< Genesis 18 >

1 The Lord appeared to Abraham at the oaks of Mamre. Abraham was sitting at the entrance to his tent as the day became really hot.
Yahwe alimtokea Abraham katika Mialoni ya Mamre, alipokua ameketi mlangoni pa hema wakati wa jua.
2 He looked up and all of a sudden he saw three men standing there. As soon as he saw them, he ran over to meet them and bowed low to the ground.
Akatazama juu na, tazama, akaona wanaume watatu wamesimama mbele yake. Alipo waona, alikimbia kupitia mlango wa hema kuwalaki na kuinama chini hadi ardhini.
3 He said, “Sir, if you please, don't continue your journey without spending some time here with me, your servant.
Akasema, “Bwana, kama nimepata upendelea machoni pako, nakuomba usinipite na kuniacha mtumishi wako.
4 Let me have some water brought so you can wash your feet and rest under the tree.
Naomba maji kidogo yaletwe, mnawe miguu yenu, na mjipumzishe chini ya mti.
5 Also let me bring some food so you can get your strength back before you go on your way, now that you've come to visit me here.” “That would be fine,” they answered. “Please do as you've suggested.”
Nami acha nilete chakula kidogo, ili kwamba mjiburudishe wenyewe. Ndipo baadae mwaweza kwenda zenu, kwa kuwa mmekuja kwa mtumishi wenu.” Nao wakasema, “Fanya kama ulivyo sema.”
6 Abraham hurried back to the tent and told Sarah, “Quick! Make some bread using three large measures of the best flour. Knead the dough and bake the bread.”
Kisha Abraham akaenda upesi hemani kwa Sara, na akasema, “Harakisha, chukua vipimo vitatu vya unga safi, uukande, na fanya mkate.”
7 Then Abraham ran to the cattle herd and chose a good, young calf and gave it to his servant who quickly killed and cooked it.
Kisha Abraham akakimbia kundini, akachukua ndama wa ng'ombe aliye laini na mzuri, na akampatia mtumishi na kwa haraka akamwandaa.
8 Then he took some yogurt, milk, and the cooked meat, and placed the food in front of them. He stood nearby under a tree while they ate.
Akatwaa siagi na maziwa na ndama aliye kwisha andaliwa, na akaweka chakula mbele yao, naye akasimama karibu nao chini ya mti wakati wanakula.
9 “Where is your wife Sarah?” they asked him. “Over there, inside the tent,” he replied.
Wakamwambia, “Mke wako Sara yuko wapi?” akajibu. “pale hemani.”
10 Then one said, “I promise you that I will come back to visit you about this time next year, and your wife Sarah will have a son.” Sarah was listening, hiding just inside the entrance to the tent behind him.
akasema, “Hakika nitarejea kwako majira ya machipuko, na tazama Sara mkeo atakuwa na mtoto wa kiume.” Sara alikuwa akisikiliza mlangoni pa hema iliyokuwa nyuma yake.
11 Abraham and Sarah were old, getting on in years. Sarah was well past the age of having children.
Abraham na Sara walikuwa wazee, umri wao ulikuwa umeendelea sana, na Sara alikuwa amepita umri ambao mwanamke anaweza kuzaa watoto.
12 Sarah was laughing inside, saying to herself, “Now that I'm old and worn out, how would I experience pleasure? My husband is old too!”
Kwa hiyo Sara akajicheka mwenyewe, akijisemesha mwenyewe, “baada ya kuwa nimechakaa na bwana wangu ni mzee, je ni tapata furaha hii?”
13 The Lord asked Abraham, “Why did Sarah laugh and ask, ‘How could it possibly be true that I'll have a child now I'm so old?’
Yahwe akamwambia Abraham, “Kwa nini Sara amecheka na kusema, Je ni kweli nitazaa mtoto, nikiwa mzee'?
14 Is anything too difficult for the Lord to do? I will come back next year when I said I would, in the spring, and Sarah will have a son.”
Je kuna jambo lolote gumu sana kwa Yahwe? Itakuwa katika wakati nilioweka mimi majira ya machipuko, nitarejea kwako. Majira haya mwakani Sara atakuwa na mtoto wa kiume.”
15 Sarah denied it because she was afraid, claiming, “I didn't laugh.” “Yes, you did laugh,” the Lord replied.
Kisha Sara akakataa na kusema, “sikucheka,” kwa kuwa aliogopa. Yahwe akasema, “hapana ulicheka.”
16 Then the men left. They looked down on Sodom and headed in that direction. Abraham accompanied them part of the way.
Kisha wale wanaume walisimama kuondoka na wakatazama chini kuelekea Sodoma. Abraham akafuatana nao kuona njia yao.
