< Genesis 18 >

1 The Lord appeared to Abraham at the oaks of Mamre. Abraham was sitting at the entrance to his tent as the day became really hot.
Bwana akamtokea Abrahamu karibu na mialoni ya Mamre wakati alipokuwa ameketi kwenye ingilio la hema lake wakati wa adhuhuri.
2 He looked up and all of a sudden he saw three men standing there. As soon as he saw them, he ran over to meet them and bowed low to the ground.
Abrahamu akainua macho akaona watu watatu wamesimama karibu naye. Alipowaona, aliharakisha kutoka kwenye ingilio la hema lake kuwalaki na kuwasujudia hadi nchi.
3 He said, “Sir, if you please, don't continue your journey without spending some time here with me, your servant.
Akasema, “Kama nimepata kibali machoni penu, ee bwana wangu, usimpite mtumishi wako.
4 Let me have some water brought so you can wash your feet and rest under the tree.
Acha yaletwe maji kidogo, kisha ninyi nyote mnawe miguu yenu na mpumzike chini ya mti huu.
5 Also let me bring some food so you can get your strength back before you go on your way, now that you've come to visit me here.” “That would be fine,” they answered. “Please do as you've suggested.”
Niruhusuni niwapatie chakula kidogo mle, ili mpate nguvu mwendelee na safari yenu, kwa kuwa mmekuja kwa mtumishi wenu.” Nao wakamjibu, “Vema sana, fanya kama unavyosema.”
6 Abraham hurried back to the tent and told Sarah, “Quick! Make some bread using three large measures of the best flour. Knead the dough and bake the bread.”
Hivyo Abrahamu akaharakisha akaingia hemani kwa Sara, akamwambia, “Chukua vipimo vitatu vya unga laini haraka, ukande na uoke mikate.”
7 Then Abraham ran to the cattle herd and chose a good, young calf and gave it to his servant who quickly killed and cooked it.
Kisha Abrahamu akakimbia kwenda kwenye kundi, akachagua ndama mzuri, laini na akampa mtumishi, ambaye aliharakisha kumtayarisha.
8 Then he took some yogurt, milk, and the cooked meat, and placed the food in front of them. He stood nearby under a tree while they ate.
Kisha akaleta jibini, maziwa na nyama ya yule ndama iliyoandaliwa, akaviweka mbele ya wageni. Walipokuwa wakila, alisimama karibu nao chini ya mti.
9 “Where is your wife Sarah?” they asked him. “Over there, inside the tent,” he replied.
Wakamuuliza, “Yuko wapi Sara mkeo?” Akasema, “Yuko huko, ndani ya hema.”
10 Then one said, “I promise you that I will come back to visit you about this time next year, and your wife Sarah will have a son.” Sarah was listening, hiding just inside the entrance to the tent behind him.
Kisha Bwana akasema, “Hakika nitakurudia tena majira kama haya mwakani na Sara mkeo atakuwa ana mwana.” Sara alikuwa akiwasikiliza kwenye ingilio la hema, lililokuwa nyuma yake.
11 Abraham and Sarah were old, getting on in years. Sarah was well past the age of having children.
Abrahamu na Sara walikuwa wazee tena waliosogea miaka, naye Sara alikuwa amekoma katika desturi ya wanawake.
12 Sarah was laughing inside, saying to herself, “Now that I'm old and worn out, how would I experience pleasure? My husband is old too!”
Hivyo Sara akacheka kimoyomoyo alipokuwa akiwaza, “Baada ya mimi kuwa mkongwe hivi na bwana wangu amezeeka, je, nitaweza kufurahia jambo hili?”
13 The Lord asked Abraham, “Why did Sarah laugh and ask, ‘How could it possibly be true that I'll have a child now I'm so old?’
Ndipo Bwana akamwambia Abrahamu, “Kwa nini Sara amecheka na kusema, ‘Kweli nitazaa mtoto nami sasa ni mzee?’
14 Is anything too difficult for the Lord to do? I will come back next year when I said I would, in the spring, and Sarah will have a son.”
Je, kuna jambo lolote gumu lisilowezekana kwa Bwana? Nitakurudia mwakani majira kama haya, naye Sara atakuwa na mwana.”
15 Sarah denied it because she was afraid, claiming, “I didn't laugh.” “Yes, you did laugh,” the Lord replied.
Sara akaogopa kwa kuwa alidanganya na kusema, “Mimi sikucheka.” Lakini Bwana akasema, “Ndiyo, ulicheka!”
16 Then the men left. They looked down on Sodom and headed in that direction. Abraham accompanied them part of the way.
Wakati watu hao waliposimama ili waondoke, walielekeza nyuso zao Sodoma, Abrahamu akawatoa kitambo kidogo ili awasindikize.
17 Then the Lord said, “Should I keep from Abraham what I'm going to do?
Ndipo Bwana akasema, “Je, nimfiche Abrahamu jambo ninalokusudia kufanya?
