woman you've taken is already married—she has a husband.”
Lakini Mungu akamjia Abimeleki katika ndoto wakati wa usiku na kumwambia, “Wewe ni kama mfu kwa sababu ya huyu mwanamke uliyemchukua; yeye ni mke wa mtu.”
4 Abimelech hadn't touched Sarah, and he asked, “Lord, do you kill good people?
Wakati huo Abimeleki alikuwa bado hajamsogelea, kwa hiyo akasema, “Je, Bwana utaliharibu taifa lisilo na hatia?
5 Didn't Abraham tell me himself, ‘She's my sister,’ and didn't Sarah also say, ‘He's my brother’? I did this in all innocence—my conscience is clear!”
Hakusema kwangu, ‘Huyu ni dada yangu,’ naye Sara pia hakusema, ‘Huyu ni kaka yangu’? Nimefanya haya kwa dhamiri njema na mikono safi.”
6 God told him in the dream, “Yes, I know you did this in all innocence, so I prevented you from sinning against me. That's why I didn't let you touch her.
Kisha Mungu akamwambia katika ndoto, “Ndiyo, najua ya kwamba umefanya haya kwa dhamiri safi, kwa hiyo nimekuzuia usinitende dhambi. Ndiyo sababu sikukuacha umguse.
7 Send the man's wife back to him. He's a prophet. He will pray for you, and you will live. But if you don't send her back to him, you should know for sure that you and all your family will die.”
Sasa umrudishe huyo mke wa mtu, kwa maana ni nabii, naye atakuombea nawe utaishi. Lakini kama hutamrudisha, ujue kwa hakika kuwa wewe na watu wako wote mtakufa.”
8 Abimelech got up early in the morning and called all his servants together. He explained everything that had happened, and they were all terrified.
Kesho yake asubuhi na mapema Abimeleki akawaita maafisa wake wote, na baada ya kuwaambia yote yaliyotokea, waliogopa sana.
9 Then Abimelech summoned Abraham and asked him “What have you done to us? How have I wronged you that you should treat me like this, bringing this terrible sin on me and my kingdom? You've done things to me that no one should ever do!”
Kisha Abimeleki akamwita Abrahamu na kumwambia, “Wewe umetufanyia nini? Nimekukosea nini hata ukaleta hatia kubwa namna hii juu yangu na ufalme wangu? Umenifanyia mambo ambayo hayakupasa kufanyika.”
10 Then Abimelech asked Abraham “What were you thinking when you did this?”
Abimeleki akamuuliza Abrahamu, “Ulikuwa na kusudi gani kufanya hivi?”
11 “Well, I thought to myself, ‘Nobody respects God in this place. They'll kill me just to get my wife,’” Abraham replied.
Abrahamu akajibu, “Niliwaza kwamba, ‘Hakika hakuna hofu ya Mungu mahali hapa, nao wataniua kwa sababu ya mke wangu.’
12 “Anyway, she really is my sister, the daughter of my father but not my mother, and I married her.
Pamoja na hayo, ni kweli kwamba yeye ni dada yangu, binti wa baba yangu ingawa si mtoto wa mama yangu; basi akawa mke wangu.
13 Since my God made me move far away from my family home, I told her, ‘If you really love me, then wherever you go with me you must tell people: He's my brother.’”
Wakati Bwana aliponifanya nisafiri mbali na nyumbani mwa baba yangu, nilimwambia, ‘Hivi ndivyo utakavyoonyesha pendo lako kwangu: Kila mahali tutakapokwenda, kuhusu mimi sema, “Huyu ni kaka yangu.”’”
14 Then Abimelech gave Abraham gifts of sheep, cattle, and male and female slaves, and returned his wife Sarah to him.
Kisha Abimeleki akatwaa kondoo na ngʼombe, na watumwa wa kiume na wa kike akampa Abrahamu, akamrudisha Sara kwa mumewe.
15 Abimelech told him, “Look over my land. You can choose to live anywhere you like.”
Abimeleki akasema, “Nchi yangu iko mbele yako, ishi popote unapotaka.”
16 Abimelech also told Sarah, “Notice that I'm giving your brother a thousand pieces of silver. This is to compensate you for the wrong done to you in the eyes of everyone with you, and to make sure that your name is publicly cleared.”
Akamwambia Sara, “Ninampa kaka yako shekeli elfu moja za fedha. Hii ni kufidia kosa lililofanyika dhidi yako mbele ya wote walio pamoja nawe; haki yako imethibitishwa kabisa.”
17 Then Abraham prayed to God, and God healed Abimelech, his wife, and his female slaves, so that they could have children again.
Kisha Abrahamu akamwomba Mungu, naye Mungu akamponya Abimeleki, mke wake, na watumwa wake wa kike kwamba waweze kupata watoto tena,
18 For the Lord had made all the women unable to have children because Abraham's wife, Sarah, had been taken.
kwa kuwa Bwana alikuwa ameyafunga matumbo ya wote katika nyumba ya Abimeleki kwa sababu ya Sara, mke wa Abrahamu.

< Genesis 20 >