17 Then the Lord said, “Should I keep from Abraham what I'm going to do?
Lakini Yahwe akasema, Je ni mfiche Abraham kile ninacho kusudia kufanya,
18 Abraham will definitely become a great and powerful nation, and all the nations on earth will be blessed through him.
Ikiwa kwa hakika Abraham atakuwa mkuu na taifa lenye nguvu, na katika yeye mataifa yote ya dunia watabarikiwa?
19 I've chosen him so that he will teach his sons and their families to follow the way of the Lord by doing what is right and good, so that I, the Lord, can do for Abraham what I promised.”
Kwa kuwa nimemchagua ili awaelekeze wanawe na nyumba yake baada yake waishike njia ya Yahwe, watende utakatifu na haki, ili kwamba Yahwe ampatie Abraham yale aliyo yasema kwake.”
20 Then the Lord said, “There are many complaints made against Sodom and Gomorrah because they sin so blatantly.
Kisha Yahwe akasema, “Kwa sababu kilio cha Sodoma na Gomora ni kikuu, na kwa kuwa dhambi yao ni kubwa,
21 I ‘m going to see if these complaints that have reached me are completely true. I'll know if they're not.”
sasa nitashuka pale na kuona kilio kilicho nifikia dhidi yake, ikiwa kweli wamefanya au hawakufanya, nitajua.”
22 The two men turned and went towards Sodom, but the Lord stayed there with Abraham.
Kwa hiyo wale wanaume wakageuka toka pale, na kuelekea Sodoma, lakini Abraham akabaki amesimama mbele ya Yahwe.
23 Abraham came to him and asked: “Are you really going to wipe out the good people along with the wicked?
Kisha Abraham alikaribia na kusema, “Je utawafutilia mbali watakatifu pamoja na waovu?
24 What if there are fifty good people in the town? Are you still going to wipe it out despite the fifty good people there?
Huenda wakawepo wenye haki hamsini katika mji. Je utawakatilia mbali na usiuache mji kwa ajili ya hao watakatifu hamsini walioko hapo?
25 No, you can't do something like that! You can't kill the good with the wicked, otherwise you would be treating the good and the wicked in the same way. You can't do that! Isn't the Judge of all the earth going to do the right thing?”
Hasha usifanye hivyo, kuwauwa watakatifu pamoja na waovu, ili kwamba watakatifu watendewe sawa na waovu. Hasha! Je muhukumu wa ulimwengu wote hatatenda haki?”
26 “If I find fifty good people in Sodom, I'll spare the whole town because of them,” the Lord replied.
Yahwe akasema, “Katika Sodoma nikipata watakatifu hamsini kwenye mji, nita uacha mji wote kwa ajili ya hao.”
27 “Since I've started, let me go on speaking to my Lord, even though I'm nothing but dust and ashes,” Abraham continued.
Abraham akajibu na kusema, “Tazama, Nimeshika kusema na Bwana wangu, hata kama mimi ni mavumbi na majivu!
28 “What if there are forty-five good people, just five less? Are you still going to wipe out the whole town just because there are five fewer people?” “I won't destroy it if I find forty-five,” the Lord replied.
Itakuwaje ikiwa kuna watano pungufu katika idadi ya hao watakatifu hamsini? Je utaangamiza mji wote kwa upungufu wa hao watano?” Akasema, “Sitaangamiza, ikiwa nitapata watu arobaini na watano pale.”
29 Abraham spoke up again and he asked the Lord, “What if only forty can be found?” “I won't do it for the sake of the forty,” the Lord replied.
Akaongea naye tena, na kusema, “Itakuwaje ikiwa arobaini watapatikana pale?” Akajibu, “Sitafanya kwa ajili ya hao arobaini.”
30 “My Lord, please don't get angry with me,” Abraham went on. “Let me ask this—what if only thirty were found?” “I won't do it if I find thirty,” the Lord replied.
Akasema, Tafadhali usikasirike, Bwana, nikiongea. Pengine thelathini watapatikana pale.” Akajibu, 'Sitafanya, ikiwa nitapata thelathini pale.”
31 “I admit I've been very bold to speak to my Lord like this,” Abraham said. “What if only twenty are found there?” “I won't do it for the sake of the twenty,” the Lord replied.
Akasema, Tazama, Nimeshika kusema na Bwana wangu! Pengine ishirini watapatikana pale.” Akajibu, “Sitaharibu kwa ajili ya hao ishirini.”
32 “Please don't get angry with me, my Lord,” Abraham said. “Just let me ask one more thing. What if only ten are found there?” “I won't destroy it for the sake of the ten,” the Lord replied.
Akasema, “Tafadhali usikasirike, Bwana, na nitasema jambo hili kwa mara ya mwisho. Huenda kumi wakaonekana kule.” Na akasema, sitaangamiza kwa ajili ya hao kumi.”
33 The Lord left once he had finished speaking with Abraham, and Abraham went home.
Yahwe akaendelea na njia yake mara tu baada ya kumaliza kuongea na Abraham, na Abraham akarudi nyumbani.

< Genesis 18 >