18 Abraham will definitely become a great and powerful nation, and all the nations on earth will be blessed through him.
Hakika Abrahamu atakuwa taifa kubwa na lenye nguvu, kupitia kwake mataifa yote ya dunia yatabarikiwa.
19 I've chosen him so that he will teach his sons and their families to follow the way of the Lord by doing what is right and good, so that I, the Lord, can do for Abraham what I promised.”
Kwa maana nimemchagua yeye, ili awaongoze watoto wake na jamaa yake kufuata njia ya Bwana, kwa kuwa waadilifu na kutenda haki, ili Bwana atimize ahadi yake kwa Abrahamu.”
20 Then the Lord said, “There are many complaints made against Sodom and Gomorrah because they sin so blatantly.
Basi Bwana akasema, “Kilio dhidi ya Sodoma na Gomora ni kikubwa sana na dhambi yao inasikitisha sana,
21 I ‘m going to see if these complaints that have reached me are completely true. I'll know if they're not.”
kwamba nitashuka nione kama waliyoyatenda ni mabaya kiasi cha kilio kilichonifikia. Kama sivyo, nitajua.”
22 The two men turned and went towards Sodom, but the Lord stayed there with Abraham.
Basi wale watu wakageuka wakaenda kuelekea Sodoma, lakini Abrahamu akabaki amesimama mbele za Bwana.
23 Abraham came to him and asked: “Are you really going to wipe out the good people along with the wicked?
Ndipo Abrahamu akamsogelea akasema: “Je, utawaangamiza wenye haki na waovu?
24 What if there are fifty good people in the town? Are you still going to wipe it out despite the fifty good people there?
Je, ikiwa watakuwepo watu wenye haki hamsini katika mji huo, hivi kweli utauangamiza na wala hutauacha kwa ajili ya hao watu hamsini wenye haki waliomo ndani yake?
25 No, you can't do something like that! You can't kill the good with the wicked, otherwise you would be treating the good and the wicked in the same way. You can't do that! Isn't the Judge of all the earth going to do the right thing?”
Hilo na liwe mbali nawe, kufanya jambo kama hilo, kuwaua wenye haki pamoja na waovu, kuwatendea wenye haki sawasawa na waovu. Iwe mbali nawe! Je, Mwamuzi wa dunia yote hatafanya lililo sawa?”
26 “If I find fifty good people in Sodom, I'll spare the whole town because of them,” the Lord replied.
Bwana akasema, “Kama nikipata watu hamsini wenye haki katika mji wa Sodoma, nitausamehe huo mji wote kwa ajili yao.”
27 “Since I've started, let me go on speaking to my Lord, even though I'm nothing but dust and ashes,” Abraham continued.
Kisha Abrahamu akasema tena: “Sasa kwa kuwa nimekuwa na ujasiri wa kuzungumza na Bwana, ingawa mimi si kitu bali ni mavumbi na majivu;
28 “What if there are forty-five good people, just five less? Are you still going to wipe out the whole town just because there are five fewer people?” “I won't destroy it if I find forty-five,” the Lord replied.
je, kama hesabu ya wenye haki imepungua watano katika hamsini, utauangamiza huo mji wote kwa ajili ya hao watano waliopungua?” Bwana akamwambia, “Kama nikiwakuta huko watu arobaini na watano, sitauangamiza.”
29 Abraham spoke up again and he asked the Lord, “What if only forty can be found?” “I won't do it for the sake of the forty,” the Lord replied.
Abrahamu akazungumza naye kwa mara nyingine, “Je, kama huko watapatikana watu arobaini tu?” Akamjibu, “Kwa ajili ya hao arobaini, sitauangamiza.”
30 “My Lord, please don't get angry with me,” Abraham went on. “Let me ask this—what if only thirty were found?” “I won't do it if I find thirty,” the Lord replied.
Ndipo akasema, “Bwana na asikasirike, lakini niruhusu nizungumze. Je, kama huko watakuwepo thelathini tu?” Akajibu, “Sitapaangamiza ikiwa nitawakuta huko watu thelathini.”
31 “I admit I've been very bold to speak to my Lord like this,” Abraham said. “What if only twenty are found there?” “I won't do it for the sake of the twenty,” the Lord replied.
Abrahamu akasema, “Sasa kwa kuwa nimekuwa na ujasiri sana kuzungumza na Bwana, je, kama wakipatikana huko watu ishirini tu?” Bwana akajibu, “Kwa ajili ya hao ishirini, sitauangamiza.”
32 “Please don't get angry with me, my Lord,” Abraham said. “Just let me ask one more thing. What if only ten are found there?” “I won't destroy it for the sake of the ten,” the Lord replied.
Abrahamu akasema, “Bwana na asikasirike, lakini niruhusu nizungumze tena mara moja tu. Itakuwaje kama watapatikana huko watu kumi tu?” Bwana akajibu, “Kwa ajili ya hao kumi, sitauangamiza.”
33 The Lord left once he had finished speaking with Abraham, and Abraham went home.
Bwana alipomaliza kuzungumza na Abrahamu, akaondoka, naye Abrahamu akarudi nyumbani kwake.

< Genesis 18